Na Juma Mohammed,MAELEZO Zanzibar
Watu 30 wakiwemo wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Mwanakwerekwe wakikabiliwa na makosa mbalimbali ikiwemo kuwashambulia Polisi,kuchoma moto matairi ya Magali barabarani na ukorofi.
Mbali na tuhuma hizo,pia wameshtakiwa kwa kufanya maandamano yasiyokuwa na kibali kinyume na sheria pamoja na uzembe na ukorofi wa kuwashambuliya polisi kwa mawe.
Watuhumiwa
hao walifikishwa katika mahakama nne tofauti, ikiwemo mahakama ya
hakimu Mohammed Ali Mohammed walikofikishwa watuhumiwa wawili, wanne kwa
hakimu Janet Nora Sekihola, 11 kwa hakimu Omar Mcha Hamza na 11
waliobakia, wamepandishwa mbele ya hakimu Valentine Andrew Katema.
Kwa
nyakati tofauti watuhumiwa hao walishitakiwa kwa makosa ya kufanya
mikusanyiko isivyo halali, uzembe na ukorofi pamoja kufanya kitendo
kinachoweza kuleta uvunjifu wa amani.
Watuhumiwa
hao ni Mbarouk Said Khalfani (45), na Mussa Juma Issa (57) wanaodaiwa
kuwa ni viongozi wa Jumuiya hiyo, ambapo walifikishwa mbele ya hakimu
Mohammed Ali Mohammed, na kusomewa shitaka la kufanya mkusanyiko isivyo
halali kinyume na kifungu cha 55 (1) (2) (3) na kifungu cha 56 cha
sheria namba 6/2004 sheria za Zanzibar.
Wengine
ni Mbwana Hamadi Juma (50), Massoud Hamadi Mohammed (17), Mohammed Juma
Salum (35), Abdulrahman Simai Khatib (19), Hashim Juma Issa (54) Matar
Fadhil Issa (54).










































