Rais dkt Shein amtembelea Sheha Aliyetiwa Tindi kali

000000Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akimuangalia Sheha wa Shehia  ya Tomondo Wilaya ya Magharibi Unguja,Mohamed Saidi Kidevu,(kulia) jinsi alivyoathirika na  Tindikali alilomwagiwa na Mtu asiyejuilikanwa  huko Tomondo juzi wakati alipokuwa akirudi kuchota maji na kuelekea nyumbani kwake,Sheha huyo yupo katika Hospitali ya Mnazi mmoja kwa matibabu,wa  kushoto Dk.Slim Mohamed Mgeni,[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.] MG 0000Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Sheha wa Shehia  ya Tomondo Wilaya ya Magharibi Unguja,Mohamed Saidi Kidevu,(kulia) aliyetiwa Tindikali na Mtu asiyejuilikanwa  huko Tomondo juzi wakati alipokuwa akirudi kuchota maji na kuelekea nyumbani kwake,Sheha huyo yupo katika Hospitali ya Mnazi mmoja kwa matibabu,wa pili kulia Kaka yake Sheha Sudu Mgeni Saidi.[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]

RATIBA YA SHEREHE ZA AU KESHO – KARIMJEE HALL

TENTATIVE PROGRAMME FOR THE CELEBRATIONS OF THE OAU/AU GOLDEN JUBILEE ON 25th MAY, 2013

 

Venue                  -        Karimjee Hall

Guest of Honour  -        Hon. Bernard Kamillius Membe (MP)

Minister for Foreign Affairs and International Cooperation

 

TIME

EVENT

RESPONSIBLE INSTITUTION

8.00

Arrival at the Ministry

All

8.30

Lighting of the OAU/AU Torch

Hon. Membe-Minister for Foreign Affairs and International Cooperation

8.35

Festive Procession led by Brass Band

Invitees

8.45

Arrival at the Karimjee Hall

Invitees

8.50-9.10

Folk Dances

Dance Troupes

9.15-9.25

Playing of the AU and the Tanzania Anthems

Brass Band

9.30-10.00

Opening Remarks

Guest of Honour (Hon. Membe)

 

10.10-11.20

Panel Discussion-Pan Africanism and African Renaissance

Key Speakers: Amb. W. M. Mangachi & Mme Tonia Kandiero

Moderator: Prof. A. Mhina

11.40-12.50

Panel Discussion-OAU/AU’s Role in the Liberation Struggle and Self-determination

Key Speakers: Amb. A. Kiwanuka & Amb. T.H. Chiliza

Moderator: Amb. M. Maundi

12.50

Closing Remarks

Dean of the African Diplomatic Group

12.50

Folk Dances

Dance Troupes

13.00

Luncheon

Caterer

 

RAIS JAKAYA KIKWETE AFUNGUA MAONYESHO YA MFUMO WA MATOKEO MAKUBWA ‘SASA’ AWAMU YA KWANZA

01Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwa kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa wakati wa Ufunguzi rasmi wa Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa ‘Sasa’ Awamu ya Kwanza leo Mei 24, 2013. Picha na OMR 1Msanii maarufu wa kughani, Mrisho Mpoto, wakibinjuka Sarakasi, wakati kikundi chake na Bendi yake ya Mjomba ilipokuwa ikitoa burudani katika Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa ‘Sasa’ Awamu ya Kwanza, yaliyofunguliwa na Rais Jakaya Kikwete, leo Mei 24, 2013. Picha na OMR 3MWanamuziki wa Bendi ya Mjomba, wakiimba kutoa burudani katika Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa ‘Sasa’ Awamu ya Kwanza, yaliyofunguliwa na Rais Jakaya Kikwete, leo Mei 24, 2013. Picha na OMR4Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwasili kwenye Ukumbi wa Jumba la Makumbusho ya Taifa, leo Mei 24, 2013 kwa ajili ya Kufungua rasmi Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa ‘Sasa’ Awamu ya kwanza. Picha na OMR 7Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwasili kwenye Ukumbi wa Jumba la Makumbusho ya Taifa, leo Mei 24, 2013 kwa ajili ya Kufungua rasmi Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa ‘Sasa’ Awamu ya kwanza. Picha na OMR 7Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwasili kwenye Ukumbi wa Jumba la Makumbusho ya Taifa, leo Mei 24, 2013 kwa ajili ya Kufungua rasmi Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa ‘Sasa’ Awamu ya kwanza. Picha na OMR 8Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakisikiliza maelezo kutoka kwa Mchambuzi Sera Mkuu wa Ofisi ya Rais na Mipango, Lorah Madete, wakati walipokuwa wakitembelea Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa Awamu ya Kwanza, baada ya kuyafungua rasmi leo katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es Salaam. Picha na OMR 9Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakisikiliza maelezo kutoka kwa Ofisa Mtafiti Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Dkt. Mary Shetto, wakati walipokuwa wakitembelea Maonesho ya Mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa Awamu ya Kwanza, baada ya kuyafungua rasmi leo katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es Salaam. Picha na OMR

PICHA ZA MBWA WALIOPATA MAFUNZO YA KUKABILI UHALIFU

DSC_6206Mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya Mbwa akionyesha umahiri wake wa kutumia mnyama huyo mara baada ya kupatiwa mafunzo ya kutumia mbwa Kwa ajili ya kuzuia uhalifu na kikiosi cha mbwa na farasi cha Jeshi la Polisi mafunzo hayo yalifanyika jijini Dar es salaam. (Picha na Hassan Mndeme- Jeshi la Polisi) DSC_6215Mbwa wa kiraia aliyepatiwa mafunzo  na Jeshi la Polisi ya namna ya kukabiliana na uhalifu na wahalifu  wanaobeba madawa ya kulevya hususani bangi.(Picha na Hassan Mndeme- Jeshi la Polisi DSC_6256 DSC_6267Mmoja wa wahitimu wa kike aliyepata mafunzo ya Polisi jamii na ulinzi shirikishi alipata mafunzo ya ukakamavu kwa ajili ya kukabiliana na uhalifu na wahalifu, mafunzo hayo yalifanyika jijini Dar es salaam katika viwanja vya kikosi cha mbwa na farasi cha jeshi la Polisi.( Picha na Hassan Mndeme- Jeshi la Polisi)

Dar Stock Event- Triniti bar

darStockPoster final

JESHI LA POLISI LAMTIA MBARONI MCHOCHEZI WA VURUGU NA FUJO

vujo mtwara

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA

Anuani ya Simu “MKUUPOLISI”                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                     Ofisi ya  Inspekta  Jenerali wa Polisi,
Simu : (022) 2110734                                                                                    Makao Makuu ya Polisi,
Fax Na. (022) 2135556                                                                                                           S.L.P. 9141,
Unapojibu tafadhali taja:                                                                                       DAR ES SALAAM.

24 MAY 2013

TAARIFA YA JESHI LA POLISI KWA VYOMBO VYA HABARI

Jeshi la Polisi Nchini linamshikilia mtu mmoja ambaye jina lake linahifadhiwa kwa sababu za kiupelelezi kwa tuhuma za kueneza ujumbe wa uchochezi na chuki kwa wananchi na viongozi wa serikali kwa njia ya simu ya mkononi akituma SMS kwa lengo la kuchochea fujo, vurugu na kutoa matusi kwa viongozi hao.

Mtu huyo amekuwa akifanikisha kazi hiyo kwa kutumia Chips (sim card) 13 za simu za mkononi ambazo amekamatwa nazo. Jeshi la Polisi linaendelea kumhoji mtu huyo na ushahidi utakapokamilika atafikishwa mahakamani.

Aidha, Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi wenye taarifa zingine za wahahlifu kama hao kujitokeza na kutoa taarifa hizo polisi ili wahalifu hao waweze kukamatwa na kuchukuliwa hatua stahiki, wakiwemo watu wanaowashawishi wenzao kwa njia ya fedha, kuwashauri ama kuwasaidia kwa namna yeyote ile katika kufanikisha uhalifu huo na kusababisha uvunjifu wa amani hapa nchini.
Jeshi la polisi halitasita kumchukulia hatua mtu yeyote atakayebainika kuvunja sheria za nchi.
Imetolewa na:-
Advera Senso-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

SERIKALI: WACHIMBAJI WA MADINI WAACHE KUVAMIA MAENEO YA WAWEKEZAJI

1

Wachimbaji wadogo wa madini

Na Lydia Churi, MAELEZO-DODOMA

 Serikali imewataka wachimbaji wote wa madini nchini wanaovamia maeneo ya wawekezaji wengine kuacha kufanya vitendo hivyo na badala yake waendeleze maeneo wanayomiliki kwa mujibu wa sheria.

 Naibu Waziri wa Nishati na Madini (Madini) Steven Masele alisema tabia ya uvamizi wa leseni kubwa za utafiti unatishia nchi yetu kukosa miradi mikubwa ya migodi mipya katika siku za usoni.

 Akijibu swali la msingi lililoulizwa na mbunge wa Kishapu, Mheshimiwa Suleiman Nchambi aliyetaka kujua mpango wa serikali kuwasaidia mitaji na nyenzo za kufanyia kazi wachimbaji wadogo Mhe. Masele alisema serikali inatambua na kuthamini mchango wa wachimbaji hao katika kuinua uchumi na pato la taifa pamoja na kutoa ajira kwa watanzania wengi.

 Alisema inakadiriwa kuwa watanzania milioni moja wanajishughulisha na kazi ya uchimbaji wa madini nchini na kutokana na hilo serikali kuanzia mwaka wa fedha wa 2009/2010 ilianzisha mpango wa kutenga fedha kwa ajili ya kutoa mikopo kwa wachimbaji wadogo ili waweze kununua vifaa bora vya uchimbaji na uongezaji thamani madini.

 Amewashauri wachimbaji wadogo nchini kuungana ili iwe rahisi kukopesheka kupitia utaratibu ulioandaliwa na serikali. Aidha amewashauri wachimbaji wadogo kuomba mikopo kupitia taasisi nyingine za kifedha kama vile benki na kuhakikisha wanatimiza vigezo vinavyotakiwa na taasisi husika.

Akizungumzia vurugu zilizotokea jana baina ya wachimbaji wadogo na STAMICO huko Buhemba mkoani Mara, Mhe. Masele amewataka wananchi wa eneo hilo kuwa wavumilivu wakati serikali ikiangalia namna ya kutatua tatizo hilo.

MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI MJINI DODOMA LEO

ngelejaWaziri wa Katiba na Sheria,Mh Mathias Chikawe (kushoto), Mbunge wa Sengerema,Mh William Ngeleja na Mbunge wa Peramio, Mh Jenister Mhagama wakifurahi jambo wakati wakitoka ndani ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma jana. Picha zote na Zawadi Msalla wa MAELEZO. sittaWaziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mh Samuel Sitta akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka 2013/14 Bungeni mjini Dodoma.

PHELAN NA STEELE KIBARUA CHAO KUOTA NYASI UNITED, MOYES AMTAKA KOCHA WA EVERTON KUMSAIDIA MAJUKUMU!!

Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com

Kocha msaidizi wa mabingwa wa soka nchini Uingereza, Manchester United Mike Phelan na kocha wa makipa Eric Steele wamejawa na wasiwasi wa kibarua chao kuota nyasi kufuatia ujio mpya wa kocha wa united David Moyes ambaye anasemekana ana mipango ya kumleta kocha mwenza wa Everton Jimmy Lumsden kuwa msaidizi wake katika safari yake ya kuifundisha klabu yake mpya.

Nafasi ya Phelan amekuwa hatarini tangu United imtangaze Moyes kuwa mrithi wa mikoba ya kibabu Alexndar Chapman Ferguson kwani kocha huyo anaonekana kuwa na nia ya kumleta kocha Lumsden ili kuenda sambamba kuijenga United mpya.

Moyes alikutana na Phelon jumanne ya wiki hii wakiwa na Ferguson, Steele na kocha wa sasa wa United Rene Muelensteen katika uwanja wa mazoezi wa Carrington ambapo Moyes alisema leo Ijumaa ataanika mipango yake pamoja na kumtaja msaidizi wake.

Get out, No 2: Mike Phelan was appointed as Sir Alex Ferguson's right-hand man in September 2008 KITUMBUA KINAINGIA MCHANGA: Mike Phelan aliteuliwa na Ferguson kuwa msaidizi wake septemba mwaka 2008

 

On his way: Eric Steele (foreground) will leave his post at Manchester United ANASEPA ZAKE: Kocha wa makipa Eric Steele (wambele) anasemekana kutimka zake baada ya ujio wa David Moyes

 

End of an era: Phelan looks on as Paul Scholes hoists aloft the Premier League title and (below) walking out of the Old Trafford tunnel for possibly the last time MWISHO WA KAZI: Phelan  inawezekana ubingwa wa msimu uliomalizika mei 18 ukawa wa mwisho kukaa Old Trafford

 

Mike Phelan Mike Phelan inawezekana haya ndiyo matembezi ya mwishoni OT kufutaia kocha Moyes kumhitaji kocha wa Everton kuwa msaidizi

 

In with the new: David Moyes will replace Sir Alex Ferguson at Manchester United next season David Moyes  anarithi mikoba ya  Sir Alex Ferguson

 

The National Assembly in Collaboration with the UNDP under the Legislative Support Project Conducted a one day workshop to Mps and Staff on Social and Economic Policies

Yesterday the Office of the National Assembly and the UNDP under the Legislative Support Project organized a one day workshop on Social and economic Policies, Economic growth and development to the Members of the National Assembly and staff aiming at building capacity for Mps and Staff during the Budget session in Dodoma. The workshop is part of the Legislative Support Project to strengthen the capacity of the Mps and Staff in various areas for an effective Oversight, Legislation and representation.

1

One of the Presenter at the workshop on Social and economic Policies, Economic growth and development to the Members of the National Assembly Dr. Haji Semboja from the University of Dar es Salaam, presenting a topic on importance of social economic policies in the budget process for sustainable economic growth and development. The workshop was organized by the office of The National Assembly in Collaboration with the UNDP under the Legislative Support Project 2Mr. Hassan Abdallh from Social and Economic Research Foundation presenting the topic on skills and techniques required by Mps and Staff in using social and economic policies during the Budget process 3Prof. Faustin Kamuzora from Mzumbe University giving outline of what is Challenges facing economic growth and development in Tanzania during the workshop 4Cross section of Mps listening to the presentations attentively during the workshop 5Cross section of Mps listening to the presentations attentively during the workshop 6Cross section of Mps listening to the presentations attentively during the workshop 7Cross section of Mps listening to the presentations attentively during the workshop 8Moderator of the workshop who is also a Chairperson of the Standing Committee on Local Government Hon. Dr. Hamis Kigwangala giving some comments 10Hon. Madabida giving her contribution to the presenters 11Hon. Suleman Zedi curiously posing a question to the presenter during the workshop 12Hon. Athuman Mfutakamba giving some statistics on how good policies can improve the country’s development

SEMINA YA USAJILI- TMS KUFANYIKA MEI 25!!

tenga1

Na Boniface Wambura

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeandaa semina ya usajili kwa njia ya mtandao (Transfer Matching System-TMS) kwa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom kwa ajili ya msimu wa 2013/2014.

 

Semina hiyo itafanyika Jumamosi (Mei 25 mwaka huu) kwenye ofisi za TFF saa 3 kamili asubuhi ikishirikisha watu wawili kutoka kila klabu ambao ni TMS Manager, na ofisa mwingine wa klabu.

 

Klabu za ligi hiyo zinazotakiwa kuhudhuria semina ya usajili ni Ashanti United, Azam, Coastal Union, JKT Ruvu, Kagera Sugar, Mbeya City, Mgambo Shooting, Mtibwa Sugar, Oljoro JKT, Rhino Rangers, Ruvu Shooting, Simba, Tanzania Prisons na Yanga.

TFF YASEMA WENYEVITI WA VYAMA VYA MIKOA NDIYO WASIMAMIZI RCL!!

1

Msemaji wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF, Boniface Wambura Mgoyo

Na Boniface Wambura, TFF

Wakati mechi za kwanza za raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) zinachezwa wikiendi hii, Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imesisitiza kuwa wasimamizi wa mechi za ligi hiyo ni wenyeviti wa mikoa wa vyama vya mpira wa miguu.

 

Kamati hiyo chini ya uenyekiti wa Ramadhan Nassib ilikutana jana (Mei 23 mwaka huu) kupitia ripoti za makamishna kwa mechi za raundi ya kwanza ya RCL iliyomalizika wikiendi ya Mei 18 na 19 mwaka huu.

 

Kuhusu viwanja vinavyotumika kwa ligi hiyo, Kamati imesema vitaendelea kuwa vile vya makao makuu ya mikoa, na kwa vile vilivyokuwa vimeombwa vifanyiwe marekebisho ili viweze kukaguliwa kwa ajili ya RCL msimu ujao. Pia imeitaka mikoa kuendelea kuboresha viwanja vinavyotumika sasa, lakini vina upungufu.

 

Vilevile Kamati imebaini kuwa zimekuwepo pingamizi kuhusu usajili wa wachezaji ambapo imesema haiwezi kujadili pingamizi hizo kwa vile mikoa yote haikuwasilisha usajili wa wachezaji wa klabu husika uliofanyika mikoani kama ilivyoagizwa na kuelekezwa na TFF.

 

Hata hivyo, Kamati imeitaka mikoa ambayo klabu zao zimefanikiwa kuingia raundi ya pili kuwasilisha usajili huo haraka.

 

Pia Kamati imebaini kuwa zipo baadhi ya klabu ambazo zimekata rufani kuhusu usajili wa baadhi ya wachezaji, na kusisitiza kilichowasilishwa ni pingamizi kwa vile kwa mujibu wa kanuni masuala ya uwanjani hayakatiwi rufani. Hivyo, Kamati imeshauri klabu zilizokata rufani zilirejeshewe ada zilizolipa kwa ajili hiyo.

 

Makamishna na waamuzi wanaosimamia mechi za RCL wamekumbushwa kuwa ili mchezaji aruhusiwe kucheza mechi ni lazima awe na leseni yake (kadi ya usajili), vinginevyo asiruhusiwe kucheza mechi husika.

Mechi za RCL zinaendelea wikiendi hii ambapo zote zitachezwa Jumapili (Mei 26 mwaka huu) isipokuwa mechi kati ya Friends Rangers ya Dar es Salaam na African Sports ya Tanga itakayochezwa Jumamosi (Mei 25 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi.

 

Nayo mechi kati ya Abajalo ya Dar es Salaam na Kariakoo ya Lindi iliyokuwa ichezwe Jumamosi kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam sasa itachezwa Jumapili kwa vile siku hiyo uwanja huo utatumika kwa mazoezi ya Taifa Stars.

 

Mechi nyingine za RCL zitakazochezwa Mei 26 mwaka huu ni Machava FC ya Kilimanjaro dhidi ya Mpwapwa Stars ya Dodoma kwenye Uwanja wa Ushirika mjini Moshi, Stand United FC ya Shinyanga itakuwa mgeni wa Magic Pressure ya Singida kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida.

 

Polisi Jamii ya Bunda mkoani Mara na Biharamulo FC ya Kagera zitaumana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma. Mjini Kigoma kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika ni kati ya wenyeji Saigon FC na Katavi Warriors ya Katavi.

 

Nayo Kimondo SC ya Mbeya itakuwa mgeni wa Njombe Mji ya Njombe katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe. Mechi za marudiano zitachezwa kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu.

 

Timu zitakazofuzu kucheza raundi ya tatu zitacheza mechi za kwanza kati ya Juni 8 na 9 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitakuwa kati ya Juni 15 na 16 mwaka huu.

KIEMBA AKUBALI KUSAINI MSIMBAZI, KASEJA MAZUNGUMZO YAENDELEA, KAPOMBE BADO ANA MKATABA!!

DSC_3196

Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam

Kiungo matata wa wekundu wa Msimbazi Simba, Amri Athman Kiemba amekubali kuongeza mkataba wa kuichezea klabu hiyo kwa msimu ujao wa ligi kuu soka Tanzania bara.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Keptein Zacharia Hans Poppe ameimabia FULLSHANGWE kuwa Amri Kiemba wameshazungumza nae na kukubaliana kuongeza mkataba wake jambo ambalo limewapa raha sana kutokana na ubora wa mchezaji huyo aliyekuwa akitajwa kuihama Simba na kujiunga na Yanga msimu ujao.

“Kuhusu Kiemba tumeshaziba midomo ya watu, amekubali kwa moyo mkunjufu kuitumikia klabu yake msimu ujao, ni bonge la mchezaji, tunafurahi kuwa nae katika kikosi chetu”. Alisema Poppe.

Kuhusu nahodha Juma Kaseja, Poppe alisema wanaendelea kuzungumza nae ili kumsainisha mkataba mwingine huku wakikubaliana kuboresha maslahi yake klabuni hapo.

“Kuna watu wanazungumza na Kaseja, nadhani wanaendelea vizuri na mimi nitakutana nae tumalizane, haondoki ng`oo, atakuwepo Simba, cha msingi mashabiki wa Simba wawe watulivu”. Alisema Poppe.

Kuhus suala la Shomary Kapombe, Poppe amewatoa mashabiki wa kuwa mchezaji huyo bado ana mkataba na Simba hadi aprili mwakani na ataendelea kubaki msimbazi.

“Wanamsimbazi wasiwe na wasiwasi, Kapombe ni wetu na kila kitu kipo sawa”. Alisema Poppe.

Poppe alisema baada ya vijana hao kurudi kutoka Morocco wanapokwenda kuitumikia timu ya taifa, watasaini mikataba minono zaidi.

Kwa upande mwingine, Hans Poppe alisema zoezi la kuwasainisha mikataba mipya wachezaji wote wa timu hiyo linaendelea vizuri, ikiwemo wale waliopandishwa kutoka kikosi cha pili, yaani Simba B.

Poppe aliongeza kuwa  mwaka huu wanahitaji kufanya mambo yao kimya kimya ili kuwazuia wale wasiojua kusaka wachezaji ila wakijua Simba wamempa nani wanakimbilia kuwasainisha.

“Tunataka kuongeza wachezaji wengine wapya ili kuongeza nguvu ya kikosi, safari hii tunafanya kimyakimya kuwazuia ndugu zetu wasiojua kutafuta wachezaji na kufanya hesabu

TANZANIA,KENYA ZAVUTANA JUU YA VIJANA WALIOUWAWA NAROK

Liberatus-Sabas

Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas

MIILI  mitatu ya watanzania wa jamii ya Kisonjo waliouwawa katika eneo la Narok wilayani Kajiado nchini Kenya imeingia katika sura mpya mara baada ya Serikali ya Tanzania kushindwa kuirejesha nchini miili hiyo huku serikali ya Kenya ikidai kuwa hawakuwa watanzania

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas alisema kuwa tayari mtu mmoja ambaye ni askari polisi anashikiliwa na jeshi hilo kwa uchunguzi zaidi ingawaje alisema kwa sasa jina la askari huyo linahifadhiwa kwa ajili ya  upelelezi

Sabas alisema kuwa wanamshikilia askari huyo kwa kosa la upotevu wa silaha ambayo inasadikiwa kuwa ilitumika katika tukio uhalifu linalohusishwa na mauji ya vijana hao watatu wa Kitanzania nchini Kenya.

Kuhusu Marehemu hao, kamanda amesema kuwa Serikali ya Kenya kupitia Jeshi lake la polisi ndio wanajukumu la kurejesha  Miili yao hapa nchini .

Awali Msemaji wa familia tatu za marehemu hao,Pasto Webo alidai kuwa askari wa kituo cha polisi Loliondo waliwatoza kiasi Milioni mbili na nusu kwa ikiwa kama gharama za kuwasafirisha marehemu kutoka kenya kwa gari la Polisi kwa kiwango cha shilingi laki nane kwa kila mwili mmoja.

Lakini Kamanda wa Polisi alisema kuwa Jeshi hilo halina utaratibu wa kusafirisha marehemu na kwamba anafuatilia madai hayo na itakapobainika kuwa ni kweli watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Kuhusu kuhusika kwa polisi wa loliondo na kupotea kwa vijana wao watatu msemaji wa familia hizo tatu alidai kuwa May tatu mtoto wake ambaye ni Tibiti webo alikuja nyumbani kwake akiwa na askari polisi ambaye anajulikana kwa jina la Lazaro ambapo walikula chakula na walipoondoka kwa pamoja kijana huyo hakuonekana tena.

Pia alidai inasemekana kuwa kijana huyo alimpitia  rafiki yake ambaye amejulikana kwa jina la Kadogo anna ambapo tangu alipoondoka  tarehe tatu mwezi huu hawakuonekana tena  mpaka  hivi karibuni polisi walipowaletea ripoti pamoja na picha kuwa vijana wao wameuwawa vibaya Narok

“Tulipotazama hizo picha tuliweza kuwatambua vijana wetu wawili  lakini pia alikuwepo mwingine wa tatu ambaye tunadhani kuwa anatokea kijiji cha jirani”

Inadaiwa kuwa polisi waliwaeleza kuwa vijana wao waliuwawa katika tukio la ujambazi  katika eneo la Narrok  ambapo ilidaiwa kuwa waliwavamia wafanyabiashara kwa ajili ya kuwapora fedha lakini wakauwawa na wananchi wenye hasira kali

Katika tukio hilo vijana hao walikutwa na silaha ambayo inaaminika kuwa walipewa na askari wa kituo cha polisi cha loliondo.

Akizungumza kwa njia ya simu kutoka Dar es salam balozi wa Kenya Nchini Tanzania ,Mutinda Mutiso alidai kuwa vijana waliouwa sio watanzania bali ni wa Kenya huku akiongeza kuwa tukio hilo lilitokea wakati yeye akiwa nchini humo.

 

MRADI WA UENDELEZAJI MIJI TANZANIA (TSCP) WAENDELEA VIZURI

0016 Wawakilishi wa Mradi wa TSCP na Wawakilishi wa World Bank katika picha ya pamoja, hivi karibuni walipotembelea Mwanza katika kubaini utekelezaji na maendeleo ya maeneo mbalimbali ya mradi huoWawakilishi wa Mradi wa TSCP na Wawakilishi wa World Bank katika picha ya pamoja, hivi karibuni walipotembelea Mwanza katika kubaini utekelezaji na maendeleo ya maeneo mbalimbali ya mradi huo.JPG SONY DSCTimu ya wataalamu kutoka  OWM-TAMISEMI-katika Mradi wa Mpango Miji Mkakati (TSCP ) Pamoja na wawakilishi kutoka Benki ya Dunia pamoja na Ubalozi wa Denmak wakikagua Ujenzi wa Barabara zinazoendelea kujengwa kupitia mradi wa TSCP katka  Mnispaa ya Mtwara Mikindani katika kubaini utekelezaji na maendeleo ya maeneo mbalimbali ya mradi Tanga - Ujenzi wa mifereji ya maji ukiendeleaHii ni baadhi ya mifereji iliyokamilika baada ya ujenzi huko Tanga.

………………………………………………………….

Toka uzinduzi wa mradi wa uendelezaji Miji. Tanzania Strategic Cities Project (TSCP),uanze
mnamo mwaka 2010.  Umekuwa ukiboresha huduma za msingi mijini kufikia
walengwa. Mradi huu wa uendelezaji miji Tanzania umeundwa kwa ajili ya kukabili
changamoto mbalimbali za Miji ya Tanzania. Mradi huu unatekelezwa na Halmashauri
nchini, chini ya usimamizi wa Ofisi ya Waziri Mkuu – Tamisemi.
Mradi huu ni mkopo kutoka Benki ya Dunia na ruzuku kutoka Danida.
Mwanzoni mwa wiki mwandishi wetu aliongea na Kaimu Katibu Mkuu wa Tamisemi Bwn.
Jumanne Sagini ambaye alikua na haya ya kusema “Mradi wa uendelezaji miji Tanzania
upo na una lengo la kuboresha viwango na kurahisisha ufikiwaji wa huduma za msingi
Mijini kwa kukarabati na kupanua miundombinu ya Miji pamoja na kuziimarishia uwezo
taasisi husika katika kuboresha mapato na usimamizi wake”
Bwn. Jumanne Sagini aliendelea kusema “Mradi huu umegawanyika katika maeneo
makuu matatu ambayo ni Miundo mbinu na huduma za miji; Uimarishaji wa Taasisi
pamoja na Usimamizi wa Mradi; na ni miji saba tu ndiyo itakayofaidika na mradi huu.
Miji yenyewe ni Tanga, Arusha, Mwanza, Kigoma, Mbeya, Mtwara, na Dodoma, Kwa
Mji wa Dodoma, Mradi unatekelezwa na Halmashauri ya Manispaa Dodoma Ustawishaji
Makao Makuu Dodoma (CDA)”.
Mradi huu unagharama ya $ 175.5, ambapo $162.8 ni mkopo kutoka Benki ya Dunia na
$12.7 ni ruzuku kutoka DANIDA. Mkopo wa Benki ya Dunia ni kwa ajili ya maeneo ya
Miundombinu na huduma za miji, wakati ruzuku kutoka DANIDA itagharamia uimarishaji
wa Taasisi katika kutekeleza majukumu yake.
Ili kujua kwa undani zaidi kuhusu mradi huu, Mwandishi wetu wa habari aliongea na
Mratibu wa mradi huu Mhandisi Davis Ben Shemangale.
Mhandisi Davis Ben Shemangale alielezea : “Mradi huu ni njia ya kutekeleza dhana ya
kugatua madaraka toka Serikali Kuu kwenda kwa umma, mradi huu wa TSCP
unaendeshwa na Halmashauri husika kwa kuchagua na kuitekeleza miradi kwa kadri ya
vipaumbele vyao”.
Mhandisi Davis Ben Shemangale alimalizia kwa kusema “mradi huu umewekwa katika
awamu tatu hadi nne kwa kila mji na mpaka sasa wakandarasi kwa awamu zote
wamekwisha anza kazi” aliendelea kwa kusema “wakandarasi kwaajili ya kutekeleza
awamu ya kwanza walianza kazi Novemba mwaka 2011 na awamu ya pili walianza kazi
mwezi June mwaka 2012 ambapo awamu ya tatu na ya nne walianza kazi mwezi
Novemba 2012”

NAPE YUPO BERLIN, UJERUMANI

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, CCM, Nape Nnauye (katikati) akikaribishwa na baadhi ya viongozi wa chama cha SPD mjini Berlin, Ujerumani alipowasili jana kuhudhuria sherehe za miaka 150 ya kuzaliwa kwa chama hicho cha SPD.

LIONEL MESSI NDOTO ZA KUTWAA UBINGWA WA DUNIA ZAENDELEA KUSUMBUA KICHWA CHAKE!!

Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com

Mshambuliaji nyota wa klabu ya Fc Barcelona, raia wa Argentina Lionel Andrew Jorge Messi amesema tangu aondoke nchini kwake akiwa na miaka 13 kujiunga na Real Madrid anaota kutwaa ubingwa wa kombe la dunia ambao hajawahi kushinda na kikosi cha timu ya taifa licha ya kuwa mchezaji nyota ngazi ya soka la klabu.

Messi aliyeshinda tuzo ya mchezaji bora wa FIFA mara nne mfululizo toka mwaka 2009 ameshida kombe la ligi ya mabingwa barani ulaya mara tatu na kombe la ligi kuu nchini Hispania mara sita amesema sasa kila usiku ndoto za kutwaa ubingwa wa dunia zinamsumbua sana.

Messi ameshinda kila kitu kwa sasa kasoro kombe la dunia, hivyo anaota kufanya hivyo ili kuwafurahisha mashabiki wa Argentina.

Nyota huyo alisema kuwa alisimuliwa na wazazi wake kuwa tangu akiwa na miaka miwili au mitatu alikuwa anaonesha kuwa atacheza soka kutokana na kupenda kushika mpira.

“Tangu nikiwa mdogo sana nilikuwa nawaza kuwa mchezaji wa kimataifa, nimefanikiwa kwa kiwango fulani, lakini nadhani ni muhimu sana kwangu kushinda kombe laq dunia kwa sasa nikiwa na miaka 25″. Alisema Messi.

Star in the making: Lionel Messi moved to Barcelona from Argentina as a 13-year-oldNYOTA A UKWELI: Lionel Messi alijiunga na Barcelona kutoka Argentina akiwa na miaka 13

Goal: In our exclusive video interview, Messi reveals his desire to win the World Cup with ArgentinaKatika mahojiano maalumu  Messi amesema anatamani sana kushinda kombe la dunia kwa sasa akiwa na timu ya taifa lake Argentina

messifilmbanner
No 1: Messi's elusive dribbling and prolific goal-scoring have earned him the reputation as the world's bestUwezo wa Messi kupiga chenga na kufunga mabao kumemfanya awe mchezaji bora zaidi duniani
Mine: Messi has won the World Player of the Year award four times in a row from 2009TUZO YAKE: Messi ameshinda tuzo ya FIFA mara nne mfululizo toka mwaka 2009
Glittering: The Argentine won his sixth La Liga title with Barcelona this seasonSI MCHEZO: Messi ameshinda kombe la sita msimu huu katika ligi ya Hispania akiwa na FC Barcelona
Glittering: The Argentine won his sixth La Liga title with Barcelona this season
Glittering: The Argentine won his sixth La Liga title with Barcelona this season
Double: Messi celebrates his second Champions League triumph in 2009 after beating Manchester UnitedUBINGWA: Messi alipokuwa akishangilia ubingwa wa UEFA mwaka 2009 baada ya kuifunga Manchester United
Triple crown: Messi lifts his third Champions League in 2011 after Barcelona again beat Manchester United Messi akinyanyua mzigo wa UEFA mwaka 2011 baada ya kuwafunga United kwa mara nyingine
Out: In Messi's two World Cups, Argentina were beaten by Germany in the quarter-finals in 2006 and 2010NJE:  Messi katika mchezo  dhidi ya Nigeria kombe la dunia mwaka 2010 nchini Afrika Kusini ambapo walifungwa katika hatua ya nusu fainali mnamo mwaka mabao
Leader: Diego Maradona's side were beaten 4-0 by Germany in the quarter-finals of the 2010 World CupKIONGOZI: Diego Maradona alitandikwa maboa  4-0  na Ujerumani katika mechi ya robo fainali ya kombe la nia mwaka 2010 nchini Afrika kusini

Spearhead: Messi will lead Argentina's quest for World Cup glory in 2014 on Brazilian soilITAKUWAJE?: Messi ataiongoza Argentina kutafuta ubingwa kombe la dunia mwakani nchini Brazil

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA UTOKOMEZAJI WA UGONJWA WA FISTULA, JIJINI DAR

 3Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na baba wa mtoto, Elizabeth Nora kutoka Dodoma aliyelazwa katika Hospitali ya CCBRT, wakati Makamu alipofika hospitalini hapo leo Mei 23, 2013 kwa ajili ya kushiriki katika  Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Utokomezaji wa Ugonjwa wa Fistula. Picha na OMR 4Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Dokta wa Hospitali ya CCBRT, wakati alipokuwa akitembelea katika wodi za wagonjwa waliolazwa katika Hospitali hiyo, alipofika hospitalini hapo leo Mei 23, 2013 kwa ajili ya kushiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Utokomezaji wa Ugonjwa wa Fistula. Kulia ni Mtoto Boniface Patrick akiwa na Baba yake, Patrick Luwao, Wakazi wa Dodoma, akiwa amelazwa baada ya kufanyiwa upasuaji na kuongezewa sehemu ya mguu uliokuwa mfupi. Picha na OMR 5Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Stellah Nzyemba, ambaye awali alikuwa mgonjwa na baada ya kutibiwa katika Hospitali hiyo ya CCBRT na kupona ameajiriwa ili kuwasaidia wagonjwa wa Fistula. Makamu alifika hospitalini hapo leo Mei 23, 2013 kwa ajili ya kushiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Utokomezaji wa Ugonjwa wa Fistula. Picha na OMR 8Makamu wa Rais Dkt Bilal, akimjulia hali mtoto mgonjwa aliyelazwa katika Hospitali hiyo ya CCBRT. 10Makamu wa Rais Dkt. Bilal, akiwasili katika eneo lililoandaliwa maalum kwa ajili ya kufanyia shughuli za maadhimisho hayo. 11Balozi wa Uingereza nchini, Dianna Melrose, akizungumza wakati wa maadhimisho hayo. 12Balozi wa Ugonjwa wa Fistula, Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Mwana FA, akisoma hotuba yake kuhusiana na kuzunguka katika baadhi ya mikoa na kutoa ujumbe kwa wananchi na hasa kina mama kuhusu Ugonjwa huo.

13Wasanii 21 walioungana na kuimba wimbo wa Kidole kimoja, wakitoa burudani jukwaa 15Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Utokomezaji wa Ugonjwa wa Fistula, yaliyofanyika leo Mei 23, 2013 Jijini Dar es Salaam. Picha na OMR

16Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Utokomezaji wa Ugonjwa wa Fistula, yaliyofanyika leo Mei 23, 2013 Jijini Dar es Salaam. Picha na OMR

RAIS DKT.JAKAYA KIKWETE AKUTANA NA WANANDINGA WA TIMU YA TAIFA “TAIFA STARS”LEO IKULU!!

Picha na 1Rais Jakaya Kikwete akiongea na wachezaji wa timu ya mpira ya Taifa, Taifa Stars leo Ikulu jijini Dar es salaam alipokutana nao kuwapa hamasa waweze kupata ushindi katika mchezo wao dhidi ya Moroco utakaochezwa Juni 7, na michezo  mingine  ikiwa ni hatua ya kuiwezesha timu hiyo kukata tiketi ya  kushiriki  mashindano ya kombe la dunia mwaka 2014. Picha na 2Rais Jakaya Kikwete akiongea na wachezaji wa timu ya mpira ya Taifa, Taifa Stars leo Ikulu jijini Dar es salaam alipokutana nao kuwapa hamasa waweze kupata ushindi katika mchezo wao dhidi ya Moroco utakaochezwa Juni 7, na michezo  mingine  ikiwa ni hatua ya kuiwezesha timu hiyo kukata tiketi ya  kushiriki  mashindano ya kombe la dunia mwaka 2014. Picha na 4Rais Jakaya Kikwete akiwaaga wachezaji wa Timu ya Taifa Stars mara baada ya kukutana nao leo Ikulu Jijini Dar es salaam kuwahamasisha washinde mchezo dhidi ya timu ya Taifa ya Moroco utakaofanyika June 7 ikiwa ni sehemu ya Taifa Stars kutafuta ticketi ya kucheza mashindano ya Kombe la Dunia. Picha na 5Meneja wa Timu ya Taifa Stars Bw. Mukebesi akiteta jambo na Kepteni wa Timu ya Taifa Stars Juma Kaseja Ikulu jijini Dar es salaam walipokutana na Rais Jakaya Kikwete. Picha no 3Wachezaji wa Timu ya Taifa Stars wakipata chakula walichoandaliwa na Rais Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo alipokutana nao kuwatakia ushindi katika mchezo wao dhidi ya Moroco. Picha na 6Rais Jakaya Kikwete akiwa katika Picha ya Pamoja na wachezaji wa Timu ya Taifa , Taifa Stars, viongozi wa Wizara ya Habari, Vijana ,Utamaduni na Michezo na Viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Picha na 7Rais Jakaya Kikwete akiwa katika Picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Taifa , Taifa Stars Ikulu jijini Dar es salaam.

Picha na Aron Msigwa – MAELEZO na Freddy Maro Ikulu.

Na Veronica Kazimoto –MAELEZO

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo amekutana na timu ya Taifa (Taifa stars) kwa lengo la kuitia moyo katika mechi ijayo kati yake na timu ya Moroco ikiwa ni harakati za Tanzania kutafuta tiketi ya kucheza fainali za kombe la Dunia kwa mara ya kwanza  mwaka 2014.

Rais Kikwete ameiambia timu hiyo kuwa ina uwezo mkubwa  wa kusonga mbele kutokana na uwezo mkubwa waliouonesha katika mchezo wao  dhidi ya Gambia ambapo walifanikiwa kupata  ushindi wa bao 2-0.

 “Maadamu mara ya kwanza mliwashinda Gambia, hakikisheni pia mnapata ushindi dhidi ya Moroco, mkishinda tunafurahi sana na mkishindwa tunanyong’onyea sana,” amesema Rais Kikwete.

 Aidha amempongeza kocha wa timu hiyo Kim Poulsen  pamoja na Kamati ya Taifa ya ushindi ya Taifa stars kwa kuisaidia timu hiyo kiasi cha shilingi milioni 30 ikiwa ni mkakati wa kuiongezea nguvu kwa hatua iliyofikia  na kuwataka wachezaji kujituma ili kuwafurahisha watanzania ambao hivi sasa wanaipenda timu yao ya Taifa.

 Nae Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Fenera Mukangara amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa michezo nchini  ili kuondoa changamoto zinazoikabili timu hiyo.

 Kwa upande wake Kocha Poulsen, amemshukuru Rais Kikwete kwa kuwakaribisha na kuwatia moyo ambapo ameahidi kuifundisha vizuri timu hiyo ili kuhakikisha kuwa wanapata ushindi.

 Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake nahoidha wa timu hiyo Juma Kaseja amemshukuru Rais Kikwete na kuahidi kujituma kwenye mazoezi na hatimaye kuibuka washindi  kwenye mechi zijazo.

 Taifa stars ambayo inakamata nafasi ya pili katika kundi C inatarajia kucheza ugenini na Morocco mnamo Juni 7 mwaka huu.

WAKAZI WA MBEZI BEACH WAHAMASISHWA KUPELEKA WATOTO KUPIMA AFYA BURE

DR WATOTO 059 bMkurugenziwahospitaliya IMTU Dkt. Ali Mzige akisitiza umuhimu wa wazazi kujali afya za watoto na kufuatilia uzito wa watoto wao walio chini ya umri wa miaka mitano alipokua akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam ,Kulia kwake ni Bw.Saibal Sarbadhikari Meneja Mkuu wa umoja wa BANGO SANGHO.

DR WATOTO 064 bMkurugenzi wa hospitali ya IMTU Dkt. Ali Mzige akihamasisha wananchi kujitokeza katika zoezi la upimaji afya bure kwa watoto walio chini ya miaka mitano,utakaofanyika jumapili Mei 26 katika hospitali hiyo iliyopo Mbezi Beach. Kushoto kwake ni Bw.Saibal Sarbadhikari Meneja Mkuu wa umoja wa BANGO SANGHO.

Na Genofeva Matemu -MAELEZO

HOSPITALI ya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Tekinolojia (IMTU hospital) kwa kushirikiana na Umoja wa Jamii ya watu kutoka India Bengali waliopo nchini Tanzania watatoa huduma ya upimaji afya bure jumapili Mei 26 mwaka huu  kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano wanaoishi maeneo ya Mbezi Beach .

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa hospitali ya IMTU Dkt. Ali Mzige alipokua akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusiana na afya ya mtoto na umuhimu wa maziwa ya mama hasa kwa watoto walio chini ya miezi 6 .

Dkt. Mzige amesema wanakusudia kupima uzito, presha na kutazama afya ya kinywa kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano ambapo watatumia vifaa maalumu vya upimaji presha kwa watoto hao.

“Tutapima uzito ambao takwimu zake ni Kg 10 kwa mtoto wa mwaka mmoja, Kg 11 kwa mtoto wa mwaka mmoja na nusu, Kg 12 mtoto wa miaka 2, Kg 13 kwa mtoto wa miaka miwili na nusu, Kg 14 kwa mtoto wa miaka 3, Kg 15 kwa mtoto wa miaka mitatu na nusu, Kg 16 mtoto wa miaka 4, Kg 17 mtoto wa miaka minne na nusu, na Kg 18 ni kwa mtoto wa miaka mitano”, amesema Dkt. Mzige.

Akirejea matokeo ya sensa ya mwaka 2012 Dkt. Mzige amesema matokeo hayo yalionesha kuwa asilimia 42 ya watoto chini ya miaka mitano hapa nchini wamedumaa, ambapo asilimia 16 wana uzito pungufu (Underweight) na asilimia 5 wamekonda (Marasmic) wako kwenye rangi nyekundu ya kadi za watoto za kliniki.

Aidha Dkt. Mzige ameishauri jamii kula lishe bora na kamili sababu lishe bora huanzia nyumbani hivyo ni jukumu la jamii kupata elimu  ya chakula bora na mlo kamili wenye kujenga afya bora kwa watoto.

Zoezi la upimaji wa afya kwa watoto limeanza rasmi mwaka huu na linatarajiwa kufanyika kila mwaka au mara mbili kwa mwaka kwa kushirikiana na uhisani wa Bango Sangho jamii ya wahindi wanaoishi hapa nchini  ambao wamekua wakitoa vifaa vya kupimia afya za watoto.

 

 

 

 

WASANII 320 KUJIMWAGA JUKWAANI KUONESHA VIPAJI SIKU YA TAMASHA LA MASTAA CHIPUKIZI!!

101_0267

Mwenyekiti wa Shiwata, Caasim Taalib (Kulia)

TAMASHA la Mastaa chipukizi zaidi ya 320 la mwezi Mei litafanyika Jumapili 26, 2013 katika ukumbi wa Starlight Hotel kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 10 jioni.

 Mwenyekiti wa Shiwata, Caasim Taalib alisema maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika  na vikundi vya sanaa vya Kaole, Splendid, Super Shine Taarab, Five Star Modern Taarab pamoja na wasanii mbalimbali wa Bongo Flava, Maigizo,Ngoma, Dansi na Sarakasi nao wamethibitisha kushiriki.

 Taalib alisema wasanii wakongwe wa bongo flava walioalikwa ni Stara Thomas, Ommy G na waigizaji wakongwe wa Kaole na Splendid wataonesha umahiri wao katika fani ya sanaa Kauli Mbiu ikiwa ni Kilio cha Msanii .

 Vikundi vingine vitakaonesha vipaji vyao ni Kepteni  Shaibu, Tanzania Disabled, Uyoga Boga Village, Ndafu Arts Group, CGC, Magengistar Crew, Dodo Arts Group, Culture Arts Group, Wachapa Kazi Academy, Soweto Picture, Shiwata Commedy, Mwavionelachi, Manuari Arts Group, Tandale Morden Taarab na Begeja Wushu,

 Wakati huo huo SHIWATA inawapongeza wote walioshiriki tamasha  la Aprili 27 ambako zaidi ya wasanii 300 walishiriki kuonesha vipaji.

 Pia Taalib amelipongeza Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) kwa ushirikiano wao mzuri na kuwaomba viongozi wengine wa bendi za muziki, taarab,vikundi vya sanaa,mapromota,maprodusa na wadau wote kushiriki katika matamasha haya ili kujenga ushirikiano wa pamoja.

UJUMBE WA MAMLAKA YA BANDARI TANZANI (PTA) WATAMBELEA RWANDA

photo

Ujumbe wa Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA) uko nchini Rwanda kubadilishana ujuzi na uzoefu na Rwanda kuhusu utekelezaji wa mradi wa kurahisisha na kuwezesha biashara (Trade Facilitation) kwa kutumia TEHAMA – Electronic Single Window System. Muda mfupi ujao TPA itaanza utekelezaji wa mradi huo kwa niaba ya wadau wote wa sekta ya usafirishaji, Forodha, wafanyaniashara na wadau wote wa Tanzania.
Ujumbe huo wa Tanzania unaongozwa na Mkuu wa mradi na Kaimu Mkurugenzi wa idara ya TEHAMA-TPA Ndg. Phares Magesa wa kwanza kushoto katika picha juu, wengine ni Mathayo Ntandu, Jesse Shali na Kilian Chale ambao ni maofisa wakuu TPA.

NBC YADHAMINI YATOA SOMO LA UJASIRIAMALI KWA WANAWAKE WA TANGA

IMG_7777Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa (kushoto) akipokewa na Mkuu wa  Kitengo cha Huduma za Fedha zinazofuata Kanuni za Kiislamu  ‘NBC Islamic Banking’ cha Benki ya Taifa ya Biashara, Yassir Masoud alipokwenda kufungua semina ya siku moja kwa wanawake wajasiriamali waislamu iliyoandaliwa na NBC  mjini Tanga leo. Katikati  ni Meneja Tawi la NBC Tanga Deusdedit Mashalla. IMG_7810Baadhi wa washiriki wa semina ya siku moja iliyoandaliwa na Benki ya NBC Kitengo cha Islamic Banking wakiwa katika semina hiyo jijini Tanga leo.

IMG_7830Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa akifungua semina ya siku moja kwa wanawake wajasiriamali waislamu iliyoandaliwa na Benki ya NBC Kitengo cha Islamic Banking mjini Tanga LEO. Kulia ni Mkuu wa kitengo hicho, Yassir Masoud na kushoto ni Meneja Operesheni wa NBC Tawi la Tanga Kibibi Said Kibao.

Na Mwandishi Wetu

Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kupitia kitengo chake cha Huduma za Kibenki zinazofuata kanuni za kifedha za Kiislamu inatarajia kuanzisha huduma ya mikopo kwa wafanyakazi ‘Islamic Group Finance’  kabla ya Septemba mwaka huu.

 Akizungumza wakati wa semina ya siku moja ya wanawake wajasiriamali wa Kiislamu jijini Tanga jana, Mkuu wa Islamic Banking wa NBC, Yassir Masoud alisema lengo la kuanzishwa kwa huduma hiyo ni kutoa fursa za mikopo kwa wateja wao wanaohudumiwa kwa kufuata kanuni za dini hiyo.

 Masoud aliwaambia wanawake waliohudhuria semina hiyo kwamba ili waweze kujikwamua kiuchumi, wanahitaji kujifunza mbinu za biashara, akisisitiza kwamba hata mafundisho ya Kiisllamu yanatoa maelekezo kuhusu utafutaji wa riziki.

 ”Uislam umehimiza mambo ya uwekezaji, Uislamu unahimiza masuala ya mali maandiko yakisema kwamba kutafuta riziki ni sawa na kutafuta fadhila za Mwenyezi Mungu,” alisema.

 Akifungua semina hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga bibi Chiku Galawa aliwahimiza wanawake mkoani humo kujizatiti kwenye ujasiriamali ili kusaidia juhudi za serikali katika kuinua maendeleo yasiyoridhisha ya mkoa huo.

Alisema kuwa kwa kupitia semina hiyo, NBC imefungua njia mpya yenye matumaini kwa wanawake wa Tanga, njia ambayo mashirika mengine yanapaswa kuifuata.

“NBC ni moja kati ya benki kongwe yenye mtanda mpana kuliko zote nchini na imekuwa mstari wa mbele ikishirikiana na watu mbalimbali katika kuboresha maisha ya Watanzania,” alisema.

Katika siku za hivi karibuni, NBC imekuwa ikiwekeza zaidi katika kuelimisha jamii, hususan wajasiriamali kupitia semina na warsha mbalimbali huku ikishirikiana na makampuni mengine.

Mwishoni mwa mwaka jana, benki hiyo iliandaa mkutano wa wajasiriamali wadogo wadogo wa jijini Dar es Salaam kwa ushirikiano na shirika lisio la kiserikali linalojishughulisha na vijana, YESi.

NBC pia ni wadhamini wa Top 100 Midsize Companies Survey ambayo inaendeshwa kwa ushirikiano na KPMG kuyasaka na kuyazawadia makampuni ya kati yanayokuwa kwa kasi.

“Sekta ya Biashara ndogo ndogo na za kati ni muhimu katika kukuza uchumi nchini, na ni sekta inayoweza kutoa nafasi za ajira kwa wananchi wengi. NBC wametambua hilo,” alisema.

Aliishukuru benki hiyo na kuishauri iendelee kutoa mafunzo kwa wahusika wa sekta hiyo na kuwawezesha wajasiriamali kukuza biashara zao na hatimaye kuinua uchumi wa nchi.

Rais Kikwete amwapisha Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria na Mabalozi Wapya wanne

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo ikulu jijini Dar es Salaam amemwapisha Jaji  Aloycius Mujuluzi kuwa Mwenyekiti wa  tume ya kurekebisha sheria pamoja na mabalozi wanne watakaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi.Mabalozi walioapishwa leo ni pamoja na Balozi mpya katika umoja wa Falme za kiarabu(UAE) Mbarouk Nassor Mbarouk,Balozi mpya wa Tanzania nchini Uholanzi Wilson Masilingi,Balozi mpya wa Tanzania katika visiwa vya Commoro Chabaka Kilumanga na Mwakilishi wa  kudumu Tanzania Umoja wa mataifa Geneva Balozi Modest Jonathan Mero.

8E9U8078Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal  na Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe wakiwa katika picha ya pamoja na mabalozi wapya waliopaishwa leo ikulu jijini Dar es Salaam.aliyesimama mbele kushoto no Balozi Liberata Mulamula anayekuwa Balozi Mpya wa Tanzania nchini Marekani.Waliosimama nyuma kutoka kushoto ni Balozi mpya wa Tanzania Uholanzi Wilson Masilingi,Balozi mpya wa Tanzania katika visiwa vya Commoro Chabaka Kilumanga,Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa Geneva Balozi Modest jonathan Mero na Balozi mpya wa Tanzania katika falme za Kiarabu(UAE)Mbarouk Nassor Mbarouk.Kabla ya uteuzi Balozi Liberata Mulamula alikuwa msaidi wa Rais Masuala ya kidiplomasia na aliwahi kuwa katibu mkuu wa nchi za  Maziwa Makuu.(picha na Freddy Maro) Balozi Kilumanga-Commoro Akiapa Balozi Masilingi-Uholanzi akiapaBalozi Masilingi-Uholanzi akiapa Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (UAE) akiapaBalozi Mbarouk Nassor Mbarouk (UAE) akiapa Balozi Mero-Geneva akiapaBalozi Mero-Geneva akiapaJaji Aloycius Mujuluzi akiapaJaji Aloycius Mujuluzi akiapa

MKUTANO WA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI WAFANYIKA VISIWANI ZANZIBAR

DSCF0631Bw Sihaba Vuai afisa mazingira ofisi ya makamu wa kwanza wa rais zanzibar akizungumza kuhusu hali ya mazingira ya zanzibar na madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi katika mkutano wa kamati ya kitaifa ya wataalam ya mabadiliko ya tabia nchi unaoendelea mjini zanzibar

DSCF0633Wanakamati ya kitaifa ya kitaalam ya mabadiliko ya tabia nchi wakimsikiliza mtoa mada hayupo pichani katika mkutano unaoendelea mjini zanzibar (Picha na Evelyn Mkokoi)

TIMU KUTOKA GHANA YAIBUKA MSHINDI WA NUSU FAINALI YA GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™NA KUIACHA TIMU KUTOKA KENYA IKIAMBULIA NAFASI YA PILI

 Francis Wangari & Kepha Kimani - Kenya (2)Washindi wa pili wa nusu fainali ya kwanza ya Guiness Football Challenge Francis Wangari(kushoto) na  Kepha Kimani(kulia) kutoka Kenya  katika picha ya pamoja na waendeshaji wa kipindi cha Pan-Africa Guinness Football Challenge Larry Asego na Mimi Kalinda.  Naab Jonathan Baan & Desmonf Odaano - Ghana2 Washindi wa kwanza wa nusu fainali ya kwanza ya Guiness Football Challengekutoka Ghana Naab Jonathan Baan(kushoto) na Desmond Odaano(kulia) katika picha ya pamoja na waendeshaji wa kipindi cha Pan-Africa Guinness Football Challenge Larry Asego na Mimi Kalinda.

………………………………………………..

Dar es Salaam: Jana usiku kupitia televisheni za ITV na Clouds TV nusu fainali ya kwanza kabisa ya GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ ilirushwa hewani na katika runinga Afrika nzima   ambapo timu ya Ghana ilionesha ni kwanini ni timu bora ambayo ndiyo imejishindia pesa nyingi mpaka sasa.

Jonathan Nabb na Desmond Odaano walionesha uwezo na  ujasiri wao walipoibuka washindi zidi ya wapinzani wao timu kutoka Kenya katika mchezo wa jana. Katika hatua ya pesa ukutani walifanikiwa kulenga lango namba nne na hivyo kupata dola za kimarekani 12,000 wanazoziongeza katika dola 8,500 walizokuwa nazo awali katika hatua ya robo fainali.

 Wakenya Francis Ngigi na Kepha Kimani ambao ni washindi wa pili katika nusu fainali hii wataungana na Ghana katika fainali.Ingawa waliikosakosa hatua ya ukuta wa pesa wa Guinness bado wana nafasi ya kuwa mabingwa katika fainali.

 Wapenzi wa kipindi hiki cha Guinness football challenge wanaweza kupima maarifa yao katika soka kupitia GUINNESS® VIP™.  Wanaweza kufanya hivyo kwa kujisajili bure kabisa katika m.guinnessvip.com kwa kupitia simu ya mkononi.  

 Usikose kufuatilia ukurasa wa facebook wa GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE kwa habari mbalimbali.

-www.facebook.com/guinnesstanzania

Chilly Willy, Dodoma Wine, CXC Africa kudhamini Redds Miss Sinza 2013

imagesNa Mwandishi Wetu
WAKATI jumla ya warembo 13 wamejitokeza kuwania taji la Redds Mid Sinza 2013 iliyopangwa kufanyika Juni 7, kwenye ukumbi wa Meeda Club, kampuni ya Tanzania Distillers Limited (TDL),  kinywaji cha Chilly Willy na kampuni ya  CXC Africa zimejitokeza kudhamini mashindano ya Redds Miss Sinza 2013 yaliyopangwa kufanyika kwenye ukumbi w Meeda Club Juni 7.
Mratibu wa mashindano hayo, Majuto Omary alisema jana kuwa TDL imedhamini mashindano hayo kupitia kinywaji chake cha Dodoma Wine ambao pia mwaka jana walidhamini mashindano hayo.
Majuto alisema kuwa wamepata faraja kubwa mwaka huu baada ya idadi ya warembo kuongezeka sambamba na wadhamini. Wadhamini wengine ni kampuni ya TBL kupitia Redds Original, Clouds FM, Fredito Entertainment,  Sufiani Mafoto Blog na Saluti5.
Alisema kuwa warembo wameitikia wito katika mashindano hayo kwani wanataka kutwaa taji la Miss Redds Miss Tanzania ambalo Sinza ni watetezi kupitia mrembo wake Brigitte Alfred.
“Bado tunahitaji warembo zaidi ili kupamba shoo yetu ambayo ni ya mwisho kwa kanda ya Kinondoni. Pia tunawaomba wadhamini wengine kujitokeza kwani Miss Sinza 2013 ni zaidi ya promosheni na burudani,” alisema Majuto.
Mpaka sasa warembo 13 wamejitokeza katika mashindano hayo na wapo mazoezini chini ya Miss Tanzania Top Model, Mwajabu Juma.

Flaviana Matata atoa wito kwa serikali kuhusu ajali ya MV Bukoba

MARIAMiss Universe Flaviana Matata akiwa na Mkurugenzi wa Compass communicayion, Maria Sarungi wakiwasha mshumaa kwenye kaburi la Marehemu mama yake mzazi aliyefariki katika ajali ya MV Bukoba mwaka 1996.
……………………………………..
Na Mwandishi Wetu
MWANAMITINDO wa kimataifa wa Tanzania, Flaviana Matata ameiomba serikali kutangaza Mei 21 ya kila mwaka kuwa siku maalum ya maombolezo ya wasiku maalum ya maombolezo  ya wahanga wa MV Bukoba.
Ajali ya MV Bukoba ilitokea Mei 21 mwaka 1996 na kuua watu zaidi ya 1,000 na serikali kutangaza siku tatu za maombolezo ya kutokana na kuzama kwa meli hiyo iliyotokea kwenye  Ziwa Victoria. Katika ajali hiyo, Flaviana alipoteza mama na kaka yake.
Flaviana ambaye kwa sasa anafanya shughuli za kuonyesha mitindo nchini Marekani na Uingereza, amekuwa mstari wa mbele kuadhimisha siku hiyo kwa kupitia taasisi yake ya Flaviana Matata Foundation.
Akizungumza Kwa niaba ya Flaviana Matata Mkurugenzi wa Compass Communications Company Limited Maria Sarungi Tsehai alisema pamoja na ajali hiyo kuua watu wengi, lakini inasikitisha kuona jambo hilo kwa sasa limekuwa kama kumbukumbu kwa wahanga wa ajali hiyo tu na si vinginevyo.
Maria ambaye alisema hayo katika misa maalum ya kumbukumbu ya ajali hiyo iliyofanyika kwenye makabuli ya Igoma, Mwanza alisema kuwa wakati umefika sasa wa kutangaza siku ya kitaifa ya maombolezo na kwani ajali hiyo imeacha Watanzania wakiwa na huzuni kubwa.
Alisema kuwa wanashukuru sana kwa miaka hii miwili wamepata ushirikiano mzuri kutoka kwa Marine Service Company Limited na kampuni ya ndege ya Fastjet, ambapo mwaka jana walikabidhi vifaa vya kujiokolea (maboya) 500.

Veronica Lugenzi kushiriki onyesho la mavazi jijini Dar es salaam

02bNa Mwandishi Wetu

Mbunifu wa mitindo anayekuja kwa kasi,wa Tanzania Veronica Lugenzi kwa kushirikiana na wabunifu wengi kutoka nchi za Marekani, Kenya na Zambia watafanya maonyesho ya mavazi kwa mara ya kwanza kesho Jumamosi kwenye ukumbi wa Ledger Plaza wa hotel ya Bahari Beach.

Onyesho hilo linalojulikana kwa jina la Vibe Runway ni la kihistoria kwa mujibu wa Veronica kutokana na kushirikisha wabunifu wachanga, wazoefu na wa kimataifa.
Alisema kuwa wamepanga kuonyesha mavazi ya kisasa zaidi katika onesho hilo  huku wakipata burudani ya muziki kutoka kwa wasanii wa hapa nyumbani na wa nchi jirani.
Baadhi ya wabunifu maarufu ambao wataonyesha mavazi yao ni Asia Idarous Khamsin ambaye amepata umaarufu mkubwa kutokana na onyesho lake la Lady in Red na Kanga Za Kale.
Katika onesho hilo lililodhaminiwa na Vayle Springs, TeenSpot Magazine,, Gonga Mx Blog, Missie Popular Blog na Ledger Plaza Bahari Beach Hotel, pia litawashirikisha wabunifu wengine wa mavazi kama Kemi Kalikawe, B Designes na VS: VERNIC ambao wote wanatoka Tanzania.
Mbunifu kutoka Kenya ni Mohamed Bana ambapo Estelle Mantel ataiwakilisha Zambia na kutoka Marekani (Washington DC)  ni Ibrahim Pure.
Wanamitindo mbali mbali maarufu wa Tanzania watakuwepo katika onesho hiyo ambao ni, Meena Xirs, Rimaly Said Odemba,  Miss Universe- Winfrida Dominique, Miss Tanzania anayeshikilia taji la michezo, Mary Chizi, Macrida Joseph, Neema Doreen Sylvery, Rachida Ussuale na Lota Mollel.
“Pia kutakuwa na burudani kutoka kwa wasanii wa Tanzania wakiongozwa na mwakilishi wa Tanzania katika Big Brother Africa
Julio Batalia na wasanii wengine kama  G1, JC, Melisa John, Makjams na King Kapita.

PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI BUNGENI BAADA YA KUAHIRISHWA KUTOKANA NA (VURUGU ZA MTWARA)

1Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Dkt.  Emmanuel  Nchimbi  akitoa kauli ya Serikali Bungeni kuhusu vurugu zilizotokea Mkoani Mtwara. 2Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda  akiahirisha Bunge kutokana na vurugu zilizotokea Mkoani Mtwara 3Waziri wa Nchi  ofis ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)  Merry Nagu akiomba kutengua kanuni  ya Bunge  Na. 38 ili kuruhusu suala la vurugu za Mtwara kujadiliwa Bungeni.

4Waziri Mkuu Mhe.  Mizengo Pinda akizungumza na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Jaji Frederick Werema  pamoja na baadhi ya Mawaziri   ndani ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuahirishwa kwa kikao cha Bunge . 5Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Prof. Sospeter Muhongo  akizungumza na baadhi ya Mawaziri na Wabunge ndani ya ukumbi wa Bunge mara baada ya Spika wa Bunge kuahirisha bunge   6Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Emmanuel Nchimbi (Kushoto) akizungumza na mbunge wa Kinondoni Mhe. Iddi Azzan nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya bunge kuahirishwa. 7Wabunge wa Viti Maalumu wakiwa nje ya ukumbi wa Bunge baada ya Spika kuahirisha Bunge. Kutoka kushoto ni Mhe. Lucy Owenya(CHADEMA), Katikati  Mhe. Mkiwa Kimwanga(CUF) na kulia ni Mhe. Dkt. Merry Mwanjelwa(CCM).

8  Naibu Waziri wa mambo ya Ndani ya Nchi Pereira Ame Silima (Katikati), Naibu wa Viwanda na Biashara Mhe. Greygory Teu (kushoto) na mbunge wa Kilosa Mhe. Mustafa Mkullo wakizungumza nje ya ukumbi wa  Bunge.

9Kundi la Waandishi wa Habari wanaoripoti  habari za Bunge wakitoka ndani ya ukumbi huo mara baada ya Spika wa Bunge kuahirisha kikao cha Bunge.PICHA NA ZAWADI MSALLA-MAELEZO DODOMA