TUTUMIE HABARI NA PICHA MDAU!!

Monday, May 28, 2012

WATU 30 WAPANDISHWA KIZIMBANI ZANZIBAR KWA KUDAIWA KUHUSIKA NA VURUGU NA KUHARIBU MALI



Na Juma Mohammed,MAELEZO Zanzibar

Watu 30 wakiwemo wanaosadikiwa kuwa  wafuasi wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam  wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Mwanakwerekwe  wakikabiliwa na makosa mbalimbali ikiwemo kuwashambulia Polisi,kuchoma moto matairi ya Magali barabarani na ukorofi.

Mbali na tuhuma hizo,pia wameshtakiwa kwa kufanya maandamano yasiyokuwa na kibali kinyume na sheria  pamoja na  uzembe na ukorofi wa kuwashambuliya polisi kwa mawe.


Watuhumiwa hao walifikishwa katika mahakama nne tofauti, ikiwemo mahakama ya hakimu Mohammed Ali Mohammed walikofikishwa watuhumiwa wawili, wanne kwa hakimu Janet Nora Sekihola, 11 kwa hakimu Omar Mcha Hamza na 11 waliobakia, wamepandishwa mbele ya hakimu Valentine Andrew Katema.

Kwa nyakati tofauti watuhumiwa hao walishitakiwa kwa makosa ya kufanya mikusanyiko isivyo halali, uzembe na ukorofi pamoja kufanya kitendo kinachoweza kuleta uvunjifu wa amani.

Watuhumiwa hao ni Mbarouk Said Khalfani (45), na Mussa Juma Issa (57) wanaodaiwa kuwa ni viongozi wa Jumuiya hiyo, ambapo walifikishwa mbele ya hakimu Mohammed Ali Mohammed, na kusomewa shitaka la kufanya mkusanyiko isivyo halali kinyume na kifungu cha 55 (1) (2) (3) na kifungu cha 56 cha sheria namba 6/2004 sheria za Zanzibar.

Wengine ni Mbwana Hamadi Juma (50), Massoud Hamadi Mohammed (17), Mohammed Juma Salum (35), Abdulrahman Simai Khatib (19), Hashim Juma Issa (54) Matar Fadhil Issa (54).

MKOA WA RUVUMA WAPOKEA MWENGE WA UHURU LEO

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma Severin Tossi(kushoto) akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Njombe John Mahali .Mwenge wa Uhuru umepokelewa leo mkoani Ruvuma katika kijiji cha Ngelenge wilaya ya Ludewa kabla haujaanza mbio zake mkoani Ruvuma
 (Picha na Muhidin Amri Nyasa= Songea)

‘SUGU’ KUTOA BURUDANI KALI DAR LIVE JUMAPILI HII

Mwanamuziki mkongwe wa Hip Hop nchini Joseph Mbilinyi aka ‘M II’ au ‘Sugu’ amethibitisha kuwa siku ya Jumapili ijayo (Juni 3) atatoa shoo ya nguvu ndani ya Ukumbi wa Taifa wa Burudani wa Dar Live huko Mbagala, jijini Dar es Salaam.
Meneja Mkuu wa Global Publishers Abdalah Mrisho (kushoto) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu burudani itakayotolewa na Sugu akiwa na wasanii wengine wakali   ambao ni pamoja na Professor J na Juma Nature.  Kulia ni Mratibu wa Shoo za Wasanii Dar Live, Luqman Maloto.
Mr II akiongea na waandishi wa habari juu ya onyesho hilo,(kushoto) ni Mratibu wa Burudani na Matukio Dar Live, Juma Mbizo.
 Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza mkali huyo.
Mr II akiwa na wafanyakazi wa Global Publishers ambao, kutoka kushoto ni: Walusanga Ndaki, Sudi Kivea na Clarance Mulisa.  

Rais Kikwete ahutubia Wakuu wa mikoa na Wakuu wa Wilaya mjni Dodoma leo

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba yake wakati wa mafunzo ya wakuu wa mikoa makatibu tawala na wakuu wa wilaya yanayoendelea katika ukumbi wa St.Gaspar Mjini Dodoma leo(Picha na Freddy Maro)
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba yake wakati wa mafunzo ya wakuu wa mikoa makatibu tawala na wakuu wa wilaya yanayoendelea katika ukumbi wa St.Gaspar Mjini Dodoma leo(Picha na Freddy Maro)

AFRICAMAGIC SAYS THANK YOU & MAKES A BIG ANNOUNCEMENT!



Robert Whitehead -Barker Haines
 
Just six weeks after the exciting revision of its channel line-up, pioneering continental TV brand AfricaMagic has more fantastic news for viewers.

As of Monday May 28, DStv audiences tuned in to the glamorous new AfricaMagic Entertainment (channel 128) will also be able to watch two more massively popular daily series as the sensational soap operas GENERATIONS and ISIDINGO debut on the channel.

The latest development is particularly significant because it means that for viewers outside of SA, where both series are produced, the best place to watch the freshest episodes will be AfricaMagic Entertainment!

“We are very pleased that we have been able to conclude our agreement with the SABC (South African Broadcasting Corporation) for the rights to screen these two dramatic and dynamic shows that already have a proven record of attracting audiences and maintaining high levels of viewer interest. And the fact that we will be screening the latest episodes shortly after the SABC is a great benefit to our audiences,” says M-Net Africa Managing Director Biola Alabi.

Alabi goes on to express her gratitude to audiences for their understanding and support during the recent changes to the AfricaMagic channels.

SIMBA SC WALIVYOSHEREHEA UBINGWA WAO DAR LIVE

TIMU ya Simba SC ya jijini Dar jana ilisherehekea ubingwa wake wa 2011/2012 pamoja na mashabiki wake katika ukumbi wa burudani wa DAR LIVE. Sherehe hizo zilitanguliwa na msafara wa magari, pikipiki na watembea kwa miguu ambao walianzia safari yao makao makuu ya klabu hiyo Mtaa wa Msimbazi  na kupitia mitaa kadhaa ya jiji kabla ya kumalizikia katika ukumbi wa Dar Live. Katika msafara huo wachezaji wa Simba walikuwa katika lori la wazi lililopambwa bendera na vitambaa vya rangi nyekundu na nyeupe huku wakiwa na kombe lao walilolibeba.
Baadhi ya wachezaji wa Simba SC wakishangilia pamoja na kombe lao wakati wakipita katika mitaa ya jiji la Dar es Salaam jana.
(Picha: Issa Mnally na Richard Bukos/ GPL)
Mashabiki na wapenzi wa Simba SC wakiwa katika  msafara kuelekea katika Ukumbi wa Dar Live kusherehekea ubingwa wa timu yao jana.
.Mashabiki wa Simba wakiingia ndani ya Ukumbi wa Dar Live tayari kwa sherehe za ubingwa.

Uzinduzi rasmi wa tawi la Chadema Washington Dc wafanyika

Uongozi wa juu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  katika uzinduzi rasmi watawi la Chadema Washington Dc  kwenye meza ya juu wa kwanza kushoto Libe Mwangombe, akifatiwa na Mhe. Peter Msigwa,  Mwenyekiti wa tawi Mhe. Kalley Pandukizi,  Mhe. Zitto Kabwe, na Mhe. Nassari Joshua, Dogo Janja, mkutano huo ulifanyika kwenye ukumbi wa Mirage Hall uliopo University Of Bld, Hysattsville, Maryland Nchini Marekani.f
Mhe. Zitto Kabwe akitoa hutba kuelezea mpango mzima wa mambo yanavyoendelea nchini Tanzania
Wantazania waishio DMV Nchini Marekani wakiwa katika uzinduzi wa tawi la chadema Washington  Dc
Wantazania waishio DMV Nchini Marekani wakiwa katika uzinduzi wa tawi la chadema Washington  Dc

ZIARA YA WAZIRI KIGODA KATIKA KIWANDA CHA URAFIKI

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Mh, Abdala kigoda akiongea na wajumbe pamoja na Viongozi wa kiwanda cha Urafiki jijini Dar es Salaam alipotembelea kiwanda hicho leo jijini Dar es Salaam ambapo aliziona changamoto nyingi zinazozikabili kiwanda hicho ikiwemo mishahara miidogo ya wafanyakazi na akaahidi kuzifanyia kazi.
(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)
Diwani wa kata ya Ubungo  jijini  Dr es Salaam Mh, Bonifas Jacob  akieleza changamoto zinazo wakabili wafanyakazi wa kiwanda hicho pamoja na usimamiaji mbovu wa Kiwanda hicho mbele ya Waziri.
Baadhi ya wafanyakazi, Viongozi pamoja na wajumbe mbalimbali waliohudhuria kwenye ziara hiyo wakimsikiliza Mh, Waziri kwa umakini.
Naibu Meneja uchapishaji na utiaji rangi kwenye kanga Bw, Solomon Laban(kulia) akimuelekeza waziri namana mtambo huo wa utiaji Rangi unavyofanya kazi  akikagua baadhi ya Mitambo ndani ya kiwanda hicho.
Waziri akikagua uzalishaji wa kanga kiwandani hapo.
Mh. Waziri wa viwanda na Biashara akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa kiwanda hicho baada ya kumaliza matembezi.

WAZIRI WA ULINZI DK. EMMANUEL NCHIMBI ATUA VISIWANI ZANZIBAR NA KUKEMEA VITENDO VYA VURUGU

Na Juma Mohammed,MAELEZO Zanzibar

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Dk. Emmanuel Nchimbi ametua Visiwani Zanzibar leo ambapo amekemea vitendo vya vurugu,akiahidi Serikali kuwachukulia hatua ikibidi hata kuwavizia nje ya misikiti kwa wale watakaohusika na uvunjifu wa amani .

Waziri Nchi aliwasili Mjini Zanzibar akiwa na Mkuu wa Jeshi  la Polisi,Inspekta Jenerali Said Mwema kwa pamoja waliitisha mkutano uliowakutanisha viongozi wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar(JUMAZA),Mabalozi,Kamisheni ya Utalii, Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam Zanzibar(JUMIKI).

“Suala la kufuata sheria halina mjadala,lazima kila mmoja wetu afuate na kutii sheria hatutawavumilia watakaovuruga amani ya nchi…maandamano yoyote lazima yapate kibali” Aliwaambia wadau katika mkutano huo uliofanyika Makao Makuu ya Polisi Zanzibar,Ziwani.

Waziri Nchi alisema busara ya Polisi imefikia kikomo na kwamba atashangaa sana akiona busara hiyo ikiendelea wakati kuna watu au kikundi kinavunja amani ya nchi.
“Tutashangaa busara ya Polisi ikiendelea wakati watu wanaumia kwa watu wengine kuvunja amani…hatutakubali, tutaendelea kuviziana hata nje ya misikiti tutawakamata” Alisisitiza Waziri Nchi.

Waziri huyo alisema kila mtu anawajibika kitunza amani iliyopo ambapo pia alisema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yenye mfumo wa Umoja wa Kitaifa imefanyakazi nzuri katika kipindi kifupi na kuwapongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk. Ali Mohammed Shein, Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Shariff Hamad na Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd.

MSHINDI WETU WA BAJAJ KATIKA PROMOSHENI YA "VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO" AKABIDHIWA ZAWADI YAKE

Meneja Masoko wa kampuni ya Serengeti Breweries Ltd (SBL) Kanda ya Ziwa, Patrick Kisaka, kushoto akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi kabla ya kumkabidhi mshindi wa Bajaj wa shindano la Vumbua hazina chini ya kizibo, kulia ni Meneja Mauzo wa SBL Mwanza, Octavian Migire.
Meneja wa Mauzo wa Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya ziwa  Bw Patrick Kisaka akikabidhi  Bajaj kwa mshindi wa huyo katika promosheni ya VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO na SBL, Bw. Godfrey Shao mkazi wa mkoa wa Mwanza ambaye alijishindia pikipiki ya matairi matatu( BAJAJ) kupitia bia ya Tusker Lager
Godfrey Shao amesema hakutegemea hata siku moja kupata zawadi kubwa kama ile na kwamba ameishukuru sana kampuni ya bia ya Serengeti kwa kubadilisha maisha yake kwani  sasa anaweza kujiajiri na kuwasaidia wale wanaomtegemea
Bw Godfery Shao ndani ya Bajaj yake akipongezwa na wafanyakazi, wawakilishi, wapenzi na wadau wa kampuni ya bia ya Serengeti baada ya kukabidhiwa Bajaj yake  mpya kabisa

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA BALOZI WA IRAN KWA MAZUNGUMZO IKULU DAR ES SALAAM LEO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkaribisha Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mohsen Movahhed Ghomi, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu Dar es Salaam leo Mei 28, 2012 kwa mazungumzo. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Iran Nchini Tanzania,  Mohsen Movahhed Ghomi, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu Dar es Salaam leo Mei 28, 2012 kwa mazungumzo. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

Big Brother StarGame: Eviction (Sunday May 27, 2012)

The 91 day reality super-series Big Brother StarGame, produced for M-Net’s AfricaMagic, is being screened live 24/7 on DStv 197 & 198. Last night (Sunday 27 May) Mampi was evicted while Ghana’s Mildred & Keitta and Botswana’s Edith & Eve were randomly nominated to face eviction this week.
For more information log on to www.africamagic.tv/bigbrother
Pictured here: Mampi and IK
The 91 day reality super-series Big Brother StarGame, produced for M-Net’s AfricaMagic, is being screened live 24/7 on DStv 197 & 198. Last night (Sunday 27 May) Mampi was evicted while Ghana’s Mildred & Keitta and Botswana’s Edith & Eve were randomly nominated to face eviction this week.
For more information log on to www.africamagic.tv/bigbrother
Pictured here: Tanzanian artist Diamond Platinumz

NBC MOROGORO YADHAMINI KIKUNDI CHA NGOMA PERFORMING ARTS

Meneja wa Tawi wa Benki ya NBC Morogoro, Jasson Shumbusho (kulia)
akikabidhi mfano wa hundi ya shs Milioni 5.1 kwa Mkurugenzi wa Taasisi
ya Sanaa za Maonyesho ya Ngoma Africa Performing Arts, Davie Kitururu
ikiwa ni udhamini wa NBC katika tamasha la sanaa la watoto la Paukwa.
Kushoto ni Mkurugenzi mwenza wa Taasisi hiyo, Bi. Maya Davie na
wengine ni baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo.

UONGOZI WIZARA YA MIUNDOMBINU MAWASILIANO WAKUTANA NA DK. SHEIN

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein,akizungumza na Uongozi wa  Wizara ya Miundombinu na
Mawasiliano, katika utekelezaji wa mpango wa kazi za Ofisi za Wizara
hiyo huko Ikulu Mjini Zanzibar juzi,  [ Picha  na Ramadhan
Othman,IKULU.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein,akizungumza na Uongozi wa  Wizara ya Miundombinu na
Mawasiliano, katika utekelezaji wa mpango wa kazi za Ofisi za Wizara
hiyo huko Ikulu Mjini Zanzibar juzi,  [ Picha  na Ramadhan
Othman,IKULU.]

PATA GAZETI LAKO LA DIRA KILA JUMATATU



BREAKING NEWSSSSSSSSSSSSS: SIMBA YAWATEMA DERRICK WALULYA NA GERVAS KAGO

Taarifa zilizothibitishwa kutoka ndani ya klabu ya Simba zinasema uongozi wa timu hiyo umewatupia vilago nje wachezaji wake Derrick Walulya kutoka nchini Uganda na Gervas Kago kutoka Jamhuri ya Kati ambao waliitumikia klabu hiyo msimu wa ligi  uliomalizika.

Hatua hiyo pengine imekuja baada ya wachezaji hao kuchezea benchi karibu msimu mzima wa ligi wakiwa nje ya uwanja ukiacha Gervas Kago ambaye angalau kwa michezo kadhaa ya Ligi kuu ya Vodacom alikuwa akiingia dakika chache kabla ya kuisha kwa mchezo.

Hii inaonyesha kuwa Simba  watasajili wachezaji wengine ili kuziba mapengo ya wachezaji hao ambao wamewaacha.  

TWIGA STARS YACHAPWA UGENINI 2-1 NA ETHIOPIA


TIMU ya taifa ya wanawake ya Tanzania, Twiga Stars, imeanza ‘vibaya kidogo’ kampeni za kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa kwa wanawake, baada ya kufungwa mabao 2-1 jana jioni mjini Addis Ababa na wenyeji, Ethiopia.
Twiga sasa inahitaji ushindi wa 1-0, Juni 16, katika mchezo wa marudiano mjini Dar es Salaam, ili kukata tiketi ya kucheza fainali hizo kwa mara ya pili mfululizo, Novemba mwaka huu, Equatorial Guinea, zikiwa ni za nane katika historia ya michuano hiyo

Evans Bukuku's Comedy Club


Leo ni siku ya kuzaliwa kwa Mama yetu Beatrice Shemakulenge

Leo ni siku ya kuzaliwa kwa Mama yetu Beatrice Shemakulenge akiwa TIB Bank (Mlimani City). Pichani
Zeenat Singh kushoto na Mama yake  wakiwa katika picha ya pamoja, 
Ujumbe Tunampenda sana mama yetu na tunamuombea awe na afya
njema, burudani kabisa , mafanikio na maisha marefu. Urs Bahati
Singh & family.

MAONYESHO YA WANAFUNZI UDOM YAFANA JANA KATIKA UKUMBI WA CHIMWAGA ULIOPO CHUO KIKUU CHA DODOMA(UDOM)

 Muandaaji wa Maonyesho haya Ester Zangi ambaye pia ni Mwanafunzi wa Mwaka wa 3 anayesomea shahada ya kwanza ya sayansi ya siasa na utawala wa umma(Wa Kwanza Kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dodoma ambao Wameonyesha vipaji vyao Vya Kuchora Michoro inayoonekana hapo katika maonyesho yaliyofanyika jana Chuo Kikuu Cha Dodoma katika Ukumbi wa Chimwaga
PICHA NA JOSEPHAT LUKAZA WA http://josephatlukaza.blogspot.com
 Mwanafunzi wa Mwaka wa 3 anayesoma shahada ya kwanza ya filamu na sanaa anayejulikana kwa jina la wacko jacko akiwa amesimama pembeni mwa moja ya michoro aliyochora kwa Mikono yake na hapo alikua katika maonyesho yaliyofanyika chuo kikuu cha Dodoma jana
Mmiliki wa Mtandao wa Lukaza Blog Mh Josephat Lukaza (Wa kwanza Kulia) akiwa katika Picha ya Pamoja na Wadau wa Lukaza Blog mara baada ya Kumalizika kwa Maonyesho hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Chimwaga uliopo Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) katikati ni Mh Mzagamba Thobias Kutoka Uswis na Wa Kwanza Kulia ni Atu Mwanafunzi wa Mwaka wa 3 UDOM.
Wanafunzi wa UDOM wanaosoma shahada ya kwanza ya Filamu na Sanaa, Kiswahili wakionyesha uwezo wao wa kucheza boringo katika maonyesho yaliyofanyika jana Katika Ukumbi wa Chimwaga uliopo Chuo Kikuu Cah Dodoma (UDOM)


Mmoja wa wanakamati wa maandilizi ya maonyesho haya ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa 3 Bi Atu anayesoma shahada ya kwanza ya Mazingira ya Chuo Kikuu Cha Dodoma alipokua akitoa neno wakati wa maonyesho hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Chimwaga uliopo katika Chuo Kikuu cha Dodoma(UDOM) jana
Mmiliki na Mwendeshaji wa Mtandao wa Lukaza Blog Mh Josephat Lukaza alipokua akitoa maelekezo jinsi ya Lukaza Blog inavyofanya kazi na vilevile Mtandao wa Lukaza Blog unavyopatikana na ulivyoweza kupokelewa Vizuri ndani ya Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) na vyuo vikuu tanzania wakati wa Maonyesho yaliyofanyika Chuoni hapo jana
Mmoja wa Wanafunzi wanaosoma Shahada ya Kwanza ya Sanaa na Filamu Babra Kalugira akiwa kwenye Kirekodi Video (VIDEO CAMERA) akichukua video ya matukio yaliyokuwa yakiendelea katika Maonyesho hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Chimwaga uliopo Chuoni Hapo

Sunday, May 27, 2012

NMB FINANCIAL FITNESS MASHULENI

Benki ya NMB hivi karibuni Ilizindua mpango wa kukuza uelewa wa maswala ya kifedha kwa wanafunzi mashuleni unaoitwa NMB Financial Fitness, uzinduzi wa awali ulifanyika katika shule ya sekondari Pugu tarehe 17 Mei 2012 na baadae kuingia katika shule za msingi mbalimbali jijini Dar es salaam.

Mpango wa NMB Financial Fitness unalengo la kuongeza uelewa wa matumizi mazuri ya kifedha, uwekaji akiba, kujenga uwezo wa kupanga matumizi na mengine mengi.
Baada ya uzinduzi , Benki ya NMB imeendelea kutambulisha mpango huu kwenye Kanda ya Dar es Salaam katika shule mbalimbali kama utakavyoona picha mbalimbali zilizopigwa katika shule za jiji la Dar es salaam.

Wanafunzi wa shule ya Msingi Bunge wakijisomea jarida ya NMB Financial Fitness.
 Wanafunzi wa shule ya msingi Hananasifu wakijisomea jarida la NMB
Wanafunzi wa shule ya msingi Tandika wakiwa wameinua jarida lao ya NMB Financial Fitness
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi ya Ilala Boma wakiwa makini kusoma jarida la NMB Financial Fitness.
Afisa Benki ya NMB akiwaelekeza jambo wanafunzi wa shule ya msingi ya Mapambano
Wanafunzi wa Turiani wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Benki ya NMB pamoja na mwalimu wao.
Wanafunzi wa shule ya msingi Hananasifu wakisoma jarida la NMB Financial Fitness.