Toto Africa ya Mwanza na JKT Oljoro zatoka sare CCM Kirumba Mwanza

Kikosi cha JKT  Oljoro kikiwa katika picha ya pamoja kwenye uwanja wa CCM Kirumba kabla ya mpambano wao na Toto African.

Timu ya Toto African ya Mwanzaikiwa katika picha ya pamoja kabla ya mpambano huo.

…………………………………………………

Timu ya Timu ya Toto African  ya  Mwanza leo  imetoka sare  ya goli moja kwa  moja na timu ya JKT Olojoro ya Arusha katika mechi ya ufunguzi wa pazia ya ligi kuu Tanzania Bara iliyochezwa leo katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.
Mechi hiyo iliyokuwa na ushindani mkali kutoka pande zote mbili, Toto walianza kwa kasi kwa kulisakama lango la JKT Olojoro na mnamo dakika ya tatu Toto African walipata penati ambapo mchezaji wake Emmanuel Swita alikosa baada ya kipa ya JKT Olojoro Shaibu Issa kuipangua penati hiyo.
Wachezaji wa timu zote walicheza mchezo wa kuonana katika kipindi cha kwanza na hadi mapumziko timu zote zilitoka bila bila na kwenda mapumziko.

Kipindi cha pili kilianza kwa Timu zote kushambuliana kwa hatamu na timu ya Toto African wakipoteza magoli ya wazi kabisa. Kipa wa Toto African alifanya kazi kubwa ya kuondoa michomo kibao kwenye lango la timu ya Toto African.

Dakika ya 88 timu ya Jkt Oljoro walipata goli la kwanza kupitia Hemedy Amri na kisha Toto Afrikan kusawazisha dakika 89 kupitia kwa Mohamed Notto. Na hadi mwisho wa mechi Toto afrikan moja na Jkt Olojoro moja. Matukio zaidi tembelea www.fpluss.blogspot.com

MIMI NI MPIGA PICHA NA MWANDISHI WA HABARI WA KUJITEGEMEA NA KUPITIA BLOG HII NINA IMANI TUTAWEZA KUPEANA HABARI MBALIMBALI ZA BURUDANI ZITAKAZOFURAHISHA NA KUELIMISHA NAOMBA USHIRIKIANO WENU ILI TUWEZE KUFIKA TULIPOKUSUDIA

Got something to say? Go for it!