WATUMISHI KUTOKA SIERRA LEONE NA MALAWI WAWASILI NCHINI TANZANIA KUJIFUNZA UFANISI WA TUME YA UTUMISHI WA UMMA

Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma Bi. Claudia Mpangala (kulia) akiwakaribisha ofisini kwake wageni kutoka Malawi na Sierra Leone ambao wako nchini Tanzania kujifunza masuala mbalimbali ya utendaji kazi yanayofanywa na Tume ya Utumishi wa Umma.

(PICHA NA ARON MSIGWA WA MAELEZO)

Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma Bi. Claudia Mpangala (upande wa kulia katikati) akiwa na baadhi ya watendaji wa Tume ya Utumishi wa Umma akisikiliza m aelezo kutoka kwa Bi.Geoigiana Kamara (kulia) kuhusu utendaji  kazi wa  Ofisi ya Rasilimali watu ya Sierra Leone.

Afisa Tawala Mkuu wa Tume ya Utumishi wa Umma  Bw. Chele Ndaki akitoa maelezo ya namna Tume  hiyo inavyotekeleza majukumu yake kwa wageni kutoka Malawi na Sierra Leone ambao wako nchini Tanzania kujifunza masuala mbalimbali ya utendaji kazi yanayofanywa na Tume ya Utumishi wa Umma.

MIMI NI MPIGA PICHA NA MWANDISHI WA HABARI WA KUJITEGEMEA NA KUPITIA BLOG HII NINA IMANI TUTAWEZA KUPEANA HABARI MBALIMBALI ZA BURUDANI ZITAKAZOFURAHISHA NA KUELIMISHA NAOMBA USHIRIKIANO WENU ILI TUWEZE KUFIKA TULIPOKUSUDIA

Got something to say? Go for it!