Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akimuangalia Sheha wa Shehia ya Tomondo Wilaya ya Magharibi Unguja,Mohamed Saidi Kidevu,(kulia) jinsi alivyoathirika na Tindikali alilomwagiwa na Mtu asiyejuilikanwa huko Tomondo juzi wakati alipokuwa akirudi kuchota maji na kuelekea nyumbani kwake,Sheha huyo yupo katika Hospitali ya Mnazi mmoja kwa matibabu,wa kushoto Dk.Slim Mohamed Mgeni,[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Sheha wa Shehia ya Tomondo Wilaya ya Magharibi Unguja,Mohamed Saidi Kidevu,(kulia) aliyetiwa Tindikali na Mtu asiyejuilikanwa huko Tomondo juzi wakati alipokuwa akirudi kuchota maji na kuelekea nyumbani kwake,Sheha huyo yupo katika Hospitali ya Mnazi mmoja kwa matibabu,wa pili kulia Kaka yake Sheha Sudu Mgeni Saidi.[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]
Rais dkt Shein amtembelea Sheha Aliyetiwa Tindi kali
RATIBA YA SHEREHE ZA AU KESHO – KARIMJEE HALL
TENTATIVE PROGRAMME FOR THE CELEBRATIONS OF THE OAU/AU GOLDEN JUBILEE ON 25th MAY, 2013
Venue - Karimjee Hall
Guest of Honour - Hon. Bernard Kamillius Membe (MP)
Minister for Foreign Affairs and International Cooperation
|
TIME |
EVENT |
RESPONSIBLE INSTITUTION |
|
8.00 |
Arrival at the Ministry |
All |
|
8.30 |
Lighting of the OAU/AU Torch |
Hon. Membe-Minister for Foreign Affairs and International Cooperation |
|
8.35 |
Festive Procession led by Brass Band |
Invitees |
|
8.45 |
Arrival at the Karimjee Hall |
Invitees |
|
8.50-9.10 |
Folk Dances |
Dance Troupes |
|
9.15-9.25 |
Playing of the AU and the Tanzania Anthems |
Brass Band |
|
9.30-10.00 |
Opening Remarks |
Guest of Honour (Hon. Membe)
|
|
10.10-11.20 |
Panel Discussion-Pan Africanism and African Renaissance |
Key Speakers: Amb. W. M. Mangachi & Mme Tonia Kandiero Moderator: Prof. A. Mhina |
|
11.40-12.50 |
Panel Discussion-OAU/AU’s Role in the Liberation Struggle and Self-determination |
Key Speakers: Amb. A. Kiwanuka & Amb. T.H. Chiliza Moderator: Amb. M. Maundi |
|
12.50 |
Closing Remarks |
Dean of the African Diplomatic Group |
|
12.50 |
Folk Dances |
Dance Troupes |
|
13.00 |
Luncheon |
Caterer |
RAIS JAKAYA KIKWETE AFUNGUA MAONYESHO YA MFUMO WA MATOKEO MAKUBWA ‘SASA’ AWAMU YA KWANZA
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwa kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa wakati wa Ufunguzi rasmi wa Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa ‘Sasa’ Awamu ya Kwanza leo Mei 24, 2013. Picha na OMR
Msanii maarufu wa kughani, Mrisho Mpoto, wakibinjuka Sarakasi, wakati kikundi chake na Bendi yake ya Mjomba ilipokuwa ikitoa burudani katika Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa ‘Sasa’ Awamu ya Kwanza, yaliyofunguliwa na Rais Jakaya Kikwete, leo Mei 24, 2013. Picha na OMR
MWanamuziki wa Bendi ya Mjomba, wakiimba kutoa burudani katika Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa ‘Sasa’ Awamu ya Kwanza, yaliyofunguliwa na Rais Jakaya Kikwete, leo Mei 24, 2013. Picha na OMR
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwasili kwenye Ukumbi wa Jumba la Makumbusho ya Taifa, leo Mei 24, 2013 kwa ajili ya Kufungua rasmi Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa ‘Sasa’ Awamu ya kwanza. Picha na OMR
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwasili kwenye Ukumbi wa Jumba la Makumbusho ya Taifa, leo Mei 24, 2013 kwa ajili ya Kufungua rasmi Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa ‘Sasa’ Awamu ya kwanza. Picha na OMR
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwasili kwenye Ukumbi wa Jumba la Makumbusho ya Taifa, leo Mei 24, 2013 kwa ajili ya Kufungua rasmi Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa ‘Sasa’ Awamu ya kwanza. Picha na OMR
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakisikiliza maelezo kutoka kwa Mchambuzi Sera Mkuu wa Ofisi ya Rais na Mipango, Lorah Madete, wakati walipokuwa wakitembelea Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa Awamu ya Kwanza, baada ya kuyafungua rasmi leo katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es Salaam. Picha na OMR
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakisikiliza maelezo kutoka kwa Ofisa Mtafiti Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Dkt. Mary Shetto, wakati walipokuwa wakitembelea Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa Awamu ya Kwanza, baada ya kuyafungua rasmi leo katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es Salaam. Picha na OMR
PICHA ZA MBWA WALIOPATA MAFUNZO YA KUKABILI UHALIFU
Mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya Mbwa akionyesha umahiri wake wa kutumia mnyama huyo mara baada ya kupatiwa mafunzo ya kutumia mbwa Kwa ajili ya kuzuia uhalifu na kikiosi cha mbwa na farasi cha Jeshi la Polisi mafunzo hayo yalifanyika jijini Dar es salaam. (Picha na Hassan Mndeme- Jeshi la Polisi)
Mbwa wa kiraia aliyepatiwa mafunzo na Jeshi la Polisi ya namna ya kukabiliana na uhalifu na wahalifu wanaobeba madawa ya kulevya hususani bangi.(Picha na Hassan Mndeme- Jeshi la Polisi
Mmoja wa wahitimu wa kike aliyepata mafunzo ya Polisi jamii na ulinzi shirikishi alipata mafunzo ya ukakamavu kwa ajili ya kukabiliana na uhalifu na wahalifu, mafunzo hayo yalifanyika jijini Dar es salaam katika viwanja vya kikosi cha mbwa na farasi cha jeshi la Polisi.( Picha na Hassan Mndeme- Jeshi la Polisi)
JESHI LA POLISI LAMTIA MBARONI MCHOCHEZI WA VURUGU NA FUJO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA
Anuani ya Simu “MKUUPOLISI” Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi,
Simu : (022) 2110734 Makao Makuu ya Polisi,
Fax Na. (022) 2135556 S.L.P. 9141,
Unapojibu tafadhali taja: DAR ES SALAAM.
24 MAY 2013
TAARIFA YA JESHI LA POLISI KWA VYOMBO VYA HABARI
Jeshi la Polisi Nchini linamshikilia mtu mmoja ambaye jina lake linahifadhiwa kwa sababu za kiupelelezi kwa tuhuma za kueneza ujumbe wa uchochezi na chuki kwa wananchi na viongozi wa serikali kwa njia ya simu ya mkononi akituma SMS kwa lengo la kuchochea fujo, vurugu na kutoa matusi kwa viongozi hao.
Mtu huyo amekuwa akifanikisha kazi hiyo kwa kutumia Chips (sim card) 13 za simu za mkononi ambazo amekamatwa nazo. Jeshi la Polisi linaendelea kumhoji mtu huyo na ushahidi utakapokamilika atafikishwa mahakamani.
Aidha, Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi wenye taarifa zingine za wahahlifu kama hao kujitokeza na kutoa taarifa hizo polisi ili wahalifu hao waweze kukamatwa na kuchukuliwa hatua stahiki, wakiwemo watu wanaowashawishi wenzao kwa njia ya fedha, kuwashauri ama kuwasaidia kwa namna yeyote ile katika kufanikisha uhalifu huo na kusababisha uvunjifu wa amani hapa nchini.
Jeshi la polisi halitasita kumchukulia hatua mtu yeyote atakayebainika kuvunja sheria za nchi.
Imetolewa na:-
Advera Senso-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
SERIKALI: WACHIMBAJI WA MADINI WAACHE KUVAMIA MAENEO YA WAWEKEZAJI
Na Lydia Churi, MAELEZO-DODOMA
Serikali imewataka wachimbaji wote wa madini nchini wanaovamia maeneo ya wawekezaji wengine kuacha kufanya vitendo hivyo na badala yake waendeleze maeneo wanayomiliki kwa mujibu wa sheria.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini (Madini) Steven Masele alisema tabia ya uvamizi wa leseni kubwa za utafiti unatishia nchi yetu kukosa miradi mikubwa ya migodi mipya katika siku za usoni.
Akijibu swali la msingi lililoulizwa na mbunge wa Kishapu, Mheshimiwa Suleiman Nchambi aliyetaka kujua mpango wa serikali kuwasaidia mitaji na nyenzo za kufanyia kazi wachimbaji wadogo Mhe. Masele alisema serikali inatambua na kuthamini mchango wa wachimbaji hao katika kuinua uchumi na pato la taifa pamoja na kutoa ajira kwa watanzania wengi.
Alisema inakadiriwa kuwa watanzania milioni moja wanajishughulisha na kazi ya uchimbaji wa madini nchini na kutokana na hilo serikali kuanzia mwaka wa fedha wa 2009/2010 ilianzisha mpango wa kutenga fedha kwa ajili ya kutoa mikopo kwa wachimbaji wadogo ili waweze kununua vifaa bora vya uchimbaji na uongezaji thamani madini.
Amewashauri wachimbaji wadogo nchini kuungana ili iwe rahisi kukopesheka kupitia utaratibu ulioandaliwa na serikali. Aidha amewashauri wachimbaji wadogo kuomba mikopo kupitia taasisi nyingine za kifedha kama vile benki na kuhakikisha wanatimiza vigezo vinavyotakiwa na taasisi husika.
Akizungumzia vurugu zilizotokea jana baina ya wachimbaji wadogo na STAMICO huko Buhemba mkoani Mara, Mhe. Masele amewataka wananchi wa eneo hilo kuwa wavumilivu wakati serikali ikiangalia namna ya kutatua tatizo hilo.
MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI MJINI DODOMA LEO
Waziri wa Katiba na Sheria,Mh Mathias Chikawe (kushoto), Mbunge wa Sengerema,Mh William Ngeleja na Mbunge wa Peramio, Mh Jenister Mhagama wakifurahi jambo wakati wakitoka ndani ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma jana. Picha zote na Zawadi Msalla wa MAELEZO.
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mh Samuel Sitta akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka 2013/14 Bungeni mjini Dodoma.
PHELAN NA STEELE KIBARUA CHAO KUOTA NYASI UNITED, MOYES AMTAKA KOCHA WA EVERTON KUMSAIDIA MAJUKUMU!!
Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Kocha msaidizi wa mabingwa wa soka nchini Uingereza, Manchester United Mike Phelan na kocha wa makipa Eric Steele wamejawa na wasiwasi wa kibarua chao kuota nyasi kufuatia ujio mpya wa kocha wa united David Moyes ambaye anasemekana ana mipango ya kumleta kocha mwenza wa Everton Jimmy Lumsden kuwa msaidizi wake katika safari yake ya kuifundisha klabu yake mpya.
Nafasi ya Phelan amekuwa hatarini tangu United imtangaze Moyes kuwa mrithi wa mikoba ya kibabu Alexndar Chapman Ferguson kwani kocha huyo anaonekana kuwa na nia ya kumleta kocha Lumsden ili kuenda sambamba kuijenga United mpya.
Moyes alikutana na Phelon jumanne ya wiki hii wakiwa na Ferguson, Steele na kocha wa sasa wa United Rene Muelensteen katika uwanja wa mazoezi wa Carrington ambapo Moyes alisema leo Ijumaa ataanika mipango yake pamoja na kumtaja msaidizi wake.
KITUMBUA KINAINGIA MCHANGA: Mike Phelan aliteuliwa na Ferguson kuwa msaidizi wake septemba mwaka 2008
ANASEPA ZAKE: Kocha wa makipa Eric Steele (wambele) anasemekana kutimka zake baada ya ujio wa David Moyes
MWISHO WA KAZI: Phelan inawezekana ubingwa wa msimu uliomalizika mei 18 ukawa wa mwisho kukaa Old Trafford
Mike Phelan inawezekana haya ndiyo matembezi ya mwishoni OT kufutaia kocha Moyes kumhitaji kocha wa Everton kuwa msaidizi
David Moyes anarithi mikoba ya Sir Alex Ferguson
The National Assembly in Collaboration with the UNDP under the Legislative Support Project Conducted a one day workshop to Mps and Staff on Social and Economic Policies
One of the Presenter at the workshop on Social and economic Policies, Economic growth and development to the Members of the National Assembly Dr. Haji Semboja from the University of Dar es Salaam, presenting a topic on importance of social economic policies in the budget process for sustainable economic growth and development. The workshop was organized by the office of The National Assembly in Collaboration with the UNDP under the Legislative Support Project
Mr. Hassan Abdallh from Social and Economic Research Foundation presenting the topic on skills and techniques required by Mps and Staff in using social and economic policies during the Budget process
Prof. Faustin Kamuzora from Mzumbe University giving outline of what is Challenges facing economic growth and development in Tanzania during the workshop
Cross section of Mps listening to the presentations attentively during the workshop
Cross section of Mps listening to the presentations attentively during the workshop
Cross section of Mps listening to the presentations attentively during the workshop
Cross section of Mps listening to the presentations attentively during the workshop
Moderator of the workshop who is also a Chairperson of the Standing Committee on Local Government Hon. Dr. Hamis Kigwangala giving some comments
Hon. Madabida giving her contribution to the presenters
Hon. Suleman Zedi curiously posing a question to the presenter during the workshop
Hon. Athuman Mfutakamba giving some statistics on how good policies can improve the country’s development
SEMINA YA USAJILI- TMS KUFANYIKA MEI 25!!
Na Boniface Wambura
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeandaa semina ya usajili kwa njia ya mtandao (Transfer Matching System-TMS) kwa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom kwa ajili ya msimu wa 2013/2014.
Semina hiyo itafanyika Jumamosi (Mei 25 mwaka huu) kwenye ofisi za TFF saa 3 kamili asubuhi ikishirikisha watu wawili kutoka kila klabu ambao ni TMS Manager, na ofisa mwingine wa klabu.
Klabu za ligi hiyo zinazotakiwa kuhudhuria semina ya usajili ni Ashanti United, Azam, Coastal Union, JKT Ruvu, Kagera Sugar, Mbeya City, Mgambo Shooting, Mtibwa Sugar, Oljoro JKT, Rhino Rangers, Ruvu Shooting, Simba, Tanzania Prisons na Yanga.
TFF YASEMA WENYEVITI WA VYAMA VYA MIKOA NDIYO WASIMAMIZI RCL!!
Na Boniface Wambura, TFF
Wakati mechi za kwanza za raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) zinachezwa wikiendi hii, Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imesisitiza kuwa wasimamizi wa mechi za ligi hiyo ni wenyeviti wa mikoa wa vyama vya mpira wa miguu.
Kamati hiyo chini ya uenyekiti wa Ramadhan Nassib ilikutana jana (Mei 23 mwaka huu) kupitia ripoti za makamishna kwa mechi za raundi ya kwanza ya RCL iliyomalizika wikiendi ya Mei 18 na 19 mwaka huu.
Kuhusu viwanja vinavyotumika kwa ligi hiyo, Kamati imesema vitaendelea kuwa vile vya makao makuu ya mikoa, na kwa vile vilivyokuwa vimeombwa vifanyiwe marekebisho ili viweze kukaguliwa kwa ajili ya RCL msimu ujao. Pia imeitaka mikoa kuendelea kuboresha viwanja vinavyotumika sasa, lakini vina upungufu.
Vilevile Kamati imebaini kuwa zimekuwepo pingamizi kuhusu usajili wa wachezaji ambapo imesema haiwezi kujadili pingamizi hizo kwa vile mikoa yote haikuwasilisha usajili wa wachezaji wa klabu husika uliofanyika mikoani kama ilivyoagizwa na kuelekezwa na TFF.
Hata hivyo, Kamati imeitaka mikoa ambayo klabu zao zimefanikiwa kuingia raundi ya pili kuwasilisha usajili huo haraka.
Pia Kamati imebaini kuwa zipo baadhi ya klabu ambazo zimekata rufani kuhusu usajili wa baadhi ya wachezaji, na kusisitiza kilichowasilishwa ni pingamizi kwa vile kwa mujibu wa kanuni masuala ya uwanjani hayakatiwi rufani. Hivyo, Kamati imeshauri klabu zilizokata rufani zilirejeshewe ada zilizolipa kwa ajili hiyo.
Makamishna na waamuzi wanaosimamia mechi za RCL wamekumbushwa kuwa ili mchezaji aruhusiwe kucheza mechi ni lazima awe na leseni yake (kadi ya usajili), vinginevyo asiruhusiwe kucheza mechi husika.
Mechi za RCL zinaendelea wikiendi hii ambapo zote zitachezwa Jumapili (Mei 26 mwaka huu) isipokuwa mechi kati ya Friends Rangers ya Dar es Salaam na African Sports ya Tanga itakayochezwa Jumamosi (Mei 25 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi.
Nayo mechi kati ya Abajalo ya Dar es Salaam na Kariakoo ya Lindi iliyokuwa ichezwe Jumamosi kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam sasa itachezwa Jumapili kwa vile siku hiyo uwanja huo utatumika kwa mazoezi ya Taifa Stars.
Mechi nyingine za RCL zitakazochezwa Mei 26 mwaka huu ni Machava FC ya Kilimanjaro dhidi ya Mpwapwa Stars ya Dodoma kwenye Uwanja wa Ushirika mjini Moshi, Stand United FC ya Shinyanga itakuwa mgeni wa Magic Pressure ya Singida kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida.
Polisi Jamii ya Bunda mkoani Mara na Biharamulo FC ya Kagera zitaumana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma. Mjini Kigoma kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika ni kati ya wenyeji Saigon FC na Katavi Warriors ya Katavi.
Nayo Kimondo SC ya Mbeya itakuwa mgeni wa Njombe Mji ya Njombe katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe. Mechi za marudiano zitachezwa kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu.
Timu zitakazofuzu kucheza raundi ya tatu zitacheza mechi za kwanza kati ya Juni 8 na 9 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitakuwa kati ya Juni 15 na 16 mwaka huu.
KIEMBA AKUBALI KUSAINI MSIMBAZI, KASEJA MAZUNGUMZO YAENDELEA, KAPOMBE BADO ANA MKATABA!!
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Kiungo matata wa wekundu wa Msimbazi Simba, Amri Athman Kiemba amekubali kuongeza mkataba wa kuichezea klabu hiyo kwa msimu ujao wa ligi kuu soka Tanzania bara.
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Keptein Zacharia Hans Poppe ameimabia FULLSHANGWE kuwa Amri Kiemba wameshazungumza nae na kukubaliana kuongeza mkataba wake jambo ambalo limewapa raha sana kutokana na ubora wa mchezaji huyo aliyekuwa akitajwa kuihama Simba na kujiunga na Yanga msimu ujao.
“Kuhusu Kiemba tumeshaziba midomo ya watu, amekubali kwa moyo mkunjufu kuitumikia klabu yake msimu ujao, ni bonge la mchezaji, tunafurahi kuwa nae katika kikosi chetu”. Alisema Poppe.
Kuhusu nahodha Juma Kaseja, Poppe alisema wanaendelea kuzungumza nae ili kumsainisha mkataba mwingine huku wakikubaliana kuboresha maslahi yake klabuni hapo.
“Kuna watu wanazungumza na Kaseja, nadhani wanaendelea vizuri na mimi nitakutana nae tumalizane, haondoki ng`oo, atakuwepo Simba, cha msingi mashabiki wa Simba wawe watulivu”. Alisema Poppe.
Kuhus suala la Shomary Kapombe, Poppe amewatoa mashabiki wa kuwa mchezaji huyo bado ana mkataba na Simba hadi aprili mwakani na ataendelea kubaki msimbazi.
“Wanamsimbazi wasiwe na wasiwasi, Kapombe ni wetu na kila kitu kipo sawa”. Alisema Poppe.
Poppe alisema baada ya vijana hao kurudi kutoka Morocco wanapokwenda kuitumikia timu ya taifa, watasaini mikataba minono zaidi.
Kwa upande mwingine, Hans Poppe alisema zoezi la kuwasainisha mikataba mipya wachezaji wote wa timu hiyo linaendelea vizuri, ikiwemo wale waliopandishwa kutoka kikosi cha pili, yaani Simba B.
Poppe aliongeza kuwa mwaka huu wanahitaji kufanya mambo yao kimya kimya ili kuwazuia wale wasiojua kusaka wachezaji ila wakijua Simba wamempa nani wanakimbilia kuwasainisha.
“Tunataka kuongeza wachezaji wengine wapya ili kuongeza nguvu ya kikosi, safari hii tunafanya kimyakimya kuwazuia ndugu zetu wasiojua kutafuta wachezaji na kufanya hesabu
TANZANIA,KENYA ZAVUTANA JUU YA VIJANA WALIOUWAWA NAROK
MIILI mitatu ya watanzania wa jamii ya Kisonjo waliouwawa katika eneo la Narok wilayani Kajiado nchini Kenya imeingia katika sura mpya mara baada ya Serikali ya Tanzania kushindwa kuirejesha nchini miili hiyo huku serikali ya Kenya ikidai kuwa hawakuwa watanzania
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas alisema kuwa tayari mtu mmoja ambaye ni askari polisi anashikiliwa na jeshi hilo kwa uchunguzi zaidi ingawaje alisema kwa sasa jina la askari huyo linahifadhiwa kwa ajili ya upelelezi
Sabas alisema kuwa wanamshikilia askari huyo kwa kosa la upotevu wa silaha ambayo inasadikiwa kuwa ilitumika katika tukio uhalifu linalohusishwa na mauji ya vijana hao watatu wa Kitanzania nchini Kenya.
Kuhusu Marehemu hao, kamanda amesema kuwa Serikali ya Kenya kupitia Jeshi lake la polisi ndio wanajukumu la kurejesha Miili yao hapa nchini .
Awali Msemaji wa familia tatu za marehemu hao,Pasto Webo alidai kuwa askari wa kituo cha polisi Loliondo waliwatoza kiasi Milioni mbili na nusu kwa ikiwa kama gharama za kuwasafirisha marehemu kutoka kenya kwa gari la Polisi kwa kiwango cha shilingi laki nane kwa kila mwili mmoja.
Lakini Kamanda wa Polisi alisema kuwa Jeshi hilo halina utaratibu wa kusafirisha marehemu na kwamba anafuatilia madai hayo na itakapobainika kuwa ni kweli watachukuliwa hatua kali za kisheria.
Kuhusu kuhusika kwa polisi wa loliondo na kupotea kwa vijana wao watatu msemaji wa familia hizo tatu alidai kuwa May tatu mtoto wake ambaye ni Tibiti webo alikuja nyumbani kwake akiwa na askari polisi ambaye anajulikana kwa jina la Lazaro ambapo walikula chakula na walipoondoka kwa pamoja kijana huyo hakuonekana tena.
Pia alidai inasemekana kuwa kijana huyo alimpitia rafiki yake ambaye amejulikana kwa jina la Kadogo anna ambapo tangu alipoondoka tarehe tatu mwezi huu hawakuonekana tena mpaka hivi karibuni polisi walipowaletea ripoti pamoja na picha kuwa vijana wao wameuwawa vibaya Narok
“Tulipotazama hizo picha tuliweza kuwatambua vijana wetu wawili lakini pia alikuwepo mwingine wa tatu ambaye tunadhani kuwa anatokea kijiji cha jirani”
Inadaiwa kuwa polisi waliwaeleza kuwa vijana wao waliuwawa katika tukio la ujambazi katika eneo la Narrok ambapo ilidaiwa kuwa waliwavamia wafanyabiashara kwa ajili ya kuwapora fedha lakini wakauwawa na wananchi wenye hasira kali
Katika tukio hilo vijana hao walikutwa na silaha ambayo inaaminika kuwa walipewa na askari wa kituo cha polisi cha loliondo.
Akizungumza kwa njia ya simu kutoka Dar es salam balozi wa Kenya Nchini Tanzania ,Mutinda Mutiso alidai kuwa vijana waliouwa sio watanzania bali ni wa Kenya huku akiongeza kuwa tukio hilo lilitokea wakati yeye akiwa nchini humo.
MRADI WA UENDELEZAJI MIJI TANZANIA (TSCP) WAENDELEA VIZURI
Wawakilishi wa Mradi wa TSCP na Wawakilishi wa World Bank katika picha ya pamoja, hivi karibuni walipotembelea Mwanza katika kubaini utekelezaji na maendeleo ya maeneo mbalimbali ya mradi huo.JPG
Timu ya wataalamu kutoka OWM-TAMISEMI-katika Mradi wa Mpango Miji Mkakati (TSCP ) Pamoja na wawakilishi kutoka Benki ya Dunia pamoja na Ubalozi wa Denmak wakikagua Ujenzi wa Barabara zinazoendelea kujengwa kupitia mradi wa TSCP katka Mnispaa ya Mtwara Mikindani katika kubaini utekelezaji na maendeleo ya maeneo mbalimbali ya mradi
Hii ni baadhi ya mifereji iliyokamilika baada ya ujenzi huko Tanga.
………………………………………………………….
Toka uzinduzi wa mradi wa uendelezaji Miji. Tanzania Strategic Cities Project (TSCP),uanze
mnamo mwaka 2010. Umekuwa ukiboresha huduma za msingi mijini kufikia
walengwa. Mradi huu wa uendelezaji miji Tanzania umeundwa kwa ajili ya kukabili
changamoto mbalimbali za Miji ya Tanzania. Mradi huu unatekelezwa na Halmashauri
nchini, chini ya usimamizi wa Ofisi ya Waziri Mkuu – Tamisemi.
Mradi huu ni mkopo kutoka Benki ya Dunia na ruzuku kutoka Danida.
Mwanzoni mwa wiki mwandishi wetu aliongea na Kaimu Katibu Mkuu wa Tamisemi Bwn.
Jumanne Sagini ambaye alikua na haya ya kusema “Mradi wa uendelezaji miji Tanzania
upo na una lengo la kuboresha viwango na kurahisisha ufikiwaji wa huduma za msingi
Mijini kwa kukarabati na kupanua miundombinu ya Miji pamoja na kuziimarishia uwezo
taasisi husika katika kuboresha mapato na usimamizi wake”
Bwn. Jumanne Sagini aliendelea kusema “Mradi huu umegawanyika katika maeneo
makuu matatu ambayo ni Miundo mbinu na huduma za miji; Uimarishaji wa Taasisi
pamoja na Usimamizi wa Mradi; na ni miji saba tu ndiyo itakayofaidika na mradi huu.
Miji yenyewe ni Tanga, Arusha, Mwanza, Kigoma, Mbeya, Mtwara, na Dodoma, Kwa
Mji wa Dodoma, Mradi unatekelezwa na Halmashauri ya Manispaa Dodoma Ustawishaji
Makao Makuu Dodoma (CDA)”.
Mradi huu unagharama ya $ 175.5, ambapo $162.8 ni mkopo kutoka Benki ya Dunia na
$12.7 ni ruzuku kutoka DANIDA. Mkopo wa Benki ya Dunia ni kwa ajili ya maeneo ya
Miundombinu na huduma za miji, wakati ruzuku kutoka DANIDA itagharamia uimarishaji
wa Taasisi katika kutekeleza majukumu yake.
Ili kujua kwa undani zaidi kuhusu mradi huu, Mwandishi wetu wa habari aliongea na
Mratibu wa mradi huu Mhandisi Davis Ben Shemangale.
Mhandisi Davis Ben Shemangale alielezea : “Mradi huu ni njia ya kutekeleza dhana ya
kugatua madaraka toka Serikali Kuu kwenda kwa umma, mradi huu wa TSCP
unaendeshwa na Halmashauri husika kwa kuchagua na kuitekeleza miradi kwa kadri ya
vipaumbele vyao”.
Mhandisi Davis Ben Shemangale alimalizia kwa kusema “mradi huu umewekwa katika
awamu tatu hadi nne kwa kila mji na mpaka sasa wakandarasi kwa awamu zote
wamekwisha anza kazi” aliendelea kwa kusema “wakandarasi kwaajili ya kutekeleza
awamu ya kwanza walianza kazi Novemba mwaka 2011 na awamu ya pili walianza kazi
mwezi June mwaka 2012 ambapo awamu ya tatu na ya nne walianza kazi mwezi
Novemba 2012”
LIONEL MESSI NDOTO ZA KUTWAA UBINGWA WA DUNIA ZAENDELEA KUSUMBUA KICHWA CHAKE!!
Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Mshambuliaji nyota wa klabu ya Fc Barcelona, raia wa Argentina Lionel Andrew Jorge Messi amesema tangu aondoke nchini kwake akiwa na miaka 13 kujiunga na Real Madrid anaota kutwaa ubingwa wa kombe la dunia ambao hajawahi kushinda na kikosi cha timu ya taifa licha ya kuwa mchezaji nyota ngazi ya soka la klabu.
Messi aliyeshinda tuzo ya mchezaji bora wa FIFA mara nne mfululizo toka mwaka 2009 ameshida kombe la ligi ya mabingwa barani ulaya mara tatu na kombe la ligi kuu nchini Hispania mara sita amesema sasa kila usiku ndoto za kutwaa ubingwa wa dunia zinamsumbua sana.
Messi ameshinda kila kitu kwa sasa kasoro kombe la dunia, hivyo anaota kufanya hivyo ili kuwafurahisha mashabiki wa Argentina.
Nyota huyo alisema kuwa alisimuliwa na wazazi wake kuwa tangu akiwa na miaka miwili au mitatu alikuwa anaonesha kuwa atacheza soka kutokana na kupenda kushika mpira.
“Tangu nikiwa mdogo sana nilikuwa nawaza kuwa mchezaji wa kimataifa, nimefanikiwa kwa kiwango fulani, lakini nadhani ni muhimu sana kwangu kushinda kombe laq dunia kwa sasa nikiwa na miaka 25″. Alisema Messi.
NYOTA A UKWELI: Lionel Messi alijiunga na Barcelona kutoka Argentina akiwa na miaka 13
Katika mahojiano maalumu Messi amesema anatamani sana kushinda kombe la dunia kwa sasa akiwa na timu ya taifa lake Argentina

Uwezo wa Messi kupiga chenga na kufunga mabao kumemfanya awe mchezaji bora zaidi duniani
TUZO YAKE: Messi ameshinda tuzo ya FIFA mara nne mfululizo toka mwaka 2009
SI MCHEZO: Messi ameshinda kombe la sita msimu huu katika ligi ya Hispania akiwa na FC Barcelona

UBINGWA: Messi alipokuwa akishangilia ubingwa wa UEFA mwaka 2009 baada ya kuifunga Manchester United
Messi akinyanyua mzigo wa UEFA mwaka 2011 baada ya kuwafunga United kwa mara nyingine
NJE: Messi katika mchezo dhidi ya Nigeria kombe la dunia mwaka 2010 nchini Afrika Kusini ambapo walifungwa katika hatua ya nusu fainali mnamo mwaka mabao
KIONGOZI: Diego Maradona alitandikwa maboa 4-0 na Ujerumani katika mechi ya robo fainali ya kombe la nia mwaka 2010 nchini Afrika kusini
ITAKUWAJE?: Messi ataiongoza Argentina kutafuta ubingwa kombe la dunia mwakani nchini BrazilMAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA UTOKOMEZAJI WA UGONJWA WA FISTULA, JIJINI DAR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na baba wa mtoto, Elizabeth Nora kutoka Dodoma aliyelazwa katika Hospitali ya CCBRT, wakati Makamu alipofika hospitalini hapo leo Mei 23, 2013 kwa ajili ya kushiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Utokomezaji wa Ugonjwa wa Fistula. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Dokta wa Hospitali ya CCBRT, wakati alipokuwa akitembelea katika wodi za wagonjwa waliolazwa katika Hospitali hiyo, alipofika hospitalini hapo leo Mei 23, 2013 kwa ajili ya kushiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Utokomezaji wa Ugonjwa wa Fistula. Kulia ni Mtoto Boniface Patrick akiwa na Baba yake, Patrick Luwao, Wakazi wa Dodoma, akiwa amelazwa baada ya kufanyiwa upasuaji na kuongezewa sehemu ya mguu uliokuwa mfupi. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Stellah Nzyemba, ambaye awali alikuwa mgonjwa na baada ya kutibiwa katika Hospitali hiyo ya CCBRT na kupona ameajiriwa ili kuwasaidia wagonjwa wa Fistula. Makamu alifika hospitalini hapo leo Mei 23, 2013 kwa ajili ya kushiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Utokomezaji wa Ugonjwa wa Fistula. Picha na OMR
Makamu wa Rais Dkt Bilal, akimjulia hali mtoto mgonjwa aliyelazwa katika Hospitali hiyo ya CCBRT.
Makamu wa Rais Dkt. Bilal, akiwasili katika eneo lililoandaliwa maalum kwa ajili ya kufanyia shughuli za maadhimisho hayo.
Balozi wa Uingereza nchini, Dianna Melrose, akizungumza wakati wa maadhimisho hayo.
Balozi wa Ugonjwa wa Fistula, Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Mwana FA, akisoma hotuba yake kuhusiana na kuzunguka katika baadhi ya mikoa na kutoa ujumbe kwa wananchi na hasa kina mama kuhusu Ugonjwa huo.
Wasanii 21 walioungana na kuimba wimbo wa Kidole kimoja, wakitoa burudani jukwaa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Utokomezaji wa Ugonjwa wa Fistula, yaliyofanyika leo Mei 23, 2013 Jijini Dar es Salaam. Picha na OMR
RAIS DKT.JAKAYA KIKWETE AKUTANA NA WANANDINGA WA TIMU YA TAIFA “TAIFA STARS”LEO IKULU!!
Rais Jakaya Kikwete akiongea na wachezaji wa timu ya mpira ya Taifa, Taifa Stars leo Ikulu jijini Dar es salaam alipokutana nao kuwapa hamasa waweze kupata ushindi katika mchezo wao dhidi ya Moroco utakaochezwa Juni 7, na michezo mingine ikiwa ni hatua ya kuiwezesha timu hiyo kukata tiketi ya kushiriki mashindano ya kombe la dunia mwaka 2014.
Rais Jakaya Kikwete akiongea na wachezaji wa timu ya mpira ya Taifa, Taifa Stars leo Ikulu jijini Dar es salaam alipokutana nao kuwapa hamasa waweze kupata ushindi katika mchezo wao dhidi ya Moroco utakaochezwa Juni 7, na michezo mingine ikiwa ni hatua ya kuiwezesha timu hiyo kukata tiketi ya kushiriki mashindano ya kombe la dunia mwaka 2014.
Rais Jakaya Kikwete akiwaaga wachezaji wa Timu ya Taifa Stars mara baada ya kukutana nao leo Ikulu Jijini Dar es salaam kuwahamasisha washinde mchezo dhidi ya timu ya Taifa ya Moroco utakaofanyika June 7 ikiwa ni sehemu ya Taifa Stars kutafuta ticketi ya kucheza mashindano ya Kombe la Dunia.
Meneja wa Timu ya Taifa Stars Bw. Mukebesi akiteta jambo na Kepteni wa Timu ya Taifa Stars Juma Kaseja Ikulu jijini Dar es salaam walipokutana na Rais Jakaya Kikwete.
Wachezaji wa Timu ya Taifa Stars wakipata chakula walichoandaliwa na Rais Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo alipokutana nao kuwatakia ushindi katika mchezo wao dhidi ya Moroco.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika Picha ya Pamoja na wachezaji wa Timu ya Taifa , Taifa Stars, viongozi wa Wizara ya Habari, Vijana ,Utamaduni na Michezo na Viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika Picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Taifa , Taifa Stars Ikulu jijini Dar es salaam.
Picha na Aron Msigwa – MAELEZO na Freddy Maro Ikulu.
Na Veronica Kazimoto –MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo amekutana na timu ya Taifa (Taifa stars) kwa lengo la kuitia moyo katika mechi ijayo kati yake na timu ya Moroco ikiwa ni harakati za Tanzania kutafuta tiketi ya kucheza fainali za kombe la Dunia kwa mara ya kwanza mwaka 2014.
Rais Kikwete ameiambia timu hiyo kuwa ina uwezo mkubwa wa kusonga mbele kutokana na uwezo mkubwa waliouonesha katika mchezo wao dhidi ya Gambia ambapo walifanikiwa kupata ushindi wa bao 2-0.
“Maadamu mara ya kwanza mliwashinda Gambia, hakikisheni pia mnapata ushindi dhidi ya Moroco, mkishinda tunafurahi sana na mkishindwa tunanyong’onyea sana,” amesema Rais Kikwete.
Aidha amempongeza kocha wa timu hiyo Kim Poulsen pamoja na Kamati ya Taifa ya ushindi ya Taifa stars kwa kuisaidia timu hiyo kiasi cha shilingi milioni 30 ikiwa ni mkakati wa kuiongezea nguvu kwa hatua iliyofikia na kuwataka wachezaji kujituma ili kuwafurahisha watanzania ambao hivi sasa wanaipenda timu yao ya Taifa.
Nae Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Fenera Mukangara amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa michezo nchini ili kuondoa changamoto zinazoikabili timu hiyo.
Kwa upande wake Kocha Poulsen, amemshukuru Rais Kikwete kwa kuwakaribisha na kuwatia moyo ambapo ameahidi kuifundisha vizuri timu hiyo ili kuhakikisha kuwa wanapata ushindi.
Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake nahoidha wa timu hiyo Juma Kaseja amemshukuru Rais Kikwete na kuahidi kujituma kwenye mazoezi na hatimaye kuibuka washindi kwenye mechi zijazo.
Taifa stars ambayo inakamata nafasi ya pili katika kundi C inatarajia kucheza ugenini na Morocco mnamo Juni 7 mwaka huu.
WAKAZI WA MBEZI BEACH WAHAMASISHWA KUPELEKA WATOTO KUPIMA AFYA BURE
Mkurugenziwahospitaliya IMTU Dkt. Ali Mzige akisitiza umuhimu wa wazazi kujali afya za watoto na kufuatilia uzito wa watoto wao walio chini ya umri wa miaka mitano alipokua akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam ,Kulia kwake ni Bw.Saibal Sarbadhikari Meneja Mkuu wa umoja wa BANGO SANGHO.
Mkurugenzi wa hospitali ya IMTU Dkt. Ali Mzige akihamasisha wananchi kujitokeza katika zoezi la upimaji afya bure kwa watoto walio chini ya miaka mitano,utakaofanyika jumapili Mei 26 katika hospitali hiyo iliyopo Mbezi Beach. Kushoto kwake ni Bw.Saibal Sarbadhikari Meneja Mkuu wa umoja wa BANGO SANGHO.
Na Genofeva Matemu -MAELEZO
HOSPITALI ya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Tekinolojia (IMTU hospital) kwa kushirikiana na Umoja wa Jamii ya watu kutoka India Bengali waliopo nchini Tanzania watatoa huduma ya upimaji afya bure jumapili Mei 26 mwaka huu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano wanaoishi maeneo ya Mbezi Beach .
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa hospitali ya IMTU Dkt. Ali Mzige alipokua akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusiana na afya ya mtoto na umuhimu wa maziwa ya mama hasa kwa watoto walio chini ya miezi 6 .
Dkt. Mzige amesema wanakusudia kupima uzito, presha na kutazama afya ya kinywa kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano ambapo watatumia vifaa maalumu vya upimaji presha kwa watoto hao.
“Tutapima uzito ambao takwimu zake ni Kg 10 kwa mtoto wa mwaka mmoja, Kg 11 kwa mtoto wa mwaka mmoja na nusu, Kg 12 mtoto wa miaka 2, Kg 13 kwa mtoto wa miaka miwili na nusu, Kg 14 kwa mtoto wa miaka 3, Kg 15 kwa mtoto wa miaka mitatu na nusu, Kg 16 mtoto wa miaka 4, Kg 17 mtoto wa miaka minne na nusu, na Kg 18 ni kwa mtoto wa miaka mitano”, amesema Dkt. Mzige.
Akirejea matokeo ya sensa ya mwaka 2012 Dkt. Mzige amesema matokeo hayo yalionesha kuwa asilimia 42 ya watoto chini ya miaka mitano hapa nchini wamedumaa, ambapo asilimia 16 wana uzito pungufu (Underweight) na asilimia 5 wamekonda (Marasmic) wako kwenye rangi nyekundu ya kadi za watoto za kliniki.
Aidha Dkt. Mzige ameishauri jamii kula lishe bora na kamili sababu lishe bora huanzia nyumbani hivyo ni jukumu la jamii kupata elimu ya chakula bora na mlo kamili wenye kujenga afya bora kwa watoto.
Zoezi la upimaji wa afya kwa watoto limeanza rasmi mwaka huu na linatarajiwa kufanyika kila mwaka au mara mbili kwa mwaka kwa kushirikiana na uhisani wa Bango Sangho jamii ya wahindi wanaoishi hapa nchini ambao wamekua wakitoa vifaa vya kupimia afya za watoto.
WASANII 320 KUJIMWAGA JUKWAANI KUONESHA VIPAJI SIKU YA TAMASHA LA MASTAA CHIPUKIZI!!
TAMASHA la Mastaa chipukizi zaidi ya 320 la mwezi Mei litafanyika Jumapili 26, 2013 katika ukumbi wa Starlight Hotel kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 10 jioni.
Mwenyekiti wa Shiwata, Caasim Taalib alisema maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika na vikundi vya sanaa vya Kaole, Splendid, Super Shine Taarab, Five Star Modern Taarab pamoja na wasanii mbalimbali wa Bongo Flava, Maigizo,Ngoma, Dansi na Sarakasi nao wamethibitisha kushiriki.
Taalib alisema wasanii wakongwe wa bongo flava walioalikwa ni Stara Thomas, Ommy G na waigizaji wakongwe wa Kaole na Splendid wataonesha umahiri wao katika fani ya sanaa Kauli Mbiu ikiwa ni Kilio cha Msanii .
Vikundi vingine vitakaonesha vipaji vyao ni Kepteni Shaibu, Tanzania Disabled, Uyoga Boga Village, Ndafu Arts Group, CGC, Magengistar Crew, Dodo Arts Group, Culture Arts Group, Wachapa Kazi Academy, Soweto Picture, Shiwata Commedy, Mwavionelachi, Manuari Arts Group, Tandale Morden Taarab na Begeja Wushu,
Wakati huo huo SHIWATA inawapongeza wote walioshiriki tamasha la Aprili 27 ambako zaidi ya wasanii 300 walishiriki kuonesha vipaji.
Pia Taalib amelipongeza Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) kwa ushirikiano wao mzuri na kuwaomba viongozi wengine wa bendi za muziki, taarab,vikundi vya sanaa,mapromota,maprodusa na wadau wote kushiriki katika matamasha haya ili kujenga ushirikiano wa pamoja.
UJUMBE WA MAMLAKA YA BANDARI TANZANI (PTA) WATAMBELEA RWANDA
Ujumbe wa Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA) uko nchini Rwanda kubadilishana ujuzi na uzoefu na Rwanda kuhusu utekelezaji wa mradi wa kurahisisha na kuwezesha biashara (Trade Facilitation) kwa kutumia TEHAMA – Electronic Single Window System. Muda mfupi ujao TPA itaanza utekelezaji wa mradi huo kwa niaba ya wadau wote wa sekta ya usafirishaji, Forodha, wafanyaniashara na wadau wote wa Tanzania.
Ujumbe huo wa Tanzania unaongozwa na Mkuu wa mradi na Kaimu Mkurugenzi wa idara ya TEHAMA-TPA Ndg. Phares Magesa wa kwanza kushoto katika picha juu, wengine ni Mathayo Ntandu, Jesse Shali na Kilian Chale ambao ni maofisa wakuu TPA.
NBC YADHAMINI YATOA SOMO LA UJASIRIAMALI KWA WANAWAKE WA TANGA
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa (kushoto) akipokewa na Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Fedha zinazofuata Kanuni za Kiislamu ‘NBC Islamic Banking’ cha Benki ya Taifa ya Biashara, Yassir Masoud alipokwenda kufungua semina ya siku moja kwa wanawake wajasiriamali waislamu iliyoandaliwa na NBC mjini Tanga leo. Katikati ni Meneja Tawi la NBC Tanga Deusdedit Mashalla.
Baadhi wa washiriki wa semina ya siku moja iliyoandaliwa na Benki ya NBC Kitengo cha Islamic Banking wakiwa katika semina hiyo jijini Tanga leo.
Na Mwandishi Wetu
Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kupitia kitengo chake cha Huduma za Kibenki zinazofuata kanuni za kifedha za Kiislamu inatarajia kuanzisha huduma ya mikopo kwa wafanyakazi ‘Islamic Group Finance’ kabla ya Septemba mwaka huu.
Akizungumza wakati wa semina ya siku moja ya wanawake wajasiriamali wa Kiislamu jijini Tanga jana, Mkuu wa Islamic Banking wa NBC, Yassir Masoud alisema lengo la kuanzishwa kwa huduma hiyo ni kutoa fursa za mikopo kwa wateja wao wanaohudumiwa kwa kufuata kanuni za dini hiyo.
Masoud aliwaambia wanawake waliohudhuria semina hiyo kwamba ili waweze kujikwamua kiuchumi, wanahitaji kujifunza mbinu za biashara, akisisitiza kwamba hata mafundisho ya Kiisllamu yanatoa maelekezo kuhusu utafutaji wa riziki.
”Uislam umehimiza mambo ya uwekezaji, Uislamu unahimiza masuala ya mali maandiko yakisema kwamba kutafuta riziki ni sawa na kutafuta fadhila za Mwenyezi Mungu,” alisema.
Akifungua semina hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga bibi Chiku Galawa aliwahimiza wanawake mkoani humo kujizatiti kwenye ujasiriamali ili kusaidia juhudi za serikali katika kuinua maendeleo yasiyoridhisha ya mkoa huo.
Alisema kuwa kwa kupitia semina hiyo, NBC imefungua njia mpya yenye matumaini kwa wanawake wa Tanga, njia ambayo mashirika mengine yanapaswa kuifuata.
“NBC ni moja kati ya benki kongwe yenye mtanda mpana kuliko zote nchini na imekuwa mstari wa mbele ikishirikiana na watu mbalimbali katika kuboresha maisha ya Watanzania,” alisema.
Katika siku za hivi karibuni, NBC imekuwa ikiwekeza zaidi katika kuelimisha jamii, hususan wajasiriamali kupitia semina na warsha mbalimbali huku ikishirikiana na makampuni mengine.
Mwishoni mwa mwaka jana, benki hiyo iliandaa mkutano wa wajasiriamali wadogo wadogo wa jijini Dar es Salaam kwa ushirikiano na shirika lisio la kiserikali linalojishughulisha na vijana, YESi.
NBC pia ni wadhamini wa Top 100 Midsize Companies Survey ambayo inaendeshwa kwa ushirikiano na KPMG kuyasaka na kuyazawadia makampuni ya kati yanayokuwa kwa kasi.
“Sekta ya Biashara ndogo ndogo na za kati ni muhimu katika kukuza uchumi nchini, na ni sekta inayoweza kutoa nafasi za ajira kwa wananchi wengi. NBC wametambua hilo,” alisema.
Aliishukuru benki hiyo na kuishauri iendelee kutoa mafunzo kwa wahusika wa sekta hiyo na kuwawezesha wajasiriamali kukuza biashara zao na hatimaye kuinua uchumi wa nchi.
Rais Kikwete amwapisha Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria na Mabalozi Wapya wanne
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal na Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe wakiwa katika picha ya pamoja na mabalozi wapya waliopaishwa leo ikulu jijini Dar es Salaam.aliyesimama mbele kushoto no Balozi Liberata Mulamula anayekuwa Balozi Mpya wa Tanzania nchini Marekani.Waliosimama nyuma kutoka kushoto ni Balozi mpya wa Tanzania Uholanzi Wilson Masilingi,Balozi mpya wa Tanzania katika visiwa vya Commoro Chabaka Kilumanga,Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa Geneva Balozi Modest jonathan Mero na Balozi mpya wa Tanzania katika falme za Kiarabu(UAE)Mbarouk Nassor Mbarouk.Kabla ya uteuzi Balozi Liberata Mulamula alikuwa msaidi wa Rais Masuala ya kidiplomasia na aliwahi kuwa katibu mkuu wa nchi za Maziwa Makuu.(picha na Freddy Maro)
Balozi Kilumanga-Commoro Akiapa
Balozi Masilingi-Uholanzi akiapa
Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (UAE) akiapa
Balozi Mero-Geneva akiapa
Jaji Aloycius Mujuluzi akiapa
MKUTANO WA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI WAFANYIKA VISIWANI ZANZIBAR
Bw Sihaba Vuai afisa mazingira ofisi ya makamu wa kwanza wa rais zanzibar akizungumza kuhusu hali ya mazingira ya zanzibar na madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi katika mkutano wa kamati ya kitaifa ya wataalam ya mabadiliko ya tabia nchi unaoendelea mjini zanzibar
Wanakamati ya kitaifa ya kitaalam ya mabadiliko ya tabia nchi wakimsikiliza mtoa mada hayupo pichani katika mkutano unaoendelea mjini zanzibar (Picha na Evelyn Mkokoi)
TIMU KUTOKA GHANA YAIBUKA MSHINDI WA NUSU FAINALI YA GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™NA KUIACHA TIMU KUTOKA KENYA IKIAMBULIA NAFASI YA PILI
Washindi wa pili wa nusu fainali ya kwanza ya Guiness Football Challenge Francis Wangari(kushoto) na Kepha Kimani(kulia) kutoka Kenya katika picha ya pamoja na waendeshaji wa kipindi cha Pan-Africa Guinness Football Challenge Larry Asego na Mimi Kalinda.
Washindi wa kwanza wa nusu fainali ya kwanza ya Guiness Football Challengekutoka Ghana Naab Jonathan Baan(kushoto) na Desmond Odaano(kulia) katika picha ya pamoja na waendeshaji wa kipindi cha Pan-Africa Guinness Football Challenge Larry Asego na Mimi Kalinda.
………………………………………………..
Dar es Salaam: Jana usiku kupitia televisheni za ITV na Clouds TV nusu fainali ya kwanza kabisa ya GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ ilirushwa hewani na katika runinga Afrika nzima ambapo timu ya Ghana ilionesha ni kwanini ni timu bora ambayo ndiyo imejishindia pesa nyingi mpaka sasa.
Jonathan Nabb na Desmond Odaano walionesha uwezo na ujasiri wao walipoibuka washindi zidi ya wapinzani wao timu kutoka Kenya katika mchezo wa jana. Katika hatua ya pesa ukutani walifanikiwa kulenga lango namba nne na hivyo kupata dola za kimarekani 12,000 wanazoziongeza katika dola 8,500 walizokuwa nazo awali katika hatua ya robo fainali.
Wakenya Francis Ngigi na Kepha Kimani ambao ni washindi wa pili katika nusu fainali hii wataungana na Ghana katika fainali.Ingawa waliikosakosa hatua ya ukuta wa pesa wa Guinness bado wana nafasi ya kuwa mabingwa katika fainali.
Wapenzi wa kipindi hiki cha Guinness football challenge wanaweza kupima maarifa yao katika soka kupitia GUINNESS® VIP™. Wanaweza kufanya hivyo kwa kujisajili bure kabisa katika m.guinnessvip.com kwa kupitia simu ya mkononi.
Usikose kufuatilia ukurasa wa facebook wa GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE kwa habari mbalimbali.
Chilly Willy, Dodoma Wine, CXC Africa kudhamini Redds Miss Sinza 2013
Flaviana Matata atoa wito kwa serikali kuhusu ajali ya MV Bukoba
Miss Universe Flaviana Matata akiwa na Mkurugenzi wa Compass communicayion, Maria Sarungi wakiwasha mshumaa kwenye kaburi la Marehemu mama yake mzazi aliyefariki katika ajali ya MV Bukoba mwaka 1996.Veronica Lugenzi kushiriki onyesho la mavazi jijini Dar es salaam
Mbunifu wa mitindo anayekuja kwa kasi,wa Tanzania Veronica Lugenzi kwa kushirikiana na wabunifu wengi kutoka nchi za Marekani, Kenya na Zambia watafanya maonyesho ya mavazi kwa mara ya kwanza kesho Jumamosi kwenye ukumbi wa Ledger Plaza wa hotel ya Bahari Beach.
PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI BUNGENI BAADA YA KUAHIRISHWA KUTOKANA NA (VURUGU ZA MTWARA)
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi akitoa kauli ya Serikali Bungeni kuhusu vurugu zilizotokea Mkoani Mtwara.
Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda akiahirisha Bunge kutokana na vurugu zilizotokea Mkoani Mtwara
Waziri wa Nchi ofis ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) Merry Nagu akiomba kutengua kanuni ya Bunge Na. 38 ili kuruhusu suala la vurugu za Mtwara kujadiliwa Bungeni.
Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda akizungumza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Jaji Frederick Werema pamoja na baadhi ya Mawaziri ndani ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuahirishwa kwa kikao cha Bunge .
Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Prof. Sospeter Muhongo akizungumza na baadhi ya Mawaziri na Wabunge ndani ya ukumbi wa Bunge mara baada ya Spika wa Bunge kuahirisha bunge
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Emmanuel Nchimbi (Kushoto) akizungumza na mbunge wa Kinondoni Mhe. Iddi Azzan nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya bunge kuahirishwa.
Wabunge wa Viti Maalumu wakiwa nje ya ukumbi wa Bunge baada ya Spika kuahirisha Bunge. Kutoka kushoto ni Mhe. Lucy Owenya(CHADEMA), Katikati Mhe. Mkiwa Kimwanga(CUF) na kulia ni Mhe. Dkt. Merry Mwanjelwa(CCM).
Kundi la Waandishi wa Habari wanaoripoti habari za Bunge wakitoka ndani ya ukumbi huo mara baada ya Spika wa Bunge kuahirisha kikao cha Bunge.PICHA NA ZAWADI MSALLA-MAELEZO DODOMA
























RECENT COMMENTS