Archive for August 12th, 2012

TAARIFA KWA WADAU WOTE WA FULLSHANGWEBLOG.COM


Wapendwa
wadau wa mtandao wenu wa Umma Fullshangweblog tunaomba radhi kwa
usumbufu wowote utakaojitokeza kesho usiku wa kuamkia jumatatu kwa masaa
kadhaa kutokana na marekebisho madogo yatakayokuwa yakifanyika, yote
hii ni kuwaletea huduma bora kabisa kupitia hapahapa kwenye ukurasa wa
Fullshangwe, kwa sasa unaweza kututumia habari pia kupitia Email hii 
news@fullshangweblog.com,kikosi chetu kinawatakia siku njema wadau wote na mfungo mwema wa Ramadhan
.

RAIS AONANA NA RAIS MPYA WA GHANA, ATEMBELEA MASHAMBA YA MANANASI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Rais
John Dramani Mahama wa Ghana nyumbani kwake jijini  Accra leo Agosti 11,
2012 baada ya  kumtembelea na  kumpa pole ya msiba wa aliyekuwa Rais wa
nchi hiyo Marehemu John Evans Atta Mills aliyezikwa jana.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo  na Rais John Dramani Mahama wa Ghana nyumbani
kwake jijini  Accra leo Agosti 11, 2012  wakati alipomtembelea kiongozi
huyo mpya wa Ghana na  kumpa pole ya msiba wa aliyekuwa Rais wa nchi
hiyo Marehemu John Evans Atta Mills
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitazama manasi yakitayarishwa kwa
ajili ya kusafirishwa na kuuzwa nje ya nchi katika kiwanda cha  Bomarts
Farms Ltd. katika kitongoji cha Dobro nje kidogo ya jiji la Accra leo
Agosti 11, 2012
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitazama ukulima wa kisasa wa manasi
yanayolimwa  kwa ajili ya kuuzwa nje ya nchi katika shmaba la   Bomarts
Farms Ltd. katika kijiji cha Dobrokatika eneo la Nsawam  nje kidogo ya
jiji la Accra leo Agosti 11, 2012. Kulia kwake ni Mtendaji Mkuu wa
shamba hilo Bw. Anthony Botchway na mwenye suti ya buluu ni Waziri wa
Chakula na Kilimo Mhe Kwesi Ahwol
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia upandaji wa miche ya
 mananasi katika shamba la Koranco kijiji cha Obotweri nje kidogo ya
jiji la Accra. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Koranco Farms Ltd. Bw
Emmanuel B. Koranteng ambaye amekuwa akilima shamba la matunda kwa miaka
27. Mwalimu Nyerere aliwahi kumtembelea shambani hapo katikati ya miaka
ya 1980 kujionea ukulima huo wa matunda.


PICHA NA IKULU

TAMASHA LA DINI “LOVE TANZANIA” LILIVYOTIA FORA VIWANJA VYA JANGWANI JIJI DAR.

Pichani Juu na Chini ni Umati wa Watanzania uliofurika kwenye Tamasha la Dini lililopewa jina la LOVE TANZANIA linaloendelea katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam likiongozwa na Askofu Andrew Palau kutoka Marekani.
Vijana walioongoza na Askofu Andrew Palau wakitoa burudani na mafundisho ya dini kwa njia muziki.
Wana Dar es Salaam wakiendelea kumiminika katika viwanja vya Jangwani.
Mmoja wa Wahudumu katika Tamasha hilo akipata chakula cha mchana na familia yake Uwanjani hapo.
Umati wa watu ukiwa kwenye foleni ya kupata huduma ya chakula uwanja hapo.
Moja ya Magari na wafanyakazi wa Kampuni ya Usafi iliyopewa Zabuni ya kusafisha Manispaa ya Ilala Green Waste Pro Ltd likiwa limepaki katika Viwanja vya Jangwani kuhakikisha Usafi unazingatiwa Uwanjani hapo wakati tamasha la Dini lililopewa jina la LOVE TANZANIA likiendelea.
Pichani Juu na Chini ni moja ya michezo iliyofanyika kama sehemu ya burudani uwanjani hapo ambapo ilionekana kuvutia Umati wa Watanzania waliohudhuria tamasha hilo.
Vijana, Watoto kwa Wazee wakitazama mchezo wa mapikipiki.
Mmoja wa wafanyakazi wa Kampuni ya Green Waste Pro Ltd akihakikisha swala usafi linazingitiwa uwanjani hapo kama inavyoonekana.
Wananchi waliohudhuria tamasha hilo wakishuhudia mchezo wa Baiskeli.
Palikuwa hapatoshi Jangwani.
Ulinzi na Usalama kwa raia ulikuwepo.
Familia zikiendelea kula, kunywa na kufurahi uwanjani hapo.
Hili ni Jukwaa la kimataifa kutoka nchini Uganda maalum kwa ajili ya Tamasha lililopewa jina la LOVE TANZANIA likiongozwa na Askofu Andrew Palau kutoka nchini Marekani, haijawahi kutokea kusikia Sound na Mziki wa Ukweli nchini kwa mliohudhuria tamasha hili mtasema.