TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA MAZINGIRA KWA NCHI ZA AFRIKA

NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWEBLOG-ARUSHA

TANZANIA itakuwa ni mwenyeji wa mkutano wa kumi na nne wa mazingira
kwa nchi za Afrika utakaonza Rasmi September 10  mpaka 14 mwaka huu
ndani ya mkoa wa Arusha

Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa Arusha Bw Magesa Mulongo alisema kuwa
mkutano huo utaweza kuwakutanisha maelfu ya wananchi sanjari na
mawaziri wan chi hizo

Bw Magesa alisema kuwa kwa mkutano huo utaweza kuwaweka sehemu moja
wananchi pamnoja na mawaziri ambao wanahusika na mazingira kwa nchi
hizo huku lengo halisi likiwa ni kujadili mambo mbalimbali yahusiyo
mazingira

Alifafanua kuwa  mbali na hayo mwenyeji wa mkutano huo atakuwa ni
Raisi Jakaya kikwete ambapo mkutano huo pia utakuwa na faida kubwa
sana kwenye jamii hasa za mkoa wa Arusha

Aliongeza kuwa ni fursa ya wananchi wa mkoa wa Arusha kuhakikisha kuwa
wanajipanga ilivyo katika kuwapokeas wageni hao ambapo kabla ya kuanza
ka mkutano huo pia utatanguliwa na mkutano mwingine wa wadau wengine
wa mazingira ambao nao wataweza kujadili changamoto mbalimbali ambazo
zinaikabili sekta hiyo ya Mazingira hasa kwa nchi za Bara la Afrika.

MIMI NI MPIGA PICHA NA MWANDISHI WA HABARI WA KUJITEGEMEA NA KUPITIA BLOG HII NINA IMANI TUTAWEZA KUPEANA HABARI MBALIMBALI ZA BURUDANI ZITAKAZOFURAHISHA NA KUELIMISHA NAOMBA USHIRIKIANO WENU ILI TUWEZE KUFIKA TULIPOKUSUDIA

Got something to say? Go for it!