TUTUMIE HABARI NA PICHA MDAU!!

Friday, May 18, 2012

NAPE: CCM NDICHO CHAMA PEKEE CHENYE DEMOKRASIA YA KWELI NCHINI


NA MWANDISHI WETU

CCM ndicho chama cha kisiasa chenye demokrasia ya kweli tofauti na vyama vya upinzani vinavyoonekana kujaa udikteta na hivyo kubaki kuwa kama vyama vya harakati tu.

Tofauti na CCM ambayo wanachama wake wana uhuru wa kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, katika vyama vingine hawapati fursa hiyo kutokana na viongozi wake kuwajia juu wanachama wanapojitokeza kutaka kuwania nafasi za uongozi.

Hayo yamesemwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wakati akifungua Mkutano wa Uchaguzi wa viongozi wa ngazi mbalimbali tawi la CCM, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya Chama mjini Dar es Salaam.

BANYANA BANYANA KUWASILI LEO KUIVAA TWIGA STARS


 
Timu ya Taifa ya wanawake ya Afrika Kusini (Banyana Banyana) inatarajia kuwasili nchini leo (Mei 18 mwaka huu) saa 12.45 jioni kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Twiga Stars itakayofanyika Jumapili (Mei 20 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 
Banyana Banyana ina msafara wa watu 26 ambapo 18 kati ya hao ni wachezaji na itafikia kwenye hoteli ya Sapphire Court Hotel tayari kwa mechi hiyo ya kujipima nguvu kwa Twiga Stars inayojiandaa kwa mechi ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) dhidi ya Ethiopia. Mechi dhidi ya Ethiopia itachezwa Mei 27 mwaka huu jijini Addis Ababa.
 
Nayo Banyana Banyana iko katika kinyang’anyiro cha kutafuta tiketi ya Fainali za AWC ambapo katika raundi hii ya pili imepangiwa Zambia na itaanzia mechi hiyo ugenini jijini Lusaka.
 
Kesho (Mei 19 mwaka huu) saa 6 kamili mchana, makocha wa timu zote mbili, Boniface Mkwasa wa Twiga Stars na Joseph Mkhonza wa Banyana Banyana watakuwa na mkutano na Waandishi wa Habari kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuzungumzia mechi hiyo.
 
Twiga Stars na Banyana Banyana zote ziko katika raundi ya mwisho ya AWC ambapo zikifanikiwa kuwatoa wapinzani wao zitakwenda kwenye fainali hizo zitakazofanyika Novemba mwaka huu nchini Equatorial Guinea.
 
 
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

TUZO YA MWANAMICHEZO BORA WA TANZANIA

CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) Jumapili Mei 20, 2012 saa nne asubuhi kitatangaza mdhamini wa Tuzo za Mwanamichezo Bora wa Tanzania kwa mwaka 2011.

Mdhamini huyo atatangazwa kwenye mkutano ambao ataufanya Mwenyekiti wa TASWA, Juma Pinto pamoja na mdhamini wa tuzo hizo, ambapo mkutano huo utafanyika kwenye mgahawa mpya uitwao City Sports  &  Lounge uliopo jirani na mnara wa askari makutano ya barabara ya Samora na Azikiwe, Posta Dar es Salaam.

TASWA inachukua fursa hii kuwaalika waandishi wote wa habari za michezo kuhudhuria kwenye mkutano huo ili tuweze kuanza pamoja katika mbio hizi za kuelekea kwenye Tuzo ya Mwanamichezo Bora wa Mwaka 2011.

Tayari Kamati ya Tuzo ishateuliwa na imetangazwa, hivyo baada ya mkutano huo taratibu nyingine zitatangazwa kwa kadri zitakavyokuwa zimekamilishwa na Kamati Maalum ya Tuzo ya Mwanamichezo Bora wa Tanzania.

Kwa miaka mitano iliyopita walioshinda Tuzo ya Mwanamichezo Bora wa TASWA walikuwa ni  Samson Ramadhani (2006),  Martin Sulle  (2007),  Mary Naali (2008), ambao wote ni wanariadha, wakati 2009 na 2010 alikuwa mcheza netiboli Mwanaidi Hassan.

MSANII CANDY AACHIA SINGLE NYINGINE INAYOKWENDA KWA JINA LA "CHANINI"


 
 
STUDIO YA "PAMOJA RECORD" IMEACHIA SINGLE MPYA YA YULE MWANADADA CANDY AMBAYE MWEZI MMOJA ULIOPITA ALIACHIA NGOMA YAKE INAYOKWENDA KWA JINA  NIMPENDE MILELE IKIWA CHINI YA MOST RECORD..!.
LEO HII "PAMOJA RECORD" IMEACHIA SINGLE YA MWANADADA HUYO INAYOKWENDA KWA JINA LA "CHANINI", CANDY MSANII AMBAYE LICHA YA UIMBAJI  ANAKIPAJI PIA CHA KUCHEZA MUZIKI  WA AINA ZOTE.
 
CANDY AMBAYE MTAANI ANAJULIKANA KWA JINA LA (CANDY TIKISA!! AU CANDY WA KUJIACHIA..!) , AMBAYE AMEJIPATIA UMAARUFU MKUBWA PALE ALIPOSHIRIKI MASHINBDANO YA KUCHEZA MUZIKI  YALIYOKUWA YANAJULIKANA KAMA "TIKISA" AMEACHANA NA LEBO YA "MOST RECORD " NA KUPATA OFA NYINGINE KWENYE STUDIO ZA PAMOJA RECORD JIJINI DAR ES SALAAM, AMBAYO TAYARI AMESHAREKODI SINGLE YAKE HIYO MOJA INAYOITWA "CHANINI" AMBAYO TAYARI IMESHAANZA KUPIGWA KWENYE VITUO MBALIMBALI VYA REDIO.
 
KWANINI AMEACHANA NA MOST RECORD?................. CANDY ANAJIBU  KUWA HAWAKUELEWANA NA MANAGEMENT NZIMA YA MOST RECORD AMBAPO KWA SASA WAPO KWENYE MZOZO AMBAO BADO HAUJAPATIWA UFUMBUZI  LAKINI TAYARI ALIKUWA AMEREKODI SINGLE MOJA  PAMOJA NA VIDEO AMBAYO VYOTE AMEFANYIA KWENYE KAMPUNI HIYO YA MOST RECORD,  YEYE CANDY AMEIZUIA ISIONYESHWE KWENYE VITUO VYA TELEVISION MPAKA PALE MUAFAKA WAO UTAKAPOMALIZWA.

CANDY AMEWAFAGILIA SANA PAMOJA RECORD KUWA WAPO SAWA NA MAKINI SANA KWENYE KAZI NA NDIYO MAANA AMEINGIA MKATABA NAO NA HUKO ATAFANYA KAZI AMBAYO MASHABIKI WA MUZIKI WATASUUZIKA NA MUZIKI WAKE.................EBU SIKILIZA SINGLE YAKE HII YA CHANINI............ NDANI YA WIMBO HUU AMEZUNGUMZIA KITU GANI!! ...........EBU FUTATILIA ALA ZA MUZIKI JINSI GANI ZILIVYOPANGWA NA KUPANGIKA CHINI YA USIMAMIZI WA MKUBWA  WA MTAYARISHAJI WA MUZIKI  MTU MZIMA NASS B.
 


         WASIFU WAKE :

          JINA LA MSANII :   HELEN DAVID LUSEKERO
          ANAJULIKANA KAMA : CANDY
          JINA LA WIMBO : CHANINI
          STUDIO : PAMOJA RECORD
          MTAYARISHAJI WA MUZIKI : NASS B.
          MAWASILIANO :  0753915938
           EMAIL/ FACEBOOK ; hellendavid40@yahoo.com
 
WIMBO HUU NI RUKSA KUCHEZWA SEHEMU YEYOTE BILA YA MASHARTI.

MREMBO WA ZAMANI MBONI MASIMBA AZINDUA KIPINDI CHAKE CHA (MBONI TALK SHOW)



 Mboni Masimba akiongea na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Serena Dar es salaam leo wakati akizungumzia kipindi chake kitakachorushwa katika Luninga ya EATV kushoto ni Bw Tyson.
 Waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo.
 Mboni Masimba akiwa na Blogger maarufu wa kike anayeendesha blogu ya 8020Fashion Shamimu Mwasha.



WASANII wametakiwa kutumia vipindi vya Talk Show kwa ajili ya kutangaza kazi zao sanaa ndani na nje ya nchi ikiwa pamoja na kuitangaza nchi ya Tanzania.
Wito huo ulitolewa na Mtangazaji wa kipindi kipya cha Luninga, Mboni Masimba wakati wa kuzindua kipindi chake kiitwacho Mboni Talk Show chenye kuburudisha, kuelimisha na kufundisha  ambacho kitaanza kuoneshwa Alhamis ijayo katika kituo cha East Africa Television.

Mboni alisema kuwa vipindi vya Talk Show kwa sasa vinapendwa na kutazamwa na watu wengi zaidi kutokana na uvutiaji wake na mijadala mbalimbali ambayo inazungumzwa katika vipindi hivyo.

Akizungumzia kipindi chake Mboni alisema kuwa kipindi hicho kitakuwa na sehemu tano ambazo ni Ufunguzi, wakati wa maswali kutoka kwa mtangazaji kwa wageni na kutoka kwa hadhira kwenda kwa wageni, na pia kutakuwa na kipengele cha My dreams come true ambapo kipindi chake kitatoa misaada kwa watu wenye mahitaji mbalimbali na pia kutakuwa na Tamati.

Alisema kuwa kutokana na ukubwa wa Luninga ya East Africa Tv anahakika kuwa watu kutoka nchi za Afrika Mashariki wataburudika na kufurahishwa na kipindi hicho cha kipekee huku akiwataka wadau mbalimbali kutoa maoni yao mara baada kitakapoanza kurushwa.

“ Ni kwamba Tanzania kuna watu wa aina mbalimbali na wenye vipaji mbalimbali ambao wanatakiwa kuendelezwa na hapa ndipo nguvu ya Tv Talk Show inahitajika na mimi nitahakikisha kuwa kupitia kipindi change cha Mboni Show nitawafikiwa kila wenye kuhitaji msaada wa kuendelezwa kuwa wanafanyiwa hivyo” alisema Mboni

Mashauzi Classic, Mashujaa kusindikiza Miss Tabata


 
BENDI za Mashujaa na Mashauzi Classic zitatumbuiza kwenye kinyang’anyiro cha kumtafuta mrembo wa Tabata, Miss Tabata 2012 kitakachofanyika Juni Mosi katika ukumbi wa Da West Park, Tabata.
Akizungumza jana, mratibu wa shindano hilo, Godfrey Kalinga, alisema kuwa wameamua kuweka burudani nyingi yenye ladha tofauti ili kukidhi kiu ya rika zote watakaohudhuria shindano hilo ambalo ni kivutio kwa wakazi jijini.
Kalinga alisema shindano hilo pia litatumika kwa ajili ya kusherehekea miaka 10 tangu kuasisiwa kwa shindano la Miss Tabata.
“Shindano la mwaka huu litakuwa ni la aina yake kwa sababu hii utakuwa ni mwaka wetu wa 10 tangua kuanza kuandaa Miss Tabata ndio maana tunaleta burudani nyingi,” alisema mratibu huyo wa Bob Entertainment na Keen Arts.
Alisema warembo waliyowahi kushinda mataji mbalimbali ya shindano hilo, pia wamealikwa kusherehekea miaka 10 ya Miss Tabata.
Shindano hili limedhaminiwa na Dodoma Wine, Redds, Integrated Communications, Fredito Entertainment, Multichoice Tanzania, Screen Masters, Kitwe General Traders, Step In Electronics, Brake Point, Atriums Hotel na Lady Pepeta.
Warembo watakaoshiriki kwenye shindano wanaendelea na mazoezi kila siku katika ukumbi wa Dar West Park.
Warembo hao ni Neema Saleh (18), Noella Michael (19), Queen Issa (20), Hycalisa Joseph (18), Phillios Lemi (19), Wikllihemina Mvungi (20) na Nightness Rajab (19).
Wengine ni Suzanne Pancras (19), Caroline David (21), Khadija Nurdin (19), Jamila Omary (18), Advent  Mamkwe (21), Nadya Marjeby (21), Axer Peter (20), Rahama Hassan (19), Mercy Mlay (21) na Diana Simon Laizer (20).
Warembo 10 watachaguliwa kushiriki mashindano ya Miss Ilala na baadaye Miss Tanzania.
Mrembo anayeshikilia taji la Tabata kwa sasa ni Faiza Ally.
Warembo wa Tabata wamekuwa wakifanya vizuri katika mashindano ya Miss Tanzania ambapo mwaka juzi Consolata Lukosi alishinda nafasi ya tatu kabla ya kutangazwa kuwa balozi wa kinywaji cha Redds.
Katika shindano la mwaka juzi Juliet William pia alishinda nafasi ya tatu katika ngazi hiyo ya taifa.
Juliet ndiye anayeshikilia taji la dunia la Miss Progressive International.

MTANZANIA DR ENGINEER SHABAN KACHUA ATUNUKIWA RASMI SHAHADA YAKE YA UDAKTARI WA FALSAFA NCHINI CANADA.

Dr Engineer Shaban Kachua mwenye joho lenye rangi nyekundu na Bluu akiwa na waafrika wenzake wakati wa alipotunukiwa Shahada yake ya Udaktari wa falsafa Nchini Canada.
Hapa Dr Kachua akiwa amekaa mstari wa mbele kabisa na wahitimu wenzake.
Mama Mzazi wa Dr Kachua (mwenye blauzi nyeusi), akiwa na Mama mkwe wake, wote kwa pamoja walishiriki katika tukio la kihistoria la kutunukiwa Shahada ya PHD kwa mtoto wao nchini Canada.
Mrs Dr Shaban Kachua (Jemima) akiwa na furaha pamoja na watoto wao walishiriki katika shughuli ya kutunukiwa Mume wake shahada ya udaktari wa Falsafa (PHD).

Kwa sasa Dr Shaban Kachua anaishi Nchini Canada pamoja na familia yake. Sisi kama watanzania wenzake tunapenda kumpongeza sana kwa kuweza kuipeperusha vema Bendera yetu, tunapenda kumshauri pia, elimu yake hiyo aweze kuitumia pia kulisaidia Taifa lake la Tanzania hasa katika nyanja hiyo ya Sayansi, kwa kutambua zaidi tuna upungufu mkubwa wa wanasayansi katika Taifa letu.

HONGERA SANA

Mkurugenzi Msaidizi Idara ya mazingira Ofisi ya makamu wa Rais katika mahojiano maalum DW

Mkurugenzi Msaidizi Idara ya mazingira Ofisi ya makamu wa Rais Bw. Richard Muyungi katika mahujiano maalum ya kipindi cha Radio idhaa wa kiswahili ya Radio Deutsch Welle mjini Bonn Ujerumani.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya mazingira Ofisi ya makamu wa Rais Bw. Richard Muyungi katika mahujiano maalum mtangazaji Sudi Mnete (kulia) katika kipindi cha Radio katika idhaa wa kiswahili ya Radio Deutsch Welle mjini Bonn Ujerumani.(Picha na Evelyn Mkokoi)

UONGOZI WIZARA YA HABARI WAKUTANA NA RAIS IKULU.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein,akizungumza na Uongozi wa Wizara ya
Habari,Utalii,utamaduni na Michezo,katika utekelezaji wa mpango wa
kazi za Wizara hiyo huko Ikulu Mjini Zanzibar leo,(kushoto) Makamo wa
kwanza wa Rais Maalim
Seif Sharif Hamad.  [ Picha  na Ramadhan Othman,IKULU.]

MKUU WA WILAYA MPYA KASKAZINI B AAPA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein,akimuapisha  Mdungi Makame Mdungi kuwa Naibu Katibu
Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, hafla ya kiapo ilifanyika Ikulu Mjini
Zanzibar jana.{Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.}
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein,akimuapisha  Khamis Jabir Makame,kuwa Mkuu wa Wilaya
ya kaskazini B Unguja, katika hafla   iliyofanyika Ikulu Mjini
Zanzibar jana.{Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.}
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein,akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo
ya Amali,katika utekelezaji wa mpango wa kazi za Wizara hiyo huko
Ikulu Mjini Zanzibar leo,(kushoto) Makamo wa kwanza wa Rais Maalim
Seif Sharif Hamad.  [ Picha  na Ramadhan Othman,IKULU.]

ATC IMEWASILI JIJINI MWANZA MUDA MFUPI UJAO INAREJEA JIJINI DAR ES SALAAM

Kaimu Mkurugenzi wa shirika la ndege la ATC Bw. Paul Chizii kulia akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo mara baada ya kutua katika uwanja wa ndege wa Mwanza mchana huu ambapo wafanyakazi pamoja na watu mbalimbali ambao wamekuwa wakitumia shirika hilo katika kusafiri wameonekana kufurahia sana kuanza kwa safari za shirika hilo

Katika uwanja wa ndege wa Mwanza kutakuwa na hafla fupi ya kupongezana na kukaribisha ndege hiyo ambapo pia keki itakatwa na kuliwa kwa kuashiria uzinduzi rasmi wa safari zake
Abiria mbalimbali wakishuka mara baada ya ndege hiyo kuwasili jijini Mwanza nchana  huu.
Dada Lilian wa ATC akiwa katika pozi mara baada ya kushuka kwenye ndege hiyo leo mjini  Mwanza.
Abiria wakishuka kwenye ndege.
Abiria wakishuka kwenye ndege mjini Mwanza

TAYARI TUMETUA (KIA) MUDA MFUPI UJAO TUNARUKA KUELEKEA JIJINI MWANZA

 Tayari ndege mpya ya shirika la ndege la ATC aina ya  Boeing 737-500 imeshatua katika uwanja wa ndege wa Kilimanjaro Internationl Airport kwa muda kabla ya kuelekea jijini Mwanza tena na kurudi jijini Dar es salaam katikati aliyeshika ua ni mtangazaji wa Clouds Said Bonge akishoo Love na mashabiki wake pamoja na wafanyakazi wa kiwanja cha ndege cha KIA leo hii katika uzinduzi rasmi wa safari zake.
Hii ndiyo ndege yenyewe ya ATC Boeing 737-500 ikiwa katika kiwanja cha ndege cha KIA muda huu kabla ya kuruka kuelekea jijini Mwanza kabla ya kurejea jijini Dar es salaam.

MWANZA, KILIMANJARO KISHA NAREJEA DAR ES SALAAM BAADAE

Kazi ni kazi tu  na haina wakati maalum wa kufanya, niko Aiport uwanja wa ndege wa Mawlimu Julius K. Nyerere asubuhi hii nikiwa safarini kuelekea Mwanza na kisha Kilimanjaro na baada ya muda nitarejea jijini Dar es salaam,  nitakuwa mmoja wa wanahabari watakaopasha habari za uzinduzi wa ndege mpya ya shirika la ndege la ATC Boeing 737-500 inayozindua safari zake leo mambo zaidi kuhusu safari hiyo tutapashana baadae.

Naibu Waziri, ajitolea kumsomesha aliyekosa ada Handeni



 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii na Watoto Ummy Mwalimu jana ofisini kwake jijini Dar es Salaam. akiwa ofisini kwake wakati alipokutana na Mhariri Mkuu wa Mtandao wa Thehabari.com, Joachim Mushi na kufanya mahojiano 
Mhariri Mkuu wa Mtandao wa Thehabari.com, Joachim Mushi akifanya mahojiano na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii na Watoto Ummy Mwalimu jana ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri, Wizara ya Maendeleo ya Jamii na Watoto, Ummy Mwalimu (kulia) akimadilishana kadi za mawasiliano na Mhariri Mkuu wa Thehabari.com, Joachim Mushi mara baada ya mahojiano ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam.
NAIBU Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu jana amejitolea kumsaidia mtoto ambaye mzazi wake alishindwa kumpeleka shule baada ya kufaulu kwa kile kukosa ada ya shule.

Akizungumza na Mhariri Mkuu wa Mtandao wa Thehabari.com, Joachim Mushi, ofisini kwake jijini Dar es Salaam amesema ameguswa na habari hiyo iliyotolewa na mtandao huu juzi, hivyo yupo tayari kumsaidia mtoto huyo nawengine watakao kuwa na matatizo kama hayo eneo hilo.

Hata hivyo, Naibu Waziri Mwalimu, ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu kutokea Mkoa wa Tanga amesema anaamini mama wa mtoto huyo alikuwa muoga kuwasiliana na viongozi wa wilaya hiyo ya Handeni kwani wangelimsaidia na mtoto huyo kujiunga na shule.

"Kwanza napenda kuwapongeza kwa kuibua changamoto kama hizi, kimsingi nimeguswa na habari hiyo ya mtoto kushindwa kujiunga na shule kwasababu mzazi wake hana uwezo...naomba mnipe mawasiliano ili tuangalie namna ya kumsaidia," alisema Naibu Waziri huyo.

Alisema ipo haja ya halmashauri kufuata ushauri wa Serikali kwa kile kutenga asilimia 5 ya mapato yao kuwawezesha wanawake kupitia mfuko wa maendeleo ya wanawake, kwani endapo akinamama watawezesha wanaweza kufanya mabadiliko hata katika changamoto kama hizo.

"Unajua ukimuwezesha mwanamke unakuwa umeiwezesha jamii...endapo kila wilaya ikikubali kutenga asilimia 10 ya mapato yake, kwa ajili ya mfuko wa  maendeleo ya wanawake na ule wa vijana kwa kugawa asilimia tano tano kila upande tutasaidia mambo mengi, zikiwemo changamoto za maisha katika familia," alisema Mwalimu.

Juzi mtandao wa Thehabari.com pamoja na mitandao mingine washirika wa Thehabari.com walichapisha habari ya mmoja wa wanafunzi waliochanguliwa kujiunga na masomo mwaka huu kushindwa kuendelea na shule baada ya mzazi wake mmoja (mama) kushindwa kumgharamia.

Mtandao wa Thehabari.com unafanya mawasiliano na mzazi wa mtoto huyo na kuangalia namna ya kuwakutanisha na baadhi ya wasamaria waliojitolea kubeba mzigo wa masomo kwa kijana huyo. Mtandao huu utaendelea kuwajulisha taarifa zaidi za tukio hili hadi pale mtoto atakapo jiunga na shule.

Habari hii imeandaliwa na Mtandao wa Thehabari.com (wwww.thehabari.com)

FFU ! wa Ngoma Africa kuvaana na Wakameruni 5,000 Stuttgart,Ujerumani


Wakameruni wapatao zaidi ya 5,000 waishio nchini ujerumani wanatalajia kujimwaga na muziki wa dansi wa Ngoma Africa Band huko mjini Stuttgart,Ujerumani siku ya jumamosi
20 Mai 2012,katika sherehe maalumu kwa ajili  ya nchi yao "Cameroni Challenge" .
Kamati ya maandalizi ya jumuia ya wakameruni nchini Ujerumani imetoa mwaliko kwa
bendi maarufu ya muziki wa dansi barani Ulaya Ngoma Africa band almaarufu FFU,kutumbuiza
katika sherehe hizo zitakazo fanyika mjini Stuttgart,nchini Ujerumani,ambako zitahudhuriwa na
wakameruni 5000 pamoja na wageni wa mataifa mbali mbali.
Mzimu huo wa dansi Ngoma Africa band aka FFU unatarajiwa kutoa burudani ya kuwapandisha
mzuka wadau wote watakao jimwaga uwanjani,
Ngoma Africa band sasa wanatamba na mpini wao mpya " Uhuru wa Habari" sikiliza hapa www.ngoma-africa.com au http://www.ngoma-africa.com

Thursday, May 17, 2012

President Jakaya Kikwete in Washington DC

President Jakaya Mrisho kikwete speaks during a high level breakfast briefing on scaling up nutrition at the Dirksen office building in Washington DC May 17, 2012.

President Jakaya Mrisho kikwete speaks during a high level breakfast briefing on scaling up nutrition at the Dirksen office building in Washington DC May 17, 2012. Together with him at the High table are the minister of international Cooperation of Canada  Ms Beverly J. Oda, UNFP Executive Director Ms Ertharin Cousin and the CEO of Concern Worldwide, Mr Tom Arnold.
President Jakaya Mrisho kikwete greets the USAID Administrator Dr Raj Shah after taking part in a high level breakfast briefing on scaling up nutrition at the Dirksen office building in Washington DC May 17, 2012. right is the Tanzania Ambassador to the US Ms Mwanaidi sinare Maajar and second right is Ms Liberata Mulamula, Personal Assistant to the President (Diplomatic Affairs)
Photo courtesy  of  STATE HOUSE

WASHIRIKI WA BIGBROTHER STARGAME 2012 WAZUNGUMZA NA WANDISHI WA HABARI BAADA YA KUREJEA

Aliyekuwa Mwakilishi wa Tanzania katika Shindano la msimu wa 7 wa  Big Brother Stargame 2012 wapili kulia Bw.Julio Batalia  akizungumza na  waandishi wa habari kwenye mkutano uliofanyika kwenye hoteli ya Southernsun jijini Dar es salaam , wa pili kutoka kulia ni Mshiriki wa Big Brother Stargame 2012 Bi,Hilda Reiffenstein, kulia ni Meneja Masoko wa Kampuni ya Multichoice Tanzania Bi Furaha Samalu wa mwisho kulia na kushoto ni Meneja Uhusiano wa Maltchoice Tanzania Barbara Kambogi
PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE
Alikyekuwa Mshiriki wa Big Brother Stargame 2012 Bi,Hilda Reiffenstein akizungumza na wanahabari kwenye hoteli ya Southersun jijini Dar es salaam leo, kulia ni Meneja Masoko wa Kampuni ya Multichoice Tanzania Bi Furaha Samalu wa mwisho kutoka kushoto ni Meneja Uhusiano wa Maltchoice Tanzania Barbara Kambogi na Bw.Julio Batalia aliyekuwa mshiriki wa Bigbrother Stargame 2012
Afisa Mahusiano wa Multichoice Tanzania Barbara Kambogi wakwanza(kushoto) akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam ambapo ametolea ufafanuzi mfumo uliotumika mwaka huu katika kuchagua nchi itakayotoka katika shindano hilo  Afisa Mahusiano wa Multichoice Tanzania Barbara Kambogi wakwanza(kushoto) akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam ambapo ametolea ufafanuzi mfumo uliotumika mwaka huu katika kuchagua nchi itakayotoka katika shindano hilo  
Waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo leo

KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI YAWAPA MABLOGGER SEMINA YA UENDESHAJI WA MITANDAO NA MAADILI KATIKA KUPASHA HABARI ZA MASOKO

 Mkurugenzi wa mtandao wa www.fullshangweblog.com akipokea cheti chake kutoka kwa Ephraim Mafuru Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) mara baada ya kumalizika kwa semina ya Mablogger kuhusu usimamizi na maadili ya upashaji wa habari na masoko katika  uendeleshaji wa blogu na mitandao mingine, iliyofanyika leo kwenye makao makuu ya kampuni hiyo yaliyoko Oysterbay jijini Dar es salaam, katikati ni mkurugenzi wa mawasiliano wa kampuni hiyo Teddy Mapunda
 Mkurugenzi wa Fullshangweblog kushoto akizungumza na mkurugenzi wa 8020fashion Shamimu Mwasha  mara baada ya semina hiyo, kulia ni Mkurugenzi wa blogu ya Father Kidevu.
mkurugenzi wa 8020fashion Shamimu Mwasha akipokea cheti chake Ephraim Mafuru Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) katikati ni mkurugenzi wa mawasiliano wa kampuni hiyo Teddy Mapunda.
 Josephat Lukaza akipokea cheti chake kutoka kwa Ephraim Mafuru Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL), katikati ni Teddy Mapunda Mkurugenzi wa Mawasiliano (SBL) kulia ni David Shayo wa (SBL)
Mroki Mroki  kutoka blogu ya Father Kidevu kushoto akipokea cheti chake.
 Mwendeshaji wa Blogu ya Mtaa kwa Mtaa Othman Michuzi kushoto akipokea cheti chake.
 Mkurugenzi wa Blogu ya Jiachie Ahmed Michuzi kushoto akipokea cheti chake.
 Mkurugenzi wa kampuni ya R&R Caroline Gul kushoto  akipokea cheti chake.
 Mkurugenzi wa mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti Teddy Mapunda akifafanua jambo katika semina ya uendeshaji wa mitandao na maadili ya upashaji wa habari za masoko katika blogu na mitandao mingine.
Mablogger mbalimbali wakifuatilia kwa makini yaliyokuwa yakijiri katika semina ya uendeshaji wa mitandao na maadili ya upashaji wa habari za masoko katika blogu na mitandao mingine.
Mkurugenzi wa masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti  Ephraim Mafuru kulia na kushoto Mkurugenzi wa mawasiliano kampuni ya bia ya Serengeti Teddy Mapunda waliokaa wakiwa katika picha ya pamoja na mablogger bara baada ya kumaliza semina yao na kupokea vyeti leo katika makao makuu ya kampuni hiyo.

Mkuu wa mkoa arusha awaapisha wakuu wa wilaya na kuwapa somo kubwa sana

Mkuu wa wilaya ya Arusha John Mongela akiwa anaapa kiapo cha utiifu mbele ya mkuu wa mkoa wa arusha Magesa Mulongo leo


Akuu wa wilaya ya Arumeru  Nyirembe Munasa akiwa anakula kiapo cha uaminifu mbele ya mgeni rasmi

 Wakuu wa wilaya wakiwa katika picha ya pamoja na mkuu wa mkoa  wa Arusha (picha zote na  Gladness Mushi-Arusha
 

Katika jiji la Arusha leo wakuu wapya wilaya wameapishwa ambapo  Mkuu wa mkoa wa Arusha magesa mulongo amewaotaka wasiliwe sifa na badala yake wahakikishe kuwa wanajikita zaidi katika kutatua kero za  wananchi.

Mbali na hayo aliwataka washirikiane na Madiwani katika kutatua tatizo la hati chafu ndani ya halmashauri kwa kuwa kati ya halmashauri zote jijini hapa iliyo na hati safi kidogo ni halmashauri ya Meru pekee

Pia aliwataka wakuu hao kuhakikisha hawapigwi chenga na sheria mbalimbali hasa za vijiji na ile ya asilimia ishirini kwa kila lkijiji kwa kuwa kwa sasa halmashauri zinakwepa sheria hiyo na hali hiyo inapelekea wenyeviti wa vijijiji kuwa katika hali nghumu ya kiutendaji