BENDI kongwe ya muziki wa dansi Tanzania, Msondo Ngoma ‘Baba ya Muziki’ imetoa ratiba yao katika wiki baada ya mpambano wao mkali na mahasimu wao Sikinde uliofanyika Jijini Dar es salaam pamoja na Zanzibar.
Baada ya kutoa burudani ya Iddi sasa wamerudi kwa ajiri ya kutoa burudani ambapo wamesema kuwa wataanza kutoa burudani siku ya Ijumaa watakuwa Leanders Club Kinondoni, Jumamosi watakuwa Kilimani Pub Staki Shari, na jumapili watamaliza wikiendi katika Ukumbi wa Max Bar Ilala Bungoni
“Msondo ipo kamili katika kutoa burudani na ndiyo maana imeamua kutoa ratiba, hivyo tunaamini mashabiki wetu watakuja kwenye maonesho yetu kwani bila wao sisi hatuwezi kusimama na kuimba,” alisema Super D.









