All posts in BURUDANI

HAYAWIHAYAWI, SASA YAMEKUWA! USIKU WA HIP HOP, THE VODACOM MIC KING KURINDIMA J’MOSI HII DAR LIVE

Wakali tisa wa Hip Hop wanaowania gari aina ya Toyota FunCargo (new model), katika pozi mbele ya gari lao.

Na Mwandishi Wetu

ILIPANGWA, ikapangika. Baada ya kusubiririwa kwa muda mrefu, hatimaye msimu mpya wa shoo ya Usiku wa Hip Hop (2013) unachukuwa nafasi Jumamosi hii ndani ya Ukumbi wa Dar live, Mbagala-Zakhem, jijini Dar.

Wasanii wanaotamba kwenye gemu la Hip Hop, Kala Jeremiah, Fid Q, Nay wa Mitego, Joh Makini, Stamina na wengine kibao pamoja na washiriki wa Shindano la The Vodacom Mic King watakamua shoo baab’kubwa kuweka historia mpya ya burudani.

Meneja Matukio wa Ukumbi wa Dar Live, Abdallah Mrisho ‘Abby Cool’ amewahakikishia mashabiki wote wa muziki wa Hip Hop kuwa Jumamosi kutasheheni matukio kibao, ulinzi mzito utakuwepo pamoja na parking kubwa ya magari hivyo watu wafike kwa wingi watainjoi kwa nafasi na kuondoka salama ukumbini.

“Vijana tisa waliosalia katika Shindano la The Vodacom Mic King watapanda jukwaani na kushusha mistari ambapo mshiriki mmoja anatarajiwa kuondoka na gari jipya aina ya Toyota FunCargo (new model),” alisema Abby Cool na kuongeza:

“Mashabiki wanaweza kulifuatilia shindano hilo kupitia Runinga ya DTV kuweza kujua jinsi ya kuwapigia kura.”

Washiriki hao na namba zao za ushiriki kwenye mabano ni Ally (MK 02), Anold (MK 03), Bahati (MK 05), Boniface (MK 07), Emmanuel (MK 10), Ibrahim (MK 12), Karrys (MK 13), Lusajo (MK 14) na Martin (MK15). Jinsi ya kuwapigia kura, wasomaji wanatakiwa kuandika neno MK wakiambatanisha na namba ya mshiriki kisha kutuma ujumbe huo kwenda namba 15564.

OFA ZAIDI KWA MSHINDI

Mbali na mshindi kuondoka na gari, Mrisho aliongeza kuwa washindi watatu wa nafasi za juu watajipatia dili la kurekodi singo mojamoja kutoka kwa prodyuza kiwango aliyezalisha ngoma kali Bongo ikiwemo ya Kundi la Kigoma All Stars iitwayo Leka Dutigite, Tudd Thomas.

TUZO KUTOLEWA

Mrisho alitiririka na mistari kuwa, mbali na shoo kali kutoka kwa wakali hao wa Hip Hop, kutakuwa na kipengele cha kutoa tuzo za muziki wa Hip Hop katika vipengele tofauti hivyo mashabiki pia waendelee kuwapigia kura wasanii wanaowapenda.

Vipengele vitakavyotolewa tuzo ni Mwanamuziki Bora wa Hip Hop (Legendary) ambapo yamepita majina matatu; Fid Q, Joh Makini na Profesa Jay. Pia kipengele cha Mwanamuziki Bora wa Hip Hop (Chipukizi) ambacho kina majina kama Young Killer, P The Mc na Tabla huku akianisha kipengele cha mwisho ambacho ni Wimbo Bora wa Hip Hop (2012/13) chenye nyimbo kali za Dear God (Kala Jeremiah), Sihitaji Marafiki (Fid Q) na Najuta Kubalehe (Stamina).

“Ili kuwapigia kura, mashabiki wanatakiwa kuandika neno BHL wakiambatanisha na jina la msanii husika kwenda namba 15564 katika kipengele cha Msanii Bora wa Hip Hop (Legendary).

“Kipengele cha Mwanamuziki Bora wa Hip Hop (Chipukizi), mashabiki waandike neno BUA na kufuatiwa na jina la msanii wanayempenda kwenda namba 15564,” alisema Abby Cool na kuongeza:

“Kipengele cha Wimbo Bora wa Mwaka, mashabiki waandike neno BHS likifuatiwa na jina la msanii wanayempenda kisha watume ujumbe huo kwenda namba 15564.”

KUWAENZI WASANII/SOKA KWENYE SKRINI KUBWA

Abby Cool aliweka bayana kuwa katika shoo hiyo kutakuwepo na documentary maalumu ya kuwakumbuka wasanii wa Hip Hop waliotangulia mbele za haki kupitia skrini kubwa bila kusahau mashabiki wa soka watapata fursa ya kushuhudia fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (Uefa) kati ya Bayern Munich na Borrusia Dortmund. Twendeni Dar Live J’mosi!

A POWERHOUSE OF AFRICAN ARTISTS TO PERFORM AT BIG BROTHER AFRICA’S LAUNCH SHOW!

images

On Sunday 26 May, the Big Brother launch show will come alive when multiple award winning musicians from Nigeria, Kenya and South Africa take centre stage. The big night will also see 28 new housemates being revealed to audiences in over 50 African countries for season 8 of Big Brother Africa, The Chase.

With the live show screening from 19:00 CAT on AfricaMagic, AfricaMagic Entertainment, AfricaMagic World as well as on DStv channel 197 and 198. Audiences can look forward to sassy and upbeat tunes from Kenya’s very own award winner, STL. Boasting hit songs such as “Take My Time” , “Hula Hoop“, “Bad as I Wanna Be“, the singer, songwriter and rapper, also recipient of awards from the Kisima Awards, Clops Awards and Jeermaan Awards, promises to deliver an unforgettable and lasting performance with her distinct pop, soul and rap sound.

Hailing from Nigeria, musical heavy weights Don Jazzy, D’ Prince and Wande Coal are also set to grab audiences with their energetic and charming personas. Multi award-winning record producer, singer-songwriter and musician Don Jazzy, will join stars in their own right, D’ Prince and Wande Coal on stage for their collaborative performance. These chart topping hit makers from Mavin Records are also best known for songs such as “I like What I See”, “Bumper 2 Bumper” and “Who Born the Maga”. The continent can expect a sensational performance that will ignite the Big Brother live show stage.

Last but not least, one of South Africa’s leading Afro Pop music groups, Mafikizolo will also serenade audiences with their soulful and rhythmic tunes on the big launch night. With several albums and awards under their belt, the duo has brought fans far and wide, dance-floor filler hits such as ”Sibongile”, “Ndihamba Nawe”, “Nisixoshelani” and most recently “Khona”. Their performance on the Big Brother stage is sure to evoke dance moves, reminding audiences why the chart topping group remains pioneers in their field with musical experience spanning over 15 years.

The line-up will also include a slot for some comic relief from Kenyan stand-up comedian Daniel Ndambuki, popularly known as Churchill. The highly talented entertainer has also become a household name with his TV show called “Churchill Live”.

In Addition to the live screening of the launch show, the good news is that the show will also concurrently be streamed live to audiences across Africa on the Big Brother website, www.bigbrotherafrica.com.                               All you need to access the live stream is a personal computer and internet connection.

With less than a week to go, be sure not to miss the jam packed, highly anticipated Brother Africa The Chase live launch show. Thereafter Africa’s biggest reality series will be screened live for 91 days, 24/7 on DStv channels 197 and 198 while GOtv audiences will be able to see highlights on AfricaMagic World.

UTAMBULISHO WA USIKU WA HIP HOP & FAINALI ZA VODACOM MIC KING KWA WANAHABARI

Meneja Matukio wa Dar Live, Abdallah Mrisho (wa pili kushoto) akiongea na wanahabari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho huo. Wengine pichani kutoka kushoto ni DJ John Dilinga (JD), Prodyuza Ally Baucha na Prodyuza Tudd Thomas.

Kutoka kushoto waliokaa ni msanii Stamina, DJ John Dilinga, Abdallah Mrisho, Ally Baucha na Tudd Thomas katika picha ya pamoja na washiriki wa The Vodacom Mic King waliosimama nyuma.

Wakali wa MIC wanaowania gari wakiwa katika pozi na gari hilo.

Wanahabari wakichukua baadhi ya matukio.

…Wakimsikiliza Abdallah Mrisho.

Hawa ndiyo wakali tisa wanaowania gari aina ya Toyota Funcargo (New Model).

Uongozi wa Dar Live Co. Ltd leo umetambulisha tamasha kubwa la kila mwaka la Usiku wa Hip Hop na fainali za kumtafuta Mkali wa Mic zijulikano kama ‘The Vodacom Mic King’ kwa wanahabari. Tamasha hili litafanyika Jumamosi hii, Mei 25, 2013 katika Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar. Jumla ya vijana tisa wenye vipaji watapanda stejini kuchuana na mshindi ataondoka na gari aina ya Toyota Funcargo (New Model) yenye thamani ya shilingi milioni 15. Mbali na zawadi ya gari, mshindi wa kwanza, pili na watatu, watapata fursa ya kurekodi wimbo mmoja chini ya Prodyuza mahiri nchini, Tudd Thomas, aliyerekodi wimbo maarufu wa Leka Dutigite wa Kigoma All Stars na nyingine nyingi. Majaji katika shindano hili ni mwandishi mkongwe wa habari za muziki na wasanii, Abdallah Mrisho, DJ John Dilinga (JD) na Prodyuza Ally Baucha.

Tamasha hilo litapambwa na burudani kutoka kwa wakali wa Hip Hop nchini ambao ni Fid Q, Joh Makini, Stamina, Kala Jeremiah, Nay wa Mitego pamoja na shoo kali kutoka kundi la Wakali Dancers. Katika usiku huo, zitatolewa tuzo kwa wasanii wa Hip Hop na kwa wimbo bora wa Hip Hop uliofanya vizuri mwaka 2012/13. Kutakuwa na Tuzo kwa Msanii Mkongwe Bora wa Hip Hop na Msanii Chipukizi Bora wa Hip Hop pamoja na Wimbo Bora wa Hip Hop.

(PICHA NA MUSA MATEJA / GPL)

KINACHOMPONZA PRODYUZA TUDD THOMAS NI UCHAWI AU KUSAHAU?

Prodyuza Tudd Thomas.

MASHABIKI wa mtayarishaji wa muziki (Producer), mwenye uwezo wa kipekee, aliyetayarisha wimbo wa Leka dutigite wa Kigoma All Stars na zingine nyingi, Tudd Thomas, wamekuwa wakiulizana maswali mengi wao kwa wao pasipo kupata majibu.

Safari ya Tudd Thomas katika muziki, ilianzia mkoani Iringa akiwa Iringa Records aliporekodi wimbo wa mwanamuziki Marlaw unaoitwa Bembeleza. Wimbo huo ulipata tuzo ya wimbo bora wa mwaka kutoka Kilimanjaro Tanzania Music Awards mwaka 2008 na pia kumfanya Marlaw apate tuzo ya msanii bora wa kiume kupitia tuzo hizo. Baadae alihamia jijini Dar es Salaam na ndipo alipoonesha uwezo wake zaidi kwa kusuka nyimbo zilizotikisa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla.

Hakuna asiyeufahamu wimbo wa Pii Pii (Missing my baby) wa Marlaw ambao aliutengeneza yeye kupitia Studio ya JML. Wimbo huo ulipata tuzo nyingi ikiwa ni pamoja na tuzo ya Nzumari nchini Kenya mwaka 2009 mbapo uliingia kwenye kipengere cha wimbo bora wa Afrika Mashariki, kumfanya Marlaw aingie kwenye kipengele cha msanii bora wa Afrika Mashariki na kunyakua tuzo hiyo. Baada ya hapo wimbo huo ulipata tuzo ya Kilimanjaro nchini Tanzania kama wimbo bora wa mwaka wa Afro pop mwaka 2010, tuzo ya Chaguo la Teneez Music nchini Kenya kama wimbo ulioongoza kwa kuchukuliwa kwa njia ya mtandao Afrika Mashariki “The most downloaded East African song” mwaka 2010, pamoja na tuzo ya Nigeria Sound City Video Music kama wimbo bora wa Afrika Mashariki mwaka 2010.

Aliendelea kutayarisha nyimbo ambazo zilipata umaarufu mkubwa na kuingia kwenye vipengele mbalimbali vya tuzo za muziki za Kilimanjaro. Mwaka 2012, nyimbo tatu zilizotokana na mikono yake zilipata nafasi ya kushiriki tuzo hizo. Nyimbo hizo ni Liz One wa Izzo Business ambao uliingia kwenye vipengele viwili ambavyo ni wimbo bora wa mwaka na wimbo bora wa Hip hop na pia kusababisha msanii huyo aingie kwenye kipengele cha msanii bora wa Hip hop. Milele daima wa Barnaba na Kizunguzungu wa Rachel, ambapo zote ziliingia kipengele cha wimbo bora wa Zouk/Rhumba pia ni nyimbo alizotengeneza mtayarishaji huyo.

Nyimbo zingine alizotayarisha ambazo zilifanya vizuri kwenye vituo mbalimbali vya redio na TV ni Kisa pombe na Soldier za Mwasiti, Sorry sana, Mbayuwayu na Mtoto wa Afrika za Marlaw pamoja na Natumaini ya Becka aliyowashirikisha Barnaba na Amin. Pia zipo nyingine kama Unikimbie ya Amin, Tushukuru kwa yote ya Ditto, Lonely ya Linah na Magubegube ya Barnaba.

Mtayarishaji huyo ambaye hajawahi kuingia kwenye tuzo za Kilimanjaro za muziki wa hapa nchini Tanzania ambazo mwaka huu zimeongezewa kipengele cha Mtayarishaji bora chipukizi ndiye aliyetayarisha wimbo wa Leka dutigite wa Kigoma All Stars kupitia Studio yake ya Ngoma Records. Wimbo huu umeingia kwenye kipengele cha wimbo bora wa mwaka 2013. Pia alishirikiana na mtayarishaji Imma the boy kutengeneza wimbo wa Me ‘n’ U wa Ommy Dimpoz ambao umeingia kwenye kipengele hicho na vipengele vingine ambavyo ni wimbo bora wa Bongo Pop na wimbo bora wa kushirikiana.

Alipoulizwa alisema hapendi kuzungumzia juu ya kutotajwa kama miongoni mwa wanaowania tuzo. Aliendelea kusema kwamba, hata kama baadae ikitokea, kwake ni motisha tu, lakini kikubwa zaidi ni kwamba anahisi analo deni kubwa la kutumia uwezo wake ipasavyo kufanya kazi nzuri zaidi ya hapo ili kuutangaza muziki wa Tanzania kimataifa. Pia alisema ana malengo makubwa aliyojiwekea na ndiyo maana kila kukicha anawaza kutayarisha nyimbo zenye tofauti na zenye radha ya kipekee.

Tudd Thomas anaendelea kukitumia kipaji chake na ujuzi wake ipasavyo na siku chache zilizopita kuna nyimbo zisizopungua tatu zilizoingia sokoni na zinafanya vizuri, ambazo ni kazi za mikono yake. Nyimbo hizo ni Uswazi take away ya Chegge, Nyumbani ya Kigoma All Stars na pia ameshirikiana kwa kiasi kikubwa na mtayarishaji Fundi Samwel kutengeneza wimbo wa Mahakama ya mapenzi wa Linex.

DIAMOND, NEY WA MITEGO WAFANYA KUFURU DAR LIVE

Diamond Platnumz akiwapa hi mashabiki.

DAR Live usiku wa kuamkia leo ilitikisika baada ya mashabiki kujitokeza kwa wingi kushuhudia onyesho la pamoja kati ya wanamuziki wawili nyota wa kizazi kipya, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Ney wa Mitego ambao walikuwa wakizindua video ya wimbo wao wa ‘Muziki Gani’.

Wanamuziki hao kwa pamoja walitoa burudani ya nguvu ambayo ilizikonga nyoyo za mashabiki waliofurika katika ukumbi huo wa maraha uliopo Mbagala Zakhem, jijini Dar.

(PICHA ZOTE NA ISSA MNALLY/GPL)

Ney wa Mitego akiwarusha wapenzi wa burudani.

Nyomi iliyoitikia shoo hiyo.

Diamond na Ney wakiwapagawisha mashabiki.

Ney wa Mitego akisema na wapenzi wake.

Diamond Platnumz akionyesha umahiri wake stejini.

Diamond akifanya makamuzi sambamba na kundi lake.

Ney wa Mitego akilishambulia jukwaa la Dar Live.

Mashabiki wakiburudika wakati wa shoo hiyo ndani ya Dar Live.

Diamond na kundi lake katika pozi kabla ya makamuzi.

MASTAA CHIPUKIZI KUJIMWAGA KATIKA TAMASHA LA SHIWATA MEI 26!!

pic-6

          TAMASHA la Mastaa chipukizi la mwezi Mei litafanyika tarehe 26, mwezi huu katika ukumbi wa Starlight Hotel kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 10 jioni.

 Vikundi vya sanaa vya Kaole, Splendid, Super Shine Taarab, Five Star Modern Taarab pamoja na wasanii mbalimbali wa Bongo Flava, Maigizo, Ngoma, Dansi na Sarakasi wamethibitisha kushiriki tamasha hilo.

 Wasanii wakongwe wa bongo flava kama Stara Thomas, Bendi ya Msondo Ngoma na waigizaji wakongwe wa Kaole na Splendid wataonesha umahiri wao katika fani ya sanaa.

 Kauli Mbiu ni Kilio cha Msanii ambako mpaka sasa vikundi 30 kutoka jiji la Dar es Salaam vitashiriki katika tamasha hilo.

 SHIWATA pia inawapongeza wote walioshiriki tamasha  la Aprili 27 ambako zaidi ya wasanii 300 walishiriki kuonesha vipaji vyao ambako mgeni rasmi alikuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM kutoka Wilaya ya Kinondoni, Calist Lyimo ambaye alitumia nafasi hiyo kuwaasa wasanii kujituma kuonesha uwezo wao katika kuelimisha jamii.

 Pia Shiwata imeupongeza uongozi wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) kwa ushirikiano wao mzuri na kuwaomba viongozi wengine wa bendi za muziki, taarab,vikundi vya sanaa,mapromota,maprodusa na wadau wote kutoa ushirikiano katika matamasha haya ili kujenga ushirikiano wa pamoja.

 Maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika ambako wasanii kutoka vikundi mbalimbali wamepiga kambi ya kujifua ili kuonesha ubunifu wao katika tamasha hilo.

 Wakati huo huo SHIWATA inatarajia kuhamisha tamasha hilo kwa mwezi Juni kufanyikia mkoa wa Arusha ili kuwapa nafasi wasanii wa mkoa huo nao kuonesha uwezo wao.

Wasanii 100 ambao wamefanya vizuri katika matamasha mawili yaliyokwisha fanyika Dar es Salaam watapatiwa nafasi katika tamasha la Arusha ambalo linafanyika 29/6/2013

BIG BROTHER AFRICA SEASON 8 BRINGS VIEWERS……….THE CHASE!

The Chase logoThe biggest reality show in Africa is back and AfricaMagic can reveal that season 8 of Big Brother Africa has been dramatically titled The Chase. 28 housemates from 14 countries will not only be chasing after the 300 000 USD cash prize but the chance of becoming a household name and perhapseven finding romance.

Launching on Sunday 26 May, Big Brother The Chase will combine electrifying twists and big surprises that will require housemates to use their charm to get ahead, possibly leaving room for cupid’s arrow to connect two hearts or more.

Setting the tone, in line with theme, the new seasons logo showcases a glittering and slightly flirtatious feel with chic, edgy gold plated lines. The iconic Big Brother eye has an enchanting gold dust finish with a dazzling diamond centre, featuring a teasing hint of ruby red.

More good news is that the witty and entertaining IK Osakioduwa returns once again in 2013 to host The Chase. He has won many fans across the continent for his ability to speak openly with housemates and allow them to be at ease at their most vulnerable moments.

“Big Brother Africa is a pretty unique show. Every season has its own special moments and features. I’m super excited to be invited back to host the show. I have thoroughly enjoyed the past seasons and I look forward to bringing a fresh and energetic approach to The Chase,” says the popular TV and radio presenter.

Commenting on the new season M-Net Africa Managing Director Biola Alabi says, “Without revealing too much, I can say that AfricaMagic always strives to deliver the best in entertainment and Big Brother Africa remains at the forefront of our plans. We want to give audiences and loyal fans of the show, a truly unforgettable viewing experience once again. This season audiences can expect a show encompassing suspense, emotions, drama, fun, excitement and quite possibly, as we have seen in previous seasons, a little romance.

Having produced Big Brother Africa from season one, Endemol promises a sterling edition of The Chase, “Endemol is excited to present another season of Big Brother in Africa. Another vintage season lies in store with fresh new twists and surprises and ultimately great reality entertainment” adds Managing Director of Endemol South Africa Sivan Pillay.

With less than four weeks remaining to the big launch night, audiences can get the latest Big Brother Africa updates on www.bigbrotherafrica.com as well as on Facebook and Twitter.

For 91 days, Africa biggest reality series will be screened live 24/7 on DStv channels 197 and 198 while GOtv audiences will be able to see highlights. So stay tune…Biggie has returned and the fun is about to begin!

Msondo,Che Mundugwao,Majuto kuwasha moto Fainali za Taifa Miss Utalii Tanzania Mkwakwani Tanga tarehe 19.05.2013.

DSCN7178Warembo wa Miss Utalii Tanzania 2013 wakiwa katika Picha ya Pamoja

………………………………………..
Baada ya shamlashamla na mapokezi makubwa ya Miss Utalii Tanzania walipo ingia Mkoani Tanga na kupokelewa na umati mkubwa wa watu, warembo hao wapo kambini tayari kwa maandalizi ya Fainali hizo.

 Fainali za Taifa Miss Utalii Tanzania zitafanyika Tarehe 19.05.2013 Mkoani Tanga ambapo warembo zaidi ya 30 watapanda Jukwaani kuwania Taji la Taifa la Miss Utalii Tanzania 2013 ndani ya Mkwakwani.

 Sambamba na Fainali hizo za Miss Utalii , kutakuwa na Burudani ya Kukata na shoka ambayo itasindikizwa na Bendi kongwe ya Muziki Msondo Ngoma kutoka Dar es salaam, Mwanamuziki wa Kimataifa Che Mundugwao, Majuto Arts Group, Mdumange, vikundi vya ngoma na Sarakasi.

 Fainali za Taifa zitaanza kuanzia saa 7 mchana hadi saa 12 jioni Ambapo viingilio kwa watoto itakuwa 2,000 na wakubwa 5,000 Baada ya hapo kuanzia saa 1 usiku hadi Majogoo viti Maalum itakuwa ni 20,000 na kawaida itakuwa 10,000

Mpaka sasa Kambi ya Miss Utalii Tanzania 2013 ipo jijini Tanga Mwambani Hotel na inaendelea Vizuri, Warembo zaidi ya 30 kutoka mikoa yote nchini ,wanajiandaa vizuri  kwa ajili ya Fainali Hizo zitakazo fanyika wiki ijayo Tanga, Kanda Maalum ya Zanzibar na Vyuo vikuu Tanzania.

Washindi wa 1-5 wa Fainali za Taifa ,watawakilisha Tanzania katika mashindano mbalimbali ya Dunia na nchi yatakako fanyika katika mabano  International Miss Tourism World (Marekani), Miss Tourism United Nation (Mexico), Miss Heritage World (Tunasubiri Taarifa), Miss Tourism University World(Tanzania), Miss Globe International (Uturuki), Miss Tourism World ( Equatorial Guinea ), Miss Freedom Of The World ( Kosovo) , na Miss Tourism United Nation (Nigeria)  n.k

 Wakati huohuo, katika kuhakikisha kuwa maandalizi ya Fainali za taifa, za mashindano hayo ambapo mkoa wa Tanga unakuwa wenyeji kwa mara ya kwanza yanafanyika kwa ubora na hayakwami, kamati ya maandalizi ya kimkoa umeundwa ambayo mwenyekiti wake ni Peter Semfuko Afisa Utamaduni wa Jiji la Tanga. Miss Utalii Tanzania ,hadi sasa tunashikilia Jumla ya mataji 5 ya Dunia na kimataifa, yakiwemo ya Miss Tourism World 2005-Africa,Miss Tourism World 2006-SADC,Miss Tourism World 2007-Africa, Miss Tourism
Model Of The World 2008-Personality, Miss Africa 2006 – 1ST Runner Up

WATAALAM WA KUKABILIANA NA MAJANGA KUTOKA TANZANIA NA MAREKANI WAKUTANA JIJINI DAR ES SAALAAM.

Picha na 1Viongozi wa serikali ya Tanzania na Marekani, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Shamsi Vuai Nahodha (kushoto) na Balozi wa Marekani nchini Tanzania Alfonso Lenhardt (kulia) wakionyesha nyaraka mbili za Mpango wa kukabiliana na maradhi ya mafua ya ndege. Nyaraka hizo zinahusisha vikosi vya jeshi na raia nchini Tanzania na Kamandi ya Jeshi la Marekani la Kupambana na Majanga Barani Afrika (USAFRICOM). Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.  Picha na 2Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Shamsi Vuai Nahodha akizungumza na viongozi mbalimbali wa vitengo vya kukabiliana na majanga kutoka Tanzania na Marekani leo jijini Dar es salaam.Pamoja na mambo mengine amesema Tanzania inaendelea kujenga uwezo wa ndani wa kukabiliana na majanga mbalimbali. Picha na 3Balozi wa Marekani nchini Tanzania Alfonso Lenhardt akiongea na viongozi mbalimbali wa vitengo vya kukabiliana na majanga kutoka Tanzania na Marekani leo jijini Dar es salaam na kusisitiza kuwa serikali ya Marekani itaendelea kushirikiana na Tanzania na nchi nyingine katika kukabiliana na majanga yanayotokea. 

Picha na 4Washiriki wa vikosi vya kupambana na majanga kutoka Tanzania na Marekani wakiangalia moja ya filamu inayoonyesha athari za virusi vya mafua ya ndege kwa binadamu iliyowahi kutokea katika moja ya nchi na hatua zilizochukuliwa kudhibiti hali hiyo isilete maafa zaidi.

Picha na 5Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wa siku mbili kutoka Tanzania wakifuatilia masuala mbalimbali yaliyokuwa yakijadiliwa leo jijini Dar es salaam. Picha na 6Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Shamsi Vuai Nahodha akitoa ufafanuzi kwa waandishi kuhusu utayari wa Tanzania katika kukabiliana na majanga mbalimbali yanayotokea kwa kuvishirikisha vikosi vya ulinzi na usalama, wataalam wa sekta nyingine, utoaji wa tahadhari mapema kwa wananchi na uimarishaji wa kitengo cha maafa nchini.

Picha na 7Washiriki wa mkutano wa siku 2 unaojadili namna ya kukabiliana na majanga mbalimbali na athari za Virusi vya mafua ya ndege wakiwa katika picha ya pamoja leo jijini Dar es salaam.

Tamasha la Mtemi Milambo lazinduliwaTabora

Milambo 1Naibu Mayor Mhe Waziri Mlenda katika uzinduzi rasmi wa Tamasha hilo pembeni ni Mkurugenzi Mtendaji wa Chief Promotions Bw.Amon Mkoga.

………………………………………….

Tamasha la Utamaduni la kila mwaka Mtemi Milambo Festival  limezinduliwa leo 13/5/2013 uwanja wa Taasisi  mkoani Tabora.

Ambapo Mgeni Rasmi Naibu Mayor Mhe Waziri Mlenda katoa wito kwa wananchi kuuenzi utamaduni wao kwani msahau kwao ni mtumwa.

“Ngoma hizi za Wasukuma na Wanyamwezi huchezwa sana wakati wa mavuno,wananchi  husheherekea  pamoja wakati wa mavuno huku wakiukienzi utamaduni wa Kitanzania.

Kauli mbiu ya Tamasha hili mwaka huu ni KUSHOKE KUKAYA yaani turudi nyumbani tafsiri ya Kiswahili toka kinyamwezi.

DIAMOND MUSICA WALIPAMBA SHINDANO LA THE MIC KING!!

Washiriki wote tisa wakiwapungia mikono mashabiki wao.

Majaji wakitoa ushauri kwa washiriki.

Kiongozi wa Bendi ya Diamond Musica, Liva Hassan ‘Sultan’ (kushoto), akiimba sambamba na waimbaji wake.…Akizikonga nyoyo za mashabiki wa Dar Live.Wacheza shoo wakionyesha machejo yao.Mpiga drums akionyesha ufundi wake.

SHINDANO la The Mic King jana liliendelea kushika kasi katika ukumbi wa kisasa wa Dar Live ambapo bendi ya Diamond Musica ilitoa burudani kulipamba shindano hilo. Wakali wa Mic walichana mistari mbalimbali wakielekea mwishoni mwa mchuano huo utakaomalizika Mei 25, mwaka huu katika ukumbi huo.

(PICHA NA ISSA MNALLY / GPL)

UZINDUZI wa mauzo ya albamu ya bendi ya muziki ya Mashujaa

imagesNa Mwandishi Wetu

………………………………….
UZINDUZI wa mauzo ya albamu ya bendi ya muziki wa dansi ya Mashujaa ‘Wanakibega’ uliofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki umefana.

 Bendi hiyo ilifanya uzinduzi wa mauzo ya albamu yake mpya ya Risasi Kidole ambapo onesho lake
lilijaza mashabiki wengi waliofika  kufurahia burudani iliyotolewa na wanamuziki wa bendi hiyo wakisindikizwa na FM Academia.

Onesho hilo lilifanyika kwenye ukumbi wa Business Park uliopo Kijitonyama, Dar es Salaam.

Burudani hiyo ya mseto kati ya Mashujaa na Fm Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’  ilikonga nyoyo za mashabiki waliofurika ndani ya ukumbi huo.

Katika uzinduzi huo lilifanyika yukio ambalo halikutarajiwa  wakati Rais wa Wanakibega, Charlz Baba alipomvisha pete mchumba wake ambaye anatarajia kufunga naye ndoa miezi mitatu ijayo.

 Charlz aliwaambia  mashabiki kuwa kitendo anachofanya ni kutekeleza wosia marehemu mama yake kumtaka aoe.

Alisema kuwa mama yake alimuusia kama anataka kuwa na maisha mazuri ni lazima awe na familia yake kwa kufunga ndoa.
 ”Marehemu mama yangu alikuwa akinisihi kila mara nioe, nami nimeona ni vyema kufuata ushauri wake naona huyo ndiye mke mwema kwangu, ni mama yangu na baba yangu kwa kuanzia sasa,”alisema Charlz Baba.

Kwa upande wa Rais wa FM Academia Nyoshi El Saadat, alisema wapenzi wa muziki wa dansi watambue kuwa sasa ni mapinduzi rasmi ya muziki huo.

Alisema waliunganaa kufanya onesho hilo bila ya kinyongo chochote na hata bendi nyingine ikitaka kudanya hivyo iwaite, wao hawana matatizo wanachotaka wote wawe kitu kimoja.

“Naomba kila mpenzi atambue kuwa haya ni mapinduzi katika muziki wa dansi basi hata wengine nao waje tushirikiane nao sisi hatuna matatizo na mtu,” alisema Nyoshi.

Waziri mkuu Mizengo Pinda apokea matembezi ya mshikamano ya kupapambana na wizi wa kazi za sanaa mjini Dodoma

Waziri Mkuu Pinda akiwa katika picha ya pamoja na na baadhi ya Watangazaji wa Clouds FM (wote waliosimama nyuma).Reedio Clouds FM imezindua msimu wake mpya ulioitwa TWENZETU  kwa minajili ya kuielimisha jamii  kuwa na tabia ya kupenda vya kwao na  kutumia fursa walizonazo ndani ya MADE IN TANZANIA kujikwamua kimaisha.
Waziri Mkuu Pinda akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wasaniii (wote waliosimama nyuma),mara baada ya kuzungumza nao kuhusiana na mambo mbalimbali juu ya sanaa ya Tanzania na namna ya kupambana na maharamia wa kazi zao,ambapo pia redio ya Clouds FM imezindua msimu wake mpya ulioitwa Twenzetu kwa minajili ya kueilmisha jamii ya kupenda vya kwao kutumia fursa walizonazo ndani ya MADE IN TANZANIA . 
Waziri Mkuu Pinda akizungumza mbele ya  baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya/Filamu pamoja na watangazaji wa Clouds FM na wadau wengine wa sanaa waliojumuika kwa pamoja kwenye tukio hilo adhimu kabisa mapema leo mchana,mara baada kufanyika Matembezi ya mshikamano ya kuitaka Serikali iendelee kuzilinda fursa zilizopo na pia kuendelea kuutanua wigo wa upatikanaji wa fursa hizo kwa wasanii na vijana wenyewe,ikiwa sambamba na kupinga uwizi/uharamia wa kazi za sanaa hapa nchini.
Mh.Pinda aliishukuru kampuni ya Clouds Media Group kwa kazi nzuri walioianzisha ya kuwasaidia vijana kwa namna moja ama nyingine katika suala zima la kuwaamsha na kuwafungua macho na kuwaelimisha namna ya kuziona fursa zilizopo kwa ajili ya kujikwamua kimaisha,aliongeza  kuwa kupitia ujumbe huo wa MADE IN TANZANIA kinachohitajika sasa ni kupanga ratiba nzuri ya kuliendeleza zoezi hilo ikiwemo pia kwa kuzishirikisha taasisi nyingine zikiwemo za serikali katika kuhakikisha jambo hilo linaendelea.
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Dkt.Rehema Nchimbi akiwakaribisha watu wote waliofika kwenye viwanja vya Nyerere Skwea,tayari kwa kumpokea mgeni rasmi,Waziri Mkuu Pinda.
Baadhi Wadau wa Muziki na Filamu wakiwa na mabango yao yaliyobeba jumbe mbalimbali mapema leo kwenye Matembezi ya mshikamano ya kuitaka Serikali iendelee kuzilinda fursa zilizopo na pia kuendelea kuutanua wigo wa upatikanaji wa fursa hizo kwa wasanii na vijana wenyewe,ikiwa sambamba na kupinga uwizi/uharamia wa kazi za sanaa hapa nchini,yaliyoanzia kwenye uwanja wa Jamhuri na kufikia tamati viwanja vya Nyerere Skwea 
Sehemu ya umati wa watu ukiwa kwenye Matembezi ya mshikamano ya kuitaka Serikali iendelee kuzilinda fursa zilizopo na pia kuendelea kuutanua wigo wa upatikanaji wa fursa hizo kwa wasanii na vijana wenyewe katika nafasi ya kujikwamua kimaisha,ikiwa sambamba na kupinga uwizi/uharamia wa kazi za sanaa hapa nchini,yaliyoanzia kwenye uwanja wa Jamhuri na kufikia tamati viwanja vya Nyerere Skwea 
 Baadhi ya Wasanii wa Filamu hapa nchini Wema Sepetu sambamba na shosti yake Kajala walikuwa ni miongoni mwa wasaani waliounga mkono matembezi hayo ya mshikamano yaliyokuwa yametawaliwa pia na mabango kadhaa yaliyobeba jumbe mbalimbali za kupinga wizi wa kazi sanaa.
 Matembezi ya mshikamano ya kuitaka Serikali iendelee kuzilinda fursa zilizopo,ikiwa sambamba na kupinga uwizi/uharamia wa kazi za sanaa hapa nchini . 
 Baadhi ya magari yakiwa yamesimama yakipisha matembezi ya mshikamano yaliyokuwa yakielekea kwenye viwanja vya Nyerere Skwea mapema leo mchana.
 Baadhi ya Watangazaji wa clouds FM,sambamba na wasanii wa muziki wa kizazi kipya/tasnia ya filamu na wadau wengine wa sanaa wakiwa wamejumuika kwa pamoja kwenye viwanja vya Nyerere Skwea mapema leo mchana,tayari kwa kumpokea mgeni rasmi,Mh Waziri Mkuu Pinda.
Mmoja wa Watangazaji wa kipindi cha Jahazi,Wasi Wasi Mwambulambo akiserebuka na Mh.Rehema Nchimbi.
 Baada ya muda kulipita burudani ya pamoja ya mchanganyiko kama hivi safi kabisa kabla ya Waziri Mkuu kuwasili viwanjani hapo.
 Pichani kati ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt.Rehema Nchimbi,kulia mtangazaji wa Clouds FM Mbwiga Mbwiguke na Shaffih Dauda (shoto) wakitwibiwirika kwa pamoja mapema leo mchana mjini Dodoma kwenye viwanja vya Nyerere skwea.
 Mbunge wa Jimbo la Kinondoni na Mdau mkubwa wa sanaa hapa nchini,Mh.Idd Azan akiunga mkono harakati za kupapambana na maharamia wa kazi za sanaa hapa nchini
 Gari ya Waziri Mkuu Pinda ikiwasili
 Waziri Mkuu Pinda akisalimiana na Naibu Waziri wa Habari,Vijana, michezo na Utamaduni,Mh.Amos Makala habari,Michezo mara alipokuwa akiwasili kwenye viwanja vya Nyerere Skwea mapema leo mchana mjini Dodoma. 
 Waziri Mkuu Pinda akisalimiana na Mkurugenzi wa Vipindi na utafiti wa Clouds Media Group,Ruge Mutahaba mara alipokuwa akiwasili kwenye viwanja vya Nyerere Skwea mapema leo mchana mjini Dodoma.
 Waziri Mkuu Pinda akiwasili kwenye viwanja vya Nyerere Skwea,mjini Dodoma mapema leo mchana huku akiwapungia mkono baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya/Filamu pamoja na watangazaji wa Clouds FM na wananchi wengine kwa ujumla waliojumuika kwa pamoja kwenye tukio hilo adhimu kabisa mapema leo mchana,mara baada kufanyika Matembezi ya mshikamano ya kuitaka Serikali iendelee kuzilinda fursa zilizopo na pia kuendelea kuutanua wigo wa upatikanaji wa fursa hizo kwa wasanii na vijana wenyewe,ikiwa sambamba na kupinga uwizi/uharamia wa kazi za sanaa hapa nchini,pichani kati ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Dkt.Rehema Nchimbi akimkaribisha. .
 Mh.Waziri Mkuu Pinda akizungumza jambo na Muimbaji mahiri wa mashairi hapa nchini,Mrisho Mpoto.Kulia ni Mkurugenzi wa Vipindi na utafiti wa Clouds Media Group,Ruge Mutahaba na kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Chamwino,Mh.Fatma Ally akishuhudia mazungumzo hayo.

TAMASHA LA UZINDUZI WA KAMPENI YA TWENDE ZETU NI BALAA UWANJA WA JAMHURI DODOMA

J3Msanii wa muziki wa kizazi kipya anayejulikana kwa jina la Shilole akicheza na mmoja wa mashabiki wake jukwaani katika tamasha la  uzinduzi wa kampeni ya Twende Zetu linalofanyika jioni hii kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma likiwa limehudhuriwa na mashabiki lukuki wa muziki, Huu ni mwendelezo wa kampeni hiyo ambapo asubuhi ilifanyika semna kwa wasanii juu ya kujitambua na kutumia fursa walizonazo katika maisha yao badala ya kuwa walalamikaji tu.

J1Richa Mavoko akifanya vitu vykae jukwaani katika tamasha hilo. J2Richa Mavoko na kundi lake wakikamua jukwaani J4Mashabiki lukuki wakiwa wamejitokeza katika tamasha hilo J5Mwanamuziki Ben Paul akiimba katika tamasha hiloIMG_4498Msanii wa muziki wa kizazi kipya anayejulikana kwa jina la Timbulo akiimba jukwaani katika tamasha la Twende Zetu kwenye uwanja wa Jamhuri  mjini Dodoma  IMG_4545Dogo Asley kutoka kundi la TMK Mkubwa Fella na Wanawe akiimba jukwaani katika tamasha hilo.IMG_4546Dogo Asley kutoka kundi la TMK Mkubwa Fella na Wanawe akiimba jukwaani katika tamasha hilo pamoja na Dogo Muu kutoka kundi hilo pia

CLOUDS MEDIA YAANZISHA KAMPENI YA “TWENDE ZETU” KWA SEMINA NZITO NA WASANII MJINI DODOMA

1Mbunge wa Kigoma Kaskazini CHADEMA Ndugu Zitto Kabwe akizungumza na wasanii mabalimbali wakati akitoa mada katika semina ya kampeni maalum ya “Twede Zetu” iliyofanyika kwenye  ukumbi wa African Dream mjini Dodoma leo , Kampeni hiyo inazungumzia na kuhamasisha vijana kuwa wabunifu na kutumia fursa zilizopo ili kujikwamua kimaisha lakini pia kuleta maendeleo kwa wasanii wenyewe na taifa kwa ujumla Watu mbalimbali wametoa mada katika semina hiyo ambao ni Patrick Ngowi, Zeno Ngowi Msanii Mrisho Mpoto na Ndugu Zitto Kabwe mwenyewe. 2Watoa Mada katika semina hiyo Patrick Ngowi kushoto na Zeno Ngowi wakiteta jambo wakati wa semina hiyo. 3Mtoa mada Patrick Ngowi akizungumza na wasanii katika semina hiyo 4Msanii Mrisho Mpoto ambaye pia ametoa mada katika semina hiyo

4Mtoa mada Zeno Ngowi akizungumza na wasanii katika semina hiyo. 6Ndugu Zitto Kabwe akiingia katika ukumbi wa mikutano wa African Dream mjini Dodoma. 7Mtoa mada Patrick Ngowi akiingia kwenye ukumbi wa mkutano 8Mkurugenzi wa Maendeleo na Utafiti Clouds FM Bw. Ruge Mutahaba akizungumza katika semina hiyo .  9Mkubwa Fella kutoka TMK akizungumza katika semina hiyo 10DJ Elly katikati Godzilla kushoto na Izo Busness wakiwa katika semina hiyo. 11Benny Kinyaiya akizungumza katika semina hiyo kulia ni Babu Tale na kushoto ni Said Bonge. 12Millad Ayo akizungumza na kutoa mchango wake wa mawazo katika semina hiyo. 13Anold Kayanda akitoa mawazo yake. 14Ibrahim Masoud na washiriki wengine wakiwa katika semina hiyo 15Wasiwasi Mwabulamboakitoa mada katika semina hiyo. 16Dj Fetty akitoa mchango wake 17Afande Selle akiwa na wasanii wenzake katika semina hiyo. 18Khamis Mandi B. 12 akitoa mchango wake katika semina hiyo. 19Moungozaji wa semina hiyo Gerald Hando akizungumza na wasanii mbalimbali katika semina hiyo. 20Shafii Dauda na Diva wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa katika semina hiyo

KARIBU UBURUDIKE NA MALEGENDARY WENZAKO NDANI YA JOLLY’S CLUB KILA J’MOSI NA DJ JD!!

Unakumbuka? raha za ki-Legendary za muziki wa Silent Inn, Bills, FM Club, Carlifonia Dreamers, Mambo Club na Tazara? Basi DJ John Dillinga (DJ JD) na DJ Fast Eddy tunawakaribisha kujumuika na malegends wenzenu kila Jumamosi kuenzi nyakati hizo Isumba Lounge, Jolly Club kwa mchango wa elfu 10 tu mlangoni, Karibuni Sana.

WAZEE WA KIBEGA KUZINDUA MAUZO YA ALBAMU YAO BUSINESS PARK!!

1

Na Mwandishi Wetu
BENDI ya muziki wa Dansi ya Mashujaa Wazee wa Kibega leo inafanya uzinduzi wa mauzo ya Albamu yake ya Risasi Kidole, utakaofanyika kwenye Ukumbi wa Business Park, uliopo Kijitonyama Dar es Salaam.
Akizungumzia uzinduzi huo Meneja wa Wazee wa Kibega Martin Sospeter, alisema kuwa wameamua kuingiza sokoni Albamu yao kwa aina hiyo ya kufanya uzinduzi ili kila mpenzi wa muziki ajue kama nini wameamua kufanya.
Sospeter alisema katika uzinduzi huo watasindikizwa na Bendi ya  FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma.
Alisema kuwa onesho hilo litaanza mapema ili kila mpenzi aweze kuona burudani kutoka kwa bendi hizo ambazo zitakuwa zikipanda kwa zamu.
“Tumejipanga vizuri katika onesho hili la uzinduzi….ikiwa na hata jamaa zetu FM acadeamia nao, watakuja kamili katika
kuhakikisha tunatoa burudani safi kwa wapenzi wa muziki
watakaoweza kuudhulia siku hii maalum ya kuingiza sokoni
Albamu yetu ya Risasi Kidole” .Alisema Sospeter.

Kwa upande wa marais wa bendi hizo Chalz Baba (Mashujaa) na
Nyosh El Sadat wa FM. kila mmoja aliahidi kutoa burudani nzuri

usiku huo.

Chalz Baba alisema, wamejipanga vya kutosha katika uzinduzi
huo na ndio sabau kubwa ya kuwaomba FM kuwasindikiza ikiwa ni lengo la kuwapa burudani mashabiki wao.
“Tumejipanga sana, kutoa burudani nzuri nay a uhakika kwa
wadau na mashabiki wetu watakaouzulia siku hiyo, kwani
uzinduzi huo sio wa kitoto njooni mjionee wenyewe,”. Alisema
Chalz.
Aidha Chaz aliongeza kuwa, Albam hiyo inatarajiwa kuwa na
nyimbo tisa huku huku akijitamba Raper wake kama Ferguson
kufanya makamuzi ya ajabu siku hiyo.
Naye Nyoshi alisema, kutokana na utu walionao na upendo ndiyo sababu iliyowafnaya kukubali ombi la Mashujaa na kuwasindikiza katika uzinduzi huo, na kudai kuwa siku za usoni hata wao wanatarajia kuwa na uzinduzi wa albam mpya huenda
wakawaalika hata wao.

BENDI YA MASHUJAA KUZINDUA RISASI KIDOLE, FM ACADEMIA KUSINDIKIZA

1Nyoshi El Saadat kiongozi wa bendi ya FM Academia akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Busness Park leo wakati Bendi ya Mashujaa ilipotangaza kuzindua na kupeleka sokoni albam yao ya Risasi Kidole kulia ni Kiongozi wa bendi ya Mashujaa Charles Baba na kushoto ni Queen Suzy na King Dodoo. 2Mnenguaji wa bendi ya Mashujaa Lilian Intanet akionyesha makeke yake wakati wa mkutano huo kwenye ukumbi wa Busness Park.

…………………………………………..
BENDI ya muziki wa Dansi ya FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma, inatarajia kusindikiza uzinduzi wa Albamu ya mpya ya Bendi ya Mashujaa itakayokwenda kwa jila la Risasi Kidole.

Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika Jumamosi ya wiki hii katika ukumbi wa Bissines Park Kijitonyama Jijini Dar es Salaam na kuwakutanisha wanamuziki wanaokubalika kwa sasa katika tasnia hiyo Chaz Baba (Mashujaa) na Nyosh El Sadat wa FM.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Chaz Baba ambaye ni Rais wa Mashujaa alisema, wamejipanga vya kutosha katika uzinduzi huo na ndio sabau kubwa ya kuwaomba FM kuwasindikiza ikiwa ni lengo la kuwapa burudani mashabiki wao.

“Tumejipanga sana, kutoa burudani nzuri nay a uhakika kwa wadau na mashabiki wetu watakaouzulia siku hiyo, kwani uzinduzi huo sio wa kitoto njooni mjionee wenyewe,”alisema Chaz.

Aidha Chaz aliongeza kuwa, albam hiyo inatarajiwa kuwa na nyimbo tisa huku huku akijitamba Raper wake kama Fergason kufanya makamuzi ya ajabu siku hiyo.

Nae Nyosh alisema, kutokana na utu walionao na upendo ndiyo sababu iliyowafnaya kukubali ombi la Mashujaa nkuwasindikiza katika uzinduzi huo, na kudai kuwa siku za usoni hata wao wanatarajia kuwa na uzinduzi wa albam mpya huenda wakawaalika hata wao.

Redd’s Miss Kigamboni Kufanyika Juni 7

imagesNa Mwandishi Wetu

SHINDANO la kumtafuta mrembo wa kitongoji cha Kigamboni mwaka huu “Redd’s Miss Kigamboni 2013″ linatarajiwa kufanyika Ijumaa Juni 8 kwenye ukumbi wa Navy Beach kuanzia saa 2:00 usiku hapa jijini Dar es Salaam.

Tayari warembo wameshaanza mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na shindano hilo ambapo wanajifua kwenye ukumbi wa Break Point (VIP) uliopo Posta hapa jijini.
Akizungumza na gazeti hili jana, Mratibu wa shindano hilo, Somoe Ng’itu, alisema kuwa maandalizi ya shindano hilo yako katika hatua za mwisho na bado wanakaribisha warembo wenye sifa za kushiriki shindano hilo kufika mazoezini kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini.
Mratibu huyo alisema kwamba lengo la kuweka wazi na kuwahamasisha warembo ni kutaka kutoa nafasi kwa wasichana wengi zaidi kujiandikisha na hatimaye kupata mshindi atakayekiwakilisha vyema kitongoji hicho katika mashindano ya ngazi ya Kanda yatakayofanyika baadaye mwezi ujao.
“Tumeshaanza maandalizi na tunawaomba wadau wa sanaa ya urembo wa hapa nchini kujiandaa kusubiri Kigamboni kutoa mrembo wa taifa mwaka huu, tunawashiriki wenye mvuto na sifa za ushindani,” alisema Somoe.

Aliongeza kwamba fomu kwa ajili ya kushiriki shindano hilo zinapatikana bure na warembo wanafanya mazoezi chini ya Blessing Ngowi, ambaye mwaka juzi alishiriki fainali za taifa za Redd’s Miss Tanzania na alitwaa taji la Kanda ya Elimu ya Juu.

Alisema pia makampuni na taasisi mbalimbali zinakaribishwa kudhamini shindano hilo ambalo mwaka jana lilitoa mshindi katika kinyang’anyiro cha Kanda ya Temeke ambaye ni Edda Sylivester.
Edda alifanikiwa kushika nafasi ya tatu kwenye fainali za taifa huku mshindi wa taifa ni Brigitte Alfred ambaye mwaka huu ataenda kupeperusha bendera ya nchi katika mashindano ya dunia.

Wasanii wa kizazi kipya wangarisha tamasha la Airtel yatosha Mbagala


pic 14

Msanii mahiri wa Hi Hop nchini maarufu kama FID Q akikamua katika jukwaa maalum la kuitambulisha huduma kabambe ya Airtel Yatosha katika viwanja vya Zakhem jiini Dar es Salaam na kufanikisha kuwaunganisha watanzania na wakazi wa jijini Dar es salaam kwenye huduma ya Airtel Yatosha.

 pic 6Kikundi cha wakali dansi cha temeke kikitoa burdani Mfululizo katika tamasha la maalum la uzinduzi wa huduma mpya ya Airtel Yatosha lililofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya zakhem -mbagala dar es salaam na kuwavuta maelfu ya watu pic 9wanadada msanii chipukizi wa temeke akitoa burdani kwenye tamasha la Airtel yatosha lililofanyika katika viwanja vya zhakem  – Mbagala Dar es salaam mwishoni mwa wiki hii

 

pic 12

Msanii wa kikundi cha Tip Top Connection Madii akitoa burdani kwenye tamasha la Airtel yatosha lililofanyika katika viwanja vy zhakem  – Mbagala Dar es salaam mwishoni mwa wiki hii

 

pic 13

Wasanii wa kundi la Wanaume Halisi wenye makazi yao Jijini Dar es salaam Temeke wakitoa Burudani Mfululizo katika tamasha la maalum la uzinduzi wa huduma mpya ya Airtel Yatosha lililofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya zakhem -mbagala dar es salaam na kuwavuta maelfu ya watu

 ………………………………………………………..

Burdani ya tamasha la Airtel yatosha katika viwanja vya mbagala zhakem katika siku ya jumamosi na Jumapili zilifana kwa kupambwa na burudani kibao toka kwa wasanii wa kizazi kipya wakiwemo kundi zima la wanaume halisi likiongozwa na sir juma Nature, kiongzi wa tip top connectionMadii, kundi la wakali wa dansi pamoja na wasanii mbalimbali wakiwemo Ney wamitego na Roma Mkatoliki

 

Akizungumzia juu ya tamasha hilo Meneja Uhusiano wa Airtel bwana Jacksoni Mmbando alisema” tumeweza kushuhudia burdani kabambe kutoka kwa vikundi mbalimbali vya wasanii wa kizazi kipya na wasanii chipukizi wa temeke katika viwanja vya zhakem Mbagala.  lakini pia mbali na  burdani wateja wa Airtel wameweza kuunganishwa na huduma ya Airtel yatosha na kupata elimu kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na faida zake, wateja waliweza kujiunga na kusajili namba zao”.

 

“Tunawashukuru watanzania na wateja wetu wote waliojitokeza kwa wingi kupata burdani hii na tunawahaidi kuendelea kuwapa huduma bora na bei nafuu huku tukiendelea kutanua wigo wa mawasiliano nchini aliongeza “Mmbando

 

huduma ya Airtel Yatosha inamuwezesha  mtumiaji wa mtandao wa Airtel kupiga simu kwenda mitandao yote kwa gharama poa ya chini kabisa na hivyo kutokuwa na haja tena ya kubadilisha kadi ya simu pindi anapohitaji kuongea na mtu wa mtandao mwingine.pamoja muda wa maongezi mteja anapata vifurushi vya kutuma ujumbe mfupi na internet na vifurushi hivi vinapatikana kwa siku au kwa wiki, ili kujiunga na huduma hiipiga *149*99# ufurahie huduma poa na ujionee “Airtel Yatosha”

MIAKA 13 YA LADY JAYDEE

Tiketi za sherehe za kuadhimisha miaka 13 ya muziki wa Lady Jaydee zimeshaanza kuuzwa mtaani na huo hapo juu na chini ndio mfano wa jinsi zilivyo ambapo ya juu ni ile ya VIP itakayokuwezesha kupata chakula, nakala ya CD pamoja na huduma maalum ya kinywaji cha kuanzia

Hii hapa chini ni ya kawaida itakayokuwezesha kushiriki onesho, na kushuhudia burudani lukuki zitakazoongizwa na Profesa Jay, TID, Matonya, Grace Matata pamoja na Lady Jaydee mwenyewe na Machozi Band itaonekana jukwaani live siku hiyo.

Tiketi zinapatikaka Shear Illusions-Mlimani City, BM BarberShops-Kinondoni, City Sports Lounge-City Centre, American Nails-Kinondoni, Nyumbani Lounge-Tranic Plaza, na katika Bar za Samaki samaki

AFLEWO KUFANYA TAMASHA KUBWA LA KUSIFU NA KUABUDU JIJINI DAR LEO

Tamasha kubwa la kusifu na kuabudu linatarajia kufanyika leo katika ukumbi wa BCIC mbezi beach kuanzia saa 3 usiku hadi saa 12 alfajiri lenye lengo la kuliombea Taifa Amani, Upendo na uchumi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mlezi wa Aflewo (Africa Let’s Worship) Askofu Fredy Kyara, alisema watanzania wanatakiwa kujitokeza kwa wingi kwani hakuna kiingilio.

Alisema kuwa, tamasha hilo litashirikisha kwaya mbalimbali kutoka makanisa 32 ya madhehebu tofauti katika kusifu na kuabudu.

Askofu kyara alisema, tamasha hilo linafanyika kwa mara ya tatu tangia kuanzishwa hapa nchini mwaka 2011 na kuenea nchi zote za Afrika.

“Tamasha hili limeboreshwa kwa kuongeza muiondombinu ya utendaji kazi, kwa kutanua wigo wa ushirikishwaji wa makanisa mengi,” alisema Kyara.

Aidha matasha mengine ya Aflewo, yanatarajia kufanyika nchi nzima kwa kufanyika kila mkoa, kwa mwaka huu litaanza kufanyika katika mikoa ya Mwanza, Moshi na Zanzibar na hatimaye Afrika yote.

JAHAZI MODERN TAARAB KUUPAMBA MKESHA WA MEI MOSI NDANI YA DAR LIVE LEO

NGOMA AFRICA BAND INATOA SALAMU ZA HERI YA MEI MOSI KWA WADAU WOTE

Front CD Cover

Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya “Ngoma Africa band” aka FFU

yenye makao kule Ujerumani,inawatakiwa kila la heri na fanaka wadau wote

katika kusherehekea siku kuu ya wafanyakazi duniani “Mei Mosi” (1st May).

Pongezi kwa Wafanyakazi wa sekta zote kuanzia wachuuzi,akina mama nitilie,

wafanyakazi viwandani,maofisini,mashambani,wapagazi,wakokota mikokoteni n.k, Kazi ni kazi ! 

Baada ya kazi tufurahie Mei Mosi kwa kupata burudani kamili ya muziki kama vile

“Bongo Tambarare” na Supu ya mawe, n.k at FFU camp

SALAAM KUTOKA KWA MWANAMUZIKI LADY JAYDEE

JideKatika mwaka huu 2013, Inatimia miaka 13 tangu nianze kazi ya muziki.

Nashukuru MUNGU tuko pamoja na pia, nashukuru umma wa Tanzania kwa kuendelea ku support muziki wa Tanzania na kunipa nguvu mimi kama msanii.

Nashukuru vyombo vyote vya habari vinavyoshiriki kikamilifu kukuza na kulinda sanaa ya Tanzania bila kujali maslahi binafsi.

Tumeandaa sherehe kubwa na nzuri ya miaka 13 ya LADY JAYDEE, katika muziki.

Na mdhamini mkuu kwa upande wa media ni East Africa TV.

Sherehe ya miaka 13 ya Lady JayDee katika muziki itaambatana na uzinduzi wa album yangu ya sita inayokwenda kwa jina la NOTHING BUT THE TRUTH ambayo ina jumla ya nyimbo 10.

Katika sherehe hizo pia kutakuwa na show ya nyimbo zote bora za JayDee nikishirikiana na baadhi ya wasanii wenzangu hapa nchini.

Sherehe zitafanyika Ijumaa tarehe 31 May 2013.

Nawakaribisha wote tufurahi pamoja

Na Mungu awabariki

EXTRA BONGO YAZIDI KUWABAMBA MASHABIKI NDANI YA MEEDA SINZA

Mkurugenzi wa Extra bongo Ally Choki akiimba mbele ya mashabiki wake (Hawapo Pichani) ndani ya Ukumbi wa Meeda sinza jana Usiku wakati bendi yake ilipokuwa ikiburudisha pande pande hizo
Kushoto ni mwimbaji mahiri wa bendi ya Extra Bongo Athanas akiwa na Mwimbaji pekee wa kike wa bendi hiyo Khadija Mnoga a.k.a “Kimobitel” ambaye anatamba kwa sasa na wimbo wake wa “Mgeni” wakishoo luv mbele ya kamera yetu ndani ya ukumbi wa Meeda Sinza jana usiku wakati Bendi yao ilipokuwa ikitumbuiza pande hizo.
Kushoto ni mmoja wa marapa bora wa muziki wa dansi Totoo Ze Bingwa akirap ndani ya Meeda sinza wakati Bendi anayopigia mzigo Extra Bongo ilipokuwa ikitumbuiza pande hizo na kulia ni Banza Stone a.k.a Generale akimpa big up.
Maua ya Extra Bongo mzigoni
Wakata nyonga maarufu kwa sasa wa Extra bongo wakiongozwa na nyamwela wakiwapagawisha mashabiki waliohudhuria shoo hiyo ndani ya Meeda Sinza jana usiku
Waimbji bora wa Extra bongo kulia ni Rogert Hega a.k.a Katapila wakiimba ndani ya Meeda Sinza jana usiku
Rapa bora wa Extra bongo Kabatano (Kulia) akigani moja ya jimbo zao bora huku akipewa sapoti na nguli wa muziki wa dansi Banza Stone mwana masanja wakati bendi hiyo ilipokuwa ikitumbuiza maeneo ya Sinza katika ukumbi wa Meeda jana usiku.

NYAMWELA ASHUSHA MBILI KALI, NI “MANENO” NA “DUVELEE”

1BHassan Mussa aka Nyamwela Kiongozi wa Wanenguaji katika bendi ya Extra Bongo amekuja na nyimbo mpya mbili zinazokwenda kwa majini ya Maneno na Duvelee ambazo amewashirikisha wasanii kutoka kundi la THT la jijini Dar es salaam wasanii hao ni Amini Mwinyi Mkuu na Muky Kibega.

Nyimbo hizo zimerekodiwa katika studio za Kili Record kwa Producer C9 zilizoko Kinondoni jijini Dar es salaam , Akizungumzia nyimbo hizo Nyamwela amesema zimerekodiwa katika kiwango cha hali ya juu na tayari nyimbo moja ya Maneno imeshaanza kupigwa katika vituo mbalimbali vya Redio na Televisheni na inafanya vizuri sana

Huu ni mwendelezo wa kurekodi nyimbo zake ambapo anatarajia kutoa albam yake hapo baadae inatakyokuwa na nyimbo nane ambapo anasema atashirikisha wanamuziki kutoka nchi mbalimbali za Afrika Mashariki, na kwa sasa ndiyo anaaza kufanya mawasiliano na wanamuziki hao.

Fullshangweblog na kikosi kazi chake inamtakiwa mwanamuziki huyo maandalizi mema ili aweze kuleta kitu tofauti katika anga za muziki wa dansi.

NGOMA AFRIKA BAND INAWATAKIA HERI YA MIAKA 49 YA MUUNGANO WA TANZANIA

Front CD Cover

Bendi ya muziki wa dansi “Ngoma Africa Band” a.k.a FFU yenye maskani nchini  Ujerumani

inawatakia kila la heri na fanaka ya MIAKA 49 YA MUUNGANO wa jamuhuri ya TANZANIA, watanzania wote popote walipo.
Muungano wetu wa bara na visiwani ni muungano wa undugu wa damu.
Mungu Ibariki Tanzania,
Mungu Ubariki Muungano wetu.

KING KIKII, MSONDO NGOMA NA KHADIJA KOPA JUKWAA MOJA SHEKINAH GARDEN.

muzikiKundi zima la Capital Wazee Sugu wakiwa chini ya bwana mkubwa Kikumbi Mwanza Mpango King Kikii watasahambulia ndani ya ukumbi wa Shekinah Garden mbezi makonde inayotazamana na kituo cha mafuta cha Engen ijumaa ya tarehe tatu mwezi wa tano mwaka huu ( 03/05/2013 ).

Akiongea na gazeti hili, afisa masoko wa kampuni ya D & I Entertainment Peter Mwendapole amesema mbali ya King Kikii, pia usiku huo watashambulia jukwaa moja na magwiji wa muziki wa dansi nchini Msondo Ngoma Music Band ” baba ya muziki” ambao siku hiyo watamtambulisha kwa mashabiki wao mwanamuziki mkongwe mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni Shaaban Dede mwana aliyerejea nyumbani.

Aidha Mwendapole amesema ili kuikamilisha burudani hii ya aina yake na inayofanyika kwa mara ya kwanza ndani ya Shekinah Garden mbezi makonde, malkia wa mipasho Afrika Mashariki na Kati Bi Khadija Omar Kopa naye atawakonga mashabiki watakaofika kwa miondoko yake ya taarabu na hasa kibao chake kinachotamba hivi sasa cha mjini chuo kikuu.

Mwendapole amewataka mashabiki kufika kwa wingi kwani hii ni buruda ni ya aina yake ambayo itakuwa na vionjo vya kila aina, na kila atakayefika atafurahi kwani makundi yote haya yatatumbuiza kwa utaratibu maalum ili kila mmoja atii kiu yake.

Kuhusu ulinzi na usalama, amesema yote hayo yameimarishwa

TIMU KUTOKA AFRIKA MASHARIKI YAINGIA NUSU FAINALI GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™

Episode 4 winners

ROBO FAINALI – EP1 winners & hype EP 2

 *Washiriki bora kutoka Afrika wataingia katika robo fainali ya pili kuwania kufuzu nafasi ya nusu fainali*

Aprili 25, 2013, Dar es Salaam; Robo fainali ya kwanza ya Pan-African GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE™ ilifanyika jana usiku ambapo mashabiki wa Afrika masharik i walikuwa wakishangilia timu za nchi zao.  Washiriki mahiri kutoka  Cameroon,Ghana,Kenya ,Uganda na Tanzania walikutana uso kwa uso ili kushindania dola za kimarekani  250,000 na kutwaa ubigwa wa Pan-African.

 Timu ya Afrika mashariki iliyoweza kufuzu kuingia nusu fainali kutoka kipindi cha kwanza ni Francis Ngigi na Kepha Kimani kutoka Kenya. Japokuwa hawakufanikiwa kufikia hatua ya mwisho ya ukuta wa pesa wa GUINNESS lakini walifanikiwa kuingia nusu fainali. Emerand Tchouta(24) na Abdul Salam(25) kutoka Cameroon walionesha kuwa wao ni wachezaji wazuri ambapo walifanikiwa kufikia hatua ya mwisho ya ukuta wa pesa. Katika hatua ya mwisho, ambapo walifanikiwa kujipatia dola za kimarekani 5,000 kuongezea walizokuwa nazo waliposhinda mwanzoni dola 1,500.

 Timu zitahitaji kuwa na umoja na kujiamini ili kuweza kujiandaa kwa hatua zinazofuata. Timu moja kutoka Dar es Salaam Tanzania wataingia uwanjani wiki ijayo itakua na Daniel Msekwa(21) na Mwalimu Akida Hamad(26).

 Meneja wa kinywaji cha Guinness, Davis Kambi alisema, “Robo fainali ya GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE ilisisimua katika runinga ambapo Francis na Kepha walifanikiwa kuiwakilisha Afrika mashariki katika nusu fainali. Timu kutoka Kenya na Cameroon zimefuzu kuingia  nusu fainali, wiki ijayo washiriki wengine watakutana ili kujua ni nani atashinda na kufuzu hatua ya nusu fainali. Nawatakia wote kila la heri”.

 Timu nne zitakazo shiriki wiki ijayo kutafuta nafasi ya kuingia nafasi ya nusu fainali ni:

 Watakao kuwa na jezi za bluu ni Daniel Msekwa (21) ambaye ni kichwa cha timu, na mwenzie Mwalimu

  • Akida Hamad (26). Walifanikiwa kujishindia  dola za kimarekani 5,500 katika mashindano ya Afrika Mashariki hivyo wana nafasi kubwa ya kufuzu nusu fainali.
  • Wenye jezi nyekundu watakuwa wakenya, kocha wa vijana Kenneth Kamau(23) na dereva Wills Ogutu (30) wote kutoka Nairobi. Ingawawa hawakufanya vizuri sana katika sehemu zilizopita lakini wanaweza kufanya vizuri wiki ijayo wakijipanga vizuri.
  • Archille Stephanie na Martial Toubou kutoka Douala Cameroon watavaa jezi za kijani. Archille atajibu maswali wakati Martial ataonesha uwezo wake wa kucheza soka. Walifanikiwa kujishindaia dola 4,000 katika sehemu zilizopita.
  •  Jezi nyeusi watakuwa ni Dennis Nyaku(25) na Francis Nyarko(27)  wote kutoka Ho Ghana ambapo walifanikiwa kujishindia dola 1,500 katika mashindano ya kitaifa. Dennis atakuwa kichwa wakati Francis atakuwa  akionesha uwezo wake wa kusakata kabumbu na kuweka chini vifaa vya uchoraji.

 Wapenzi wa kipindi hiki cha Guiness football challenge barani Afrika wanakumbushwa kwamba nao wanaweza kushiriki kwa kufuatilia kwa karibu.   Wanaweza kufanya hivyo kwa kujisajili  bure kabisa katika tovuti ya m.guinnessvip.com kwa kupitia simu yako ya mkononi.

 Robo fainali ya pili ya Pan-African itaoneshwa katika televisheni za ITV na Clouds TV kila jumatano saa 3:15 ITV na Clouds TV saa 2:15 usiku.

 Hakikisha kuufwatilia ukurasa wa facebook wa GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE kwa habari mbalimbali-www.facebook.com/guinnesstanzania

 GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE, ni kipindi cha mchezo wa soka kinachotayarishwa na kampuni ya kimataifa ya Endemol.  Usikose kuangalia na kufuatialia kipindi hiki katika runinga yako kupitia televisheni za ITV na Clouds TV kila siku ya Jumatano usiku.

 Usisahau kuwa na chupa ya bia uipendayo ya  Guiness wakati unaangalia kipindi hiki. 

 Tafadhali kunywa kistaarabu- Hairuhusiwi kuuzwa kwa wale wenye umri chini ya miaka 18.