MKURUGENZI MTENDAJI MANDELA FUNITURE AFARIKI DUNIA


Aliyekuwa mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Mandela furniture ya mjini Iringa na Mbeya ,Felix Aron Mandela pichani amefariki dunia usiku wa kuamkia leo na mazishi yake yanataraji kufanyika leo saa 10 jioni katika makaburi ya Mtwivila mjini Iringa .

Mandela alikuwa amelazwa katika Hospitali teule ya wilaya ya Iringa Hospitali ya Ipamba .
Habari ziwafikie ndugu jama na marafiki popote pale alipo .

Tangazo hili limetolewa na mpiga picha Misanjo Livigha Mlalahoi Alwatan wa Highlands Hall Iringa.

Mandela atakumbukwa mkoani Iringa kwa jitihada mbali mbali alizozifanya katika kusaidia shule madawati ikiwemo shule ya sekondari Idodi iliyokumbwa na mkasa wa kuteketea kwa moto .

Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi
Amina

MIMI NI MPIGA PICHA NA MWANDISHI WA HABARI WA KUJITEGEMEA NA KUPITIA BLOG HII NINA IMANI TUTAWEZA KUPEANA HABARI MBALIMBALI ZA BURUDANI ZITAKAZOFURAHISHA NA KUELIMISHA NAOMBA USHIRIKIANO WENU ILI TUWEZE KUFIKA TULIPOKUSUDIA

Got something to say? Go for it!